Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV


Wekundu wa Msimbazi, Simba SC wamefanikiwa kukwea hadi nafasi ya pili katika Kundi C la Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL) baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Vipers SC ya Uganda kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo wa nne wa Kundi hilo C, Wekundu wa Msimbazi walianza vyema mchezo huo kuwasakama Cobra wa Uganda, ambapo dakika ya 45+1’ Kiungo Mshambuliaji, Clatous Chama alipachika bao hilo pekee baada ya kuwadanganya Walinzi wa Vipers SC na kupiga ‘shuti’ kali lililompita Golikipa Alfred Mukereza.

Kwa matokeo hayo, Simba SC wamefufua matumaini makubwa ya kufuzu hatua ya Robo Fainali ya Michuano hiyo baada ya kufikisha alama sita katika Kundi hilo lenye timu za Raja Casablanca ya Morocco, Horoya AC ya Guinea na Vipers SC.

Raja AC wanaendelea kuongoza Kundi wakiwa na alama 12 huku Simba SC wakiwa nafasi ya pili wakiwa na alama sita, Horoya AC wana alama nne huku Vipers wakiwa na alama moja pekee.

Machi 18, 2023 Simba SC watakuwa na kibarua dhidi ya Horoya AC kwenye uwanja wa nyumbani wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam, huku Raja Casablanca watakuwa ugenini dhidi ya wenyeji Vipers SC kwenye dimba la St. Mary’s, Kitende mjini Entebbe nchini Uganda.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...