Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda amekutana na Chama cha Wakandarasi wanawake Nchini na kufanya nao Kikao katika Ofisi za UWT Makao Makuu Dodoma .
Akizungumza leo katika Kikao hicho Mwenyekiti Chatanda amewapongeza wakandarasi hao wanawake ambao wanamuunga Mkono kwa asilimia 100 Mh Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanya kazi za Ujenzi mbalimbali kwenye miradi Nchini.
Mwenyekiti Chatanda amewaomba wanawake wa Chama cha wakandarasi Nchini kuendelea kumuunga Mkono Mh Rais kwa kufanya kazi ya Ujenzi kwa weredi Mkubwa ili fedha ambazo zimeletwa katika Maeneo tofauti ya Nchi basi yatumike kikamilifu.
Mwenyekiti Chatanda amesema najua wanawake jinsi mkipewa kazi mnavyofanya kwa weredi Mkubwa basi msiniangushe Mwanamke mwenzetu mwendeni na juhudi hiyohiyo katika kutimiza wajibu wenu wa kazi pindi mnapoaminiwa kufanya kazi sehemu mbalimbali ya Nchi yetu fanyeni kwa weredi .
"Najua Chama chenu kipo imara katika kuwasaidia wanawake wakandarasi Nchini naombeni ushirikiano mnaondelea kuutoa kwa wanawake wengine muendelee nao ili Serikali hiendelee kujua jinsi wanawake mnavyofanya kazi kubwa katika Nchi "
Hata hivyo Mwenyekiti Chatanda ametoa Rai kwa Chama hicho cha wakandarasi Nchini kuwasaidia wanawake wa chini katika kuunganisha kuingia katika Chama hicho ili waweze kujiinua kiuchumi.
Mwenyekiti Chatanda amesema sisi kama wanawake wa UWT Taifa tutawapa ushirikiano mzuri katika kufanikisha kazi zenu kwa kuwa Mh Rais anawapenda wanawake kwa kuwa nyie ndio mnaoinua uchumi wa Tanzania .
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...