Pamela Mollel, Arusha

Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa jukwaa la majaji wakuu ukanda wa nchi za kusini na Mashariki mwa Afrika(SEAJAA) utakaofanyika oktoba 23 hadi 27 jijini Arusha

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha, Mwenyekiti wa Chama cha hicho, Profesa Elisante ole Gabriel ambaye ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, amesema maandalizi ya kikao cha watendaji hao yanaendelea vizur  na kuwa Mkutano huo utakaofunguliwa na Rais Dkt Samia Hassan Suluhu.

Profesa Gabriel amesema katika  kikao hicho tayari nchi 13 zimejiunga na chama hicho huku jitihada za nchi nyingine tatu  kujiunga na chama hicho zikiendelea na badae idadi ya wanachama wengine itaongezeka kufika Afrika nzima

Aliongeza kuwa malengo ya chama hicho ni kubadilishana uzoefu katika nchi wanachama ikiwemo jinsi gani wakuu wa mahakama wanavyoendesha shughuli za mahakama

Amesema kikao kazi hicho kitajadili mambo mbalimbali kwani watendaji wakuu wanawashauri majaji wakuu katika masuala ya miundombinu, rasilimali za watu na masuala ya fedha

Pia kitakuwa na ajenda za marekebisho ya katiba ya chama hicho ikiwemo uboreshaji wa vyanzo vya fedha, uboreshaji wa mtandao wa chama hicho, mikakati ya masuala ya fedha huku nchi 13 za umoja huo zitakazoshiriki mkutano huo ambazo ni Angola, Botswana, Lesotho, Zanzibar, Shelisheli, Zimbabwe, Malawi, Msumbiji, Eswatini, Zambia, Namibia na mwenyeji Tanzania.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...