Na Ashrack Miraji Lushoto Tanga

MKUU wa Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga Zephania Sumaye amesema zoezi la undikishaji wananchi kwenye daftari la mkazi linaendelea vizuri, wananchi wamehamasika vituo vingi wameshajiandikisha na bado wanaendelea kujiandikisha.

DC Sumaye amezungumza hayo Oktoba 11 mwaka huu 2024 mara baada ya kujiandikisha katika daftari la mkazi kwenye Kituo Cha Chake Chake ambacho ni miongoni mwa kituo cha uandikishaji wananchi kwenye daftari la makazi

Aidha amesisitiza wananchi wakazi wa Lushoto kuendelea kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vilivyopo kwenye maeneo yao kujiandikisha ili wawe na uhalali wa kupiga kura Novemba 27 mwaka huu 2024.

“Tayari kama Mkuu wa Wilaya nimejiandikisha, lakini pia nimepata nafasi ya kukagua baadhi ya vituo kuona hili zoezi linaendaje, nimefarijika sana zoezi linaendelea vizuri Wananchi wamehamasika vituo vingi wameshajiandikisha na bado wanaendelea kujiandikisha”. Alisema DC Sumaye

Zoezi la Uandikishaji wananchi kwenye daftari la mkazi limeanza rasmi leo Oktoba 11 na linaendelea hadi kufikia Oktoba 20 mwaka huu 2024.

Kauli mbiu “Serikali za Mitaa, Sauti ya Wananchi, Jitokeze kushiriki Uchaguzi”



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...