NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

MGENI rasmi katika hafla ya utoaji tuzo ya Taifa ya Mwalimu ya uandishi bunifu, Prof.Abdulrazak Gurnah amewasili nchini leo April 12,2024 akipokelewa na mwenyeji wake Waziri wa Elimu Prof..Adolf Mkenda akiwa ameambatana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) Dkt.Aneth Komba.

Akizungumza na waandishi wa habari leo April 12 2024,Jijini Dar es Salaam Waziri wa Elimu Dkt.Adolf Mkenda ameonesha furaha yake wakati akimpokea mgeni huyo ambaye atashiriki zoezi la utoaji tuzo.

Prof.Mkenda amempongeza Prof.Gurnah kwa ukubali wake wa kuja kuwa mgeni rasmi katika zoezi la utoaji tuzo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ya uandishi bunifu itakayofanyika katika ukumbi wa The Super Dome Masaki Jijini Dar es Salaam.

Kwa Upande wake Prof.Abdulrazak Gurnah ameishukuru serikali kumpatia heshima kubwa ya kuja kuwasaidia waandishi wanaopatikana nchini ikiwa kuwapatia uzoefu wake alionao kwa lengo la kuinua tasnia ya uandishi bunifu.

Aidha Prof.Gurnah amesema kuwa hafikirii matumizi ya akili bandia (artificial intelligence) yataathiri kukua kwa waandishi bunifu kwa sababu andiko la mwandishi linatoa sauti (wazo) moja kwa moja tofauti na matumizi ya akili bandia ambayo hayatoi kitu halisi.

Pamoja na hayo Prof.Gurnah ameeleza kuwa ili kuongezeka kwa waandishi wengi wa fasihi na uandishi bunifu watu wengi wanapaswa kusoma ndipo watahamasika kuandika waliyonayo.

Prof.Gurnah ambaye ni mwandishi mkongwe na Mkufunzi katika Chuo cha Kent kinachopatikana nchini Ungereza alitunukiwa tuzo ya Nobel 2021 kwa uandishi wake bora wa fasihi kwa kuchunguza athari za ukoloni katika utambulisho wa Afrika Mashariki, na uzoefu wa wakimbizi wanapolazimika kutafuta makazi kwingine.

Tuzo hiyo ya Taifa ya Mwalimu Nyerere ambayo imeletwa mahususi kwaajili ya kumuenzi Baba wa Taifa na Rais wa kwanza wa Tanzania inatarijiwa kutolewa kesho April 13,2024 katika vipengele vya Riwaya,Ushahiri na hadithi za watoto.












Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...