Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Shirikisho la Soka nchini Tanzania (TFF) limetoa ufafanuzi kwa umma kuhusu adhabu ya kufungiwa miaka saba Dkt. Damas Ndumbaro ambaye ni Waziri wa sasa wa Utamaduni, Sanaa na Michezo baada ya kuwepo minong’ono kuhusu adhabu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho hilo, imetanabaisha kuwa Dkt. Ndumbaro alifungiwa miaka saba na uongozi wa TFF uliopita, hata hivyo Dkt. Ndumbaro hakukubaliana na uamuzi huo na alikata rufaa kwenye Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya Shirikisho hilo kupinga adhabu hiyo.

“Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF chini ya uongozi wa sasa ilisikiliza rufani hiyo mwaka 2017 ambapo Waziri Dkt. Ndumbaro alishinda, hivyo kuondolewa adhabu ya kufungiwa,” imeeleza taarifa hiyo ya TFF.

Hata hivyo, taarifa hiyo imetaarifu umma kuwa kwa sasa Waziri Dkt. Damas Ndumbaro ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rufani ya Leseni za Klabu ya Shirikisho la Soka nchini (TFF).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...