Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Chalinze Islamic Modern, Bagamoyo Mkoani Pwani, wameiomba Serikali kuelekeza nguvu katika ujenzi wa maabara za masomo ya sayansi kuanzia elimu ya msingi ili kuwapa uelewa wa masomo ya sayansi kwa vitendo .

Wameeleza, zipo Shule za msingi ambazo zina wanafunzi wenye uwezo wa kufanya sayansi ya vitendo changamoto ikiwa ni ukosefu wa vifaa.

Ushauri huo umetolewa na wanafunzi wa darasa la sita katika shule Msingi Chalinze , Islamic Modern baada ya wanafunzi hao kumfanyia upasuaji mnyama Sungura na kumrejesha hai.

Wanafunzi hao walieleza,licha ya masomo ya kawaida pia wanapatiwa mafunzo ya sayansi, na kwamba tukio la hilo ni kiumbe wa tatu kumfanyia upasuaji huo.

Wanafunzi Lattifa Bakari na Mussa Swed wa darasa la sita walieleza,wamefanikiwa kuwafanyia upasuaji viumbe hao ambao wote wamefanikiwa na wapo hai.

Nae Swed alisema, Tanzania ina uhaba wa madaktari bingwa hivyo kwa kuandaa wanafunzi wa sayansi kuanzia ngazi ya msingi itakuwa na uwekezaji mkubwa wa kizazi cha madaktari hao.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu Seif Hashimu alisema ,shule yao imeamua kuwapatia masomo ya sayansi wanafunzi wao kwa lengo la kuwajengea uwezo ili waendapo sekondari wasiwe wageni kwenye somo hilo.

Mwalimu Issa Machame alisema kuwa wanafundisha masomo hayo kwa lengo la kuwapatia taaluma hiyo wanafunzi wanaoanzia elimu ya msingi, ili hata watakapoingia sekondari wakikutana na masomo hayo wasiyaone mageni.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...