Na Shamimu Nyaki
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Julai 2, 2023 ametembelea eneo lililotengwa na Halmashauri ya Mji Njombe kwa ajili ya Viwanja vya Michezo.
Mhe. Chana ameipongeza Halmashauri hiyo kwa hatua hiyo ambapo amesema timu ya Wataalam kutoka wizara hiyo watafika kukagua na kutoa ushauri wa kitaalam kabla ya ujenzi huo kuanza.
Ametoa wito kwa Halmashauri zingine kuiga mfano huo ili miundombinu ya michezo iongezeke na kutoa fursa kwa wananchi kushiriki michezo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...