Na. Mwandishi Wetu.

Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa Mbeya Mbeya kikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu Patrick Mwalunenge, kimeamua kuingilia kati mgogoro wa muda mrefu wa wafanyabiashara na wamiliki wa soko kuu la Kyela.

Wakizungumza katika Mkutano Maalum wa kutatua Mgogoro huo ambao uliitwishwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mbeya, Ndg.Patrick Mwalunenge, baadhi ya wafanyabiashara wamesema wamiliki wa soko hilo, ambao ni CCM wilaya ya Kyela wamewaondoa ndani ya soko hilo kwa madai ya kupisha ujenzi mpya.

Baada ya mnyukano wa muda mrefu wa kutafuta shuluhu, chama hicho kimekuja maadhimio kadhaa ikiwa ni pamoja na kuwaruhusu wafanyabiashara ambao waliondolewa walejee sehemu zao za kufanyia bishara kwa kipindi miezi miwili wakati mchakato wa kupata ufumbuzi wa kudumu ukiendelea.

Pia CCM mkoa Mbeya imeshauri kuundwa kwa kamati maalumu ambayo itashirikisha pande zote, yaani wafanyabiashara, wamiliki, wapangaji na mkandarasi alipewa kazi ya ujenzi wa soko hilo ili kuja na majibu namna gani ujenzi mpya wa soko hilo utakuwa shirikiahi kwa pande zote.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ndugu Mwalunenge amesema chama hicho pia kitahakikisha kinafanya ukarabati wa vibanda ambavyo vilibomolewa kwa ajili ya kuanza ujenzi, huku akiahidi kutoa shilingi laki nane Tsh.800,000/= kwaajili ya kuwashika mkono mamantilie wa soko hilo.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...