NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dk.Dotto Biteko amesema kanuni ya kuwataka wafanyabiashara wa mafuta kununua mafuta yao katika kituo cha GBP Tanga zimekamilika na zitaanza kutumika rasmi Februari mwaka huu.

Dk.Biteko ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baaa ya kutemebela mradi wa bomba la mafuta wa Afrika ya Mashariki (EACOP), Flow Meter inayomilikiwa na Mamlaka ya Bandari na baadaye kituo cha kuhifadhi mafuta cha GBP.

"Kanuni zilirekebishwa mwezi uliopita na wafanyabiashara wote wa Kanda ya Kaskazini waache kwenda Dar es Salaam kununua mafuta hayo kwani ndiko kunasababisha kuongeza bei ya mafuta na muda.

" Nia ya Serikali ni kuhakikisha wafanyabiashara wa mafuta Kanda ya Kusini wanachukua mafuta yao Mtwara na wale wa Kaskazini na hata wale ambao wanatoka nchi jirani ya Kenya kuchukulia mafuta mkoani Tanga, "amesema.

Dk.Biteko ametoa mwito kwa taasisi za Serikali, Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA), EWURA, Wakala wa Uagizaji Mafuta na Shirika la Viwango (TBS) zote kwenda kasi ili kutekeleza agizo hilo ili taratibu za kushusha mafuta Tanga zianze mara moja.

Akizungumzia kuhusu Bandari ya Tanga Dk. Biteko amesema shughuli za badari zinatarajiwa kungezeka kutokana na Serikali kusaini kanuni inayoelekeza wanunuzi wa mafuta wa Kanda ya Kaskazini kununua bidhaa hiyo Tanga,

Dk Biteko amesema Serikali inathamini uwekezaji unaofanywa na kampuni ya GBP namipango yake ya kuinua uwekezaji huo na iko tayari kuhakikisha kuwa uwekezaji huuo hauna hasara,

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Gulf Bulk Petroleum (GBP) ya Tanga Badari Seif Masoud amesema kampuni hiyo iliyoanza shughuli zake mwaka 2001 sasa hivi inauwezo kwa kuhudumia malori 12 kwa mpigo kwa muda wadakika 30 na mabehewa 20 kwa muda wa dakika 45.

Ameongeza kampuni hiyo ambayo ina uwezo wa kuhifadhi lita million 203 inampangplo wa kupanua shughuli zake kwa kujenga sehemu ya kupakia na kupakua mafuta katika kina cha bahari cha mita 20 ili kuwa na uwezo wa kupokea meli kubwa zenye uzito wa tani 100,000.

Amesema kampuni ina mpango kwa kujenga mtambo wa kuzalisha vilainishi, mtambo wa gesi na wa kupokelea lami kutoka melini huku akisisitiza haja ya kuwepo na akiba kubwa ya mafuta.

Wakati huo huo, Meneja wa Bandari, Tanga, Masoud Mrisha amesema tangu kufungwa kwa flow mita katika badandari hiyo mwaka 2020 Serikali imefanikiwa kudhibiti upotevu wa mafuta uliokuwa ukitokea awali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...