Na Pamela Mollel,Longido

Viongozi wa dini na mila  mkoani Arusha,wamefanya sala maalum kumwombea Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, kwa kuwa weka mazingira wezeshi kwa wachimbaji madini kufanya shughuli zao.

Kutokana na mazingira hayo kuwa mazuri na wezeshi umewasaidia wachimbaji wazawa akiwamo Bilionea Sendeu Laizer,kuwasaidia wananchi kujikwamua kiuchumi.

Sendeu  Laizer,akizungumza na wanachi zaidi ya elfu moja katika hafla hiyo,iliyofanyika katika Kijiji cha Mundarara,kilichopo wilayani Longido,alisema amani iliyoko Tanzania hasa wilayani humo imechangia wachimbaji kufanya shughuli zao kwa uhuru.

"Sisi wawekezaji katika Wilaya ya Longido tunafanya shughuli zetu bila kuwapo kwa usumbufu wa aina yoyote kutokana na mazingira rafiki yaliyowekwa na serikali chini ya uongozi wa Rais Samia kuvutia wawekezaji,"alisema.





 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...