Na Linda Akyoo,Dodoma.

Ikiwa ni Muendelezo wa Wiki ya Huduma kwa wateja ,Mamlaka Ya maji safi na Usafi wa mazingira dodoma (DUWASA) Wamefika katika Mtaa wa Mlimwa C Uliopo Jijini Dodoma Leo tarehe 08 Oktoba,2024 Kuwasikiliza wananchi na wateja wa mtaa huo,Ambapo wametoa malalamiko mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutopata maji kwa wakati na kuingiziwa bili ilihali hawapati huduma ya maji

Akijibu malalamiko ya wateja hao Mkurungezi wa huduma kwa wateja Duwasa Bi Lena Mwakisale Amesema Suala la kusomewa Bili ya maji kwa wateja ni la Kila mwezi na Haki ya mteja kushirikishwa wakati wa usomaji wa Mita ya maji

Aidha Bi.Mwakisale Ameongeza kwa kuwaomba wananchi pindi wanapopata ujumbe wa Bili wakasome kwenye Mita zao ili kujua kama Bili iliyotumwa inauhalisia

Sambamba na hilo asema Kuwa Duwasa inatambua changamoto hiyo ya upungufu wa maji na wapo katika hatua nzuri ya kuhakikisha wananchi wa mtaa wa Mlimwa C wanaunganishwa kwenye bomba kubwa lililopo maeneo ya wajenzi.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...