Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye (Mb) ametembelea na kuona sehemu zilizoathiriwa na maporomoko ya matope Wilayani Hanang, kukagua Miundombinu ya Anuani za Makazi na Posta pamoja na Kuongeo na Waandishi wa habari.


Akiwa katika ziara hiyo Waziri Nape amevishukuru na kuvipongeza vyombo vya habari kwa kazi kubwa ya kuhabarisha umma kipindi chote ambacho wilaya ya hanang ilikumbwa na Janga kubwa la maafa.


Katika hatua nyingine Mhe. Nape amesema serikali imeandaa minara zaidi ya 30 ambayo itasaidia kupunguza changamoto ya mawasiliano katika kata ya Gendabi na maeneo mengine ya Mkoa wa Manyara.


Aidha, Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Queen Sendiga amemshukuru Mhe. Nape kwa kusudio lake la kuhakikisha mawasiliano ya Simu kwenye maeneo ya vijijini katika Mkoa wa Manyara yanaimarishwa.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...