Na.Mwandishi wetu, Arusha

Mkuu wa mkoa wa Arusha ,John Mongela amezitaka taasisi mbalimbali kuhakikisha kunakuwepo na uwiano sawa wa jinsia kati ya wanaume na wanawake ili kuwepo kwa usawa mahala pa kazi.

Ameyasema hayo jijini Arusha wakati akizungumza na wadau mbalimbali wa benki ya CRDB walipokutana katika chakula cha jioni katika kilichokutanisha wanawake wadau wa benki hiyo Jijini Arusha.

Mongela alisema kuwa,hakuna agenda ya maendeleo inayoweza kufikiwa bila kukabiliana na changamoto zinazowakabili wanawake na kuweza kupatiwa ufumbuzi kwani wanawake ni jeshi kubwa na wana mchango mkubwa sana katika jamii.

"Naipongeza sana benki ya CRDB kwa namna ambavyo imejitahidi kukumbatia usawa wa kijinsia na kuweza kuwajengea uwezo wa kuwezesha wafanyakazi wa kike kwani nameambiwa asilimia 47 ya wanawake ni wafanyakazi wa benki hii huku wanaume wakiwa ni asilimia 53 na juhudi zaidi zinaendelea za kuongeza idadi ya wanawake ni mfano mzuri wa kuigwa na taasisi zingine. "amesema Mongela.

Kwa upande wake Afisa mkuu mwendeshaji wa benki ya CRDB ,Bruce Bwile amesema kuwa,kumekuwepo na ongezeko la asilimia 3 la idadi ya wanawake katika benki hiyo tofauti na miaka ya nyuma na kuweza kuleta dhana nzima ya usawa wa kijinsia mahala pa kazi.

Amesema kuwa, benki hiyo ina programu ya kuweza kuwajengea uwezo wanawake katika ngazi ya kati ambapo wanawake mia moja wanashiriki katika programu hiyo huku lengo kuu ni kufikia idadi zaidi ya mia mbili ili kuleta usawa wa kijinsia.

"Kupitia kitengo cha biashara benki imeweza kufikia wanawake wadogo na wa kati kwa kutoa kiasi cha shs 67.3 bilioni hadi desemba 2022 ambapo jumla ya wanawake 3,122 wameweza kufikiwa katika mikoa yote Tanzania."amesema Bruce.

Aidha amesema kuwa, benki hiyo imeendelea kusisitiza jitihada zake katika maswala ya kijinsia na kukumbatia usawa katika jamii kwa ujumla ili kuondokana na changamoto ya kupigania usawa mahala pa kazi penye uwiano. 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...