Na: Mwandishi Wetu – Juba, Sudan Kusini

Bidhaa za Tanzania katika maonesho ya 24 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki maarufu Nguvu Kazi au Jua Kali zimekuwa kivutio kwa watu mbalimbali waliotembelea Banda la Tanzania kwenye Viwanja vya Freedom Hall, Juba Sudan ya Kusini.

Aidha, Bidhaa hizo ni pamoja na vikapu, pochi za wanawake, nafaka, tiba za asili, mvinyo (wine), viungo vya chakula, batiki, bidhaa za Ngozi, asali, urembo, samani (viti, meza).

Wakizungumza Wajasiriamali kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania wamesema maonesho hayo ya 24 ya Nguvu Kazi au Jua Kali yamewapatia fursa ya kutangaza bidhaa zao sambamba na kukuza masoko ya bidhaa zao na huduma wanazotoa.

Kwa upande mwengine, Wananchi wa Sudan ya Kusini wameonyesha kuvutiwa na bidhaa za wajasiriamali wa Tanzania na kueleza kuwa bidhaa hizo zina ubora na ujuzi wa hali ya juu.

Maonesho ya 24 ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki maarufu Nguvu Kazi au Jua Kali yanaongozwa na kauli mbiu “Kukuza Ubunifu wa Kipekee na Maendeleo ya Ujuzi miongoni mwa Wajasiriamali Wadogo na wa Kati wa Afrika Mashariki”.









Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...