Na Mwandishi wetu, Lindi

MKOA wa Lindi unatarajia kufanya maonyesho ya madini na fursa za uwekezaji yatakayohusisha wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Mkoa wa Lindi yanapatikana na kuchimbwa madini ya aina mbalimbali ikiwemo dhahabu, nickel, ganeti ya kijani, manganese ore, marble, gypsum na ulanga (kinywe).

Katibu Tawala wa mkoa wa Lindi, (RAS) Zuwena Omary Jiri amesema maonyesho hayo yatafanyika kwa muda wa siku sita wilayani Ruangwa Agosti 21 hadi 26.

RAS Zuwena amesema tamasha na maonyesho hayo yatahusisha fursa mbalimbali zinazopatikana mkoani Lindi ikiwemo madini, utalii, kilimo, mifugo na uvuvi.

"Lengo ni kuangazia fursa zilizopo mkoani Lindi na kujenga jukwaa ambalo wadau wa sekta ya madini na sekta shirikishi watapata nafasi ya kujadiliana, kubadilishana uzoefu na kutangaza fursa zilizopo mkoani Lindi," amesema RAS Zuwena.

Amesema wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo wafanyabiashara, wawekezaji na wapenda maendeleo tofauti kutoka ndani na nje ya nchi watashiriki tamasha na maonyesho hayo.

Amesema kauli mbiu ya maonyesho hayo ni wekeza Lindi kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo ya jamii.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Zuwena Omary Jiri akizungumza ofisini kwake juu ya maonyesho ya madini na fursa za uchumi yatakayofanyika Agosti 21 hadi 26 Mjini Ruangwa yenye kauli mbiu ya wekeza Lindi kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo ya jamii

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...