Na, Brown Jonas - WUSM
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali
Mwinyi ameridhia ushauri wa kuubadili jina uwanja wa Amaan na kuitwa
“New Amaan Sports Complex” wakati wa uzinduzi wa awamu ya tatu ya
Uwanja huo uliofanyika Desemba 27, 20203 kisiwani humo
Rais
Mwinyi ameridhia ushauri huo uliotolewa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na
Michezo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro alipokua akitoa salamu za Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"Kutokana na maboresho makubwa
yaliyofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kuufanya uwanja huu
kuwa wa kisasa na wenye viwango vya Kimataifa, mimi naomba niubadilishe
jina uitwe New Amaan Stadium" alisema Dkt. Ndumbaro.
Hafla ya
Uzinduzi wa Uwanja huo ilipambwa na Burudani mbalimbali ikiwemo Muziki
na mechi ya mpira wa miguu ya kirafiki baina ya Timu ya Mpira wa Miguu
ya Tanzania Bara "Kilimanjaro Stars" na Timu ya Mpira wa Miguu ya
Zanzibar "Zanzibar Heros ambazo zilitoka sare ya bila kufungana.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...