MAMLAKA ya Hali ya Hewa (nchini TMA) imetoa angalizo la uwepo wa mvua kubwa siku moja ya kesho Machi 3, 2023 kwa mikoa sita na upepo mkali kwa siku mbili, kesho na kesho kutwa Machi 4,2023 katika mikoa ya Lindi na Mtwara.

Katika taarifa iliyotolewa na TMA leo Machi 2, 2023  ilitoa angalizo hilo la mvua kubwa katika mikoa ya Mara, Simiyu, Shinyanga, Mwanza, Dodoma na Singida, pia uwepo wa upepo mkali unaofikia kilometa 40 kwa saa maeneo ya pwani ya Kusini mwa bahari, mikoa ya Lindi na Mtwara .

Athari zinazoweza kujitokeza ni baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshwaji wa shughuli za uchumi na usafirishaji na pia kuathirika kwa baadhi ya shughuli za uvuvi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...