Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV - Ikungi
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Daniel Chongolo amekishauri Kituo cha Uwekezaji Tanzania ( TIC) kujenga utamaduni wa kuwatembelea wawekezaji waliowasajili ili kuwatatulia changamoto walizokuwa nazo ili kufikia malengo ya Ilani ya CCM katika kuboresha mazingira rafiki kwa wawekezaji
Chongolo ametoa ushauri huo leo Februari 28,2023 alipotembelea Shamba la Kampuni ya Al Fardaws ya kutoka nchini Jordan, lililopo wilayani Ikungi mkoani Singida ambapo ameshangazwa na mwekezaji huyo ambae ameomba huduma ya umeme kwa zaidi ya miezi minne ili awekeze kwenye kilimo cha alizeti.
Kutokana na malalamiko ya kampuni hiyo,Chongolo ametoa mwezi mmoja kwa Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) kufilkisha miundombinu ya umeme kwa mwekezaji huyo anayetarajia kuwekeza kwenye zao la alizeti.
Awali Mhandisi wa Miundombinu wa Kampuni ya Al Fardaws Edward Nambiza
amesema wanatarajia kuwekeza zaidi ya Sh.bilioni 12.9 katika kilimo cha alizeti ikiwa ni pamoja na kuzalisha mbegu bora za alizeti na kukamua mafuta ya kula.
Kwa upande wake Meneje wa TANESCO Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Mhandisi Angelo Maskini amesema wanatarajia kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya umeme kufikisha katika eneo la mwekezaji Aprili mwaka huu
Katibu Mkuu Chongolo anaendelea na ziara yake mkoani Singida akiwa ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,Itikadi na Uenezi Sophia Mjema pamoja na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Oganaizesheni Issa Haji Gavu.
KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Daniel Chongolo amekishauri Kituo cha Uwekezaji Tanzania ( TIC) kujenga utamaduni wa kuwatembelea wawekezaji waliowasajili ili kuwatatulia changamoto walizokuwa nazo ili kufikia malengo ya Ilani ya CCM katika kuboresha mazingira rafiki kwa wawekezaji
Chongolo ametoa ushauri huo leo Februari 28,2023 alipotembelea Shamba la Kampuni ya Al Fardaws ya kutoka nchini Jordan, lililopo wilayani Ikungi mkoani Singida ambapo ameshangazwa na mwekezaji huyo ambae ameomba huduma ya umeme kwa zaidi ya miezi minne ili awekeze kwenye kilimo cha alizeti.
Kutokana na malalamiko ya kampuni hiyo,Chongolo ametoa mwezi mmoja kwa Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) kufilkisha miundombinu ya umeme kwa mwekezaji huyo anayetarajia kuwekeza kwenye zao la alizeti.
Awali Mhandisi wa Miundombinu wa Kampuni ya Al Fardaws Edward Nambiza
amesema wanatarajia kuwekeza zaidi ya Sh.bilioni 12.9 katika kilimo cha alizeti ikiwa ni pamoja na kuzalisha mbegu bora za alizeti na kukamua mafuta ya kula.
Kwa upande wake Meneje wa TANESCO Wilaya ya Ikungi mkoani Singida Mhandisi Angelo Maskini amesema wanatarajia kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya umeme kufikisha katika eneo la mwekezaji Aprili mwaka huu
Katibu Mkuu Chongolo anaendelea na ziara yake mkoani Singida akiwa ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,Itikadi na Uenezi Sophia Mjema pamoja na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Oganaizesheni Issa Haji Gavu.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...