NA K-VIS BLOG, DODOMA

MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma,  amewataka wafanyakazi wa Mfuko huo kudumisha Ushirikiano ili kuendelea kutoa huduma bora kwa wanachama na wadau wa Mfuko wakiwemo waajiri, wanufaika na wafanyakazi pale watakapopata ajali ama kuugua kutokana na kazi.

Dkt. Mduma ameyasema hayo Oktoba 4, 2023 kwenye ofisi za WCF, jijini Dodoma, wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya WCF ya wiki ya Kimataifa ya Huduma kwa Wateja iliyoanza Oktoba 2, 2023.

Maadhimisho ya wiki ya Huduma kwa wateja ni tukio la kimataifa ambalo linaangazia umuhimu wa huduma kwa wateja na watu wanaotoa huduma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kwa watoa huduma na wateja, ambapo mwaka huu wa 2023 imebeba kaulimbiu ya “Ushirikiano kwa Huduma Bora.”

“WCF chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu tumekuwa tukifanya kazi na kutoa huduma kwa ushirikiano kama kauli mbiu ya mwaka huu inavyosema, kuanzia ngazi ya mkurugenzi mkuu, Menejimenti mpaka kwa afisa wa kawaida.” Amesema na kuongeza..  Katika maisha yetu tunafurahia kufanya kazi na kutoa huduma kwa pamoja   tena kwa ushirikiano mkubwa bila kujali yupi ni wa ngazi ipi.” Amesisitiza Mkurugenzi Mkuu.

Amesema kama ilivyo desturi ya wafanyakazi wa WCF, kwa kauli mbiu ya mwaka huu “TEAM SERVICE” au HUDUMA KWA USHIRIKIANO, inakumbusha umuhimu wa kufanya kazi kwa kutambua ushirikiano ambao utawezesha kutoa huduma bora zaidi kwa wateja na wadau bila kusubiri wale walio katika madawati ya mapokezi.

Katika ofisi za WCF za Dar es Salaam, Temeke, Ilala, Arusha, Mbeya, Mwanza, Geita na Morogoro, wakuu wa ofisi hizo wamewahimiza wafanyakazi wenzao kuhakikisha wanadumisha ushirikiano baina yao wenyewe lakini na wanaowahudumia ili kudumisha taswira nzuri iliyopo ya Mfuko huo.

MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma,  akimuhudumia mteja (Mwnaachama) wa Mfuko huo kwenye ofisi za WCF, jijini Dodoma Oktoba 4, 2023.










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...