NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV
KLABU ya Simba imefanikiwa kutoka sare ya 2-2 katika uwanja wake wa nyumbani dhidi ya timu ya Al Ahly ya nchini Misri katika mchezo wa robo fainali Michuano ya African Football League.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa wa ufunguzi, Al Ahly ilifanikiwa kupata bao kipindi cha kwanza kabla ya mapumziko kupitia kwa mshambuliaji wao Reda Slim na kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa 1-0.
Simba Sc ilirudi kipindi cha pili wakiwa na hali mpya kwani walitawala mchezo na kufanikiwa kupata bao la kusawazisha kupitia kwa Kibu Denis dakika ya 53 ya Mchezo.
Kocha wa Simba Sc alifanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji kipindi hicho cha pili, mabadiliko ambayo yalizaa matunda kwani baada ya kuingia Sadio Kanoute alifanikiwa kupachika bao zuri na kuwafanya Simba kuwa mbele 2-1.
Dakika tatu baadae Al Ahly walisawazisha kupitia kwa nyota wao Karhaba dakika ya 63 ya mchezo.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...