Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro akizunngumza wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) uliyofanyika katika hoteli ya Tanga Beach Resort, Desemba 19, 2022 jijini Tanga.
 
 =======   ======   =======
 
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) wametakiwa kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi kwa lugha rahisi ili kuwezesha jamii kufahamu zaidi umuhimu wa bima hapa nchini.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa tatu wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) uliyofanyika katika hoteli ya Tanga Beach Resort, Desemba 19, 2022 jijini Tanga,  Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro amesema kuwa ni wajibu sasa wa watumishi wa bima kuwa wabunifu katika utoaji wa elimu ili kuhamasisha watu wengi wanajiunga ili kusaidia jamii lakini pia kuongeza mapato ya nchi.

''Niwakati sasa kufikiria kuendesha kazi zenu kidigitali ili kuwezesha mambo mengi zaidi kwenda kwa urahisi, kwani Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan nia yake kubwa ni kuona taasisi nyingi za kiserikali zikitekeleza majukumu yao kidigitali zaidi'' Alisema Dkt. Ndumbaro.

Aidha Dkt. Ndumbaro amewataka watumishi kuweka usiri zaidi katika kutoa huduma ili kuwepo usiri baina na mtumishi na mteja Sambamba na kuzingatia uzalendo na kufanya kazi kwa juhudi na maarifa.

Kwa upande wake Kamishina wa Bima Tanzania, Baghayo Saqware amebainisha changamoto mbalimbali wanazo kutana nazo wakati wa utekelezaji wa majukumu yao kwenye sekta ya bima ambayo ni kutokuwepo kwa sera ya bima hapa nchini pamoja na kutokuwepo kwa bodi ya taifa ya bima na hivyo kupelekea mambo mengi ya kiutumishi kukwama.
Kamishna wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware akizunngumza wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) uliyofanyika katika hoteli ya Tanga Beach Resort, Desemba 19, 2022 jijini Tanga.
Naibu Kamishna wa Bima Tanzania na Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), Khadija Said akizunngumza wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) uliyofanyika katika hoteli ya Tanga Beach Resort, Desemba 19, 2022 jijini Tanga.
Baadhi ya Wafanyakakazi wa Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA) wakiwa kwenye Mkutano huo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...