BODI ya Wakurugenzi ya Shirika la Viwango Tanzania (TBS) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Othman Chande Othman imefanya ziara ya kutembelea ofisi za TBS zilizopo katika mipaka ya Tunduma na Kasumulu ili kujionea shughuli zinazofanyika.

Dhumuni la Ziara hiyo ni kuona changamoto zilizopo na kuzitafutia mkakati na kuielekeza Menejimenti ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao na kuwezesha biashara.

Aidha Bodi hiyo imefanya ziara hiyo Desemba 10 katika mpaka wa Tunduma mkoani Songwe na Desemba 11 kwenye mpaka wa Kasumulu mkoani Mbeya.

Pamoja na hayo Bodi imeielekeza menejimenti ya TBS kuja na mikakati ya bidhaa zinazoingia kupitia njia za panya na kukwepa ukaguzi ikiwa ni pamoja na  kuendelea kutoa elimu ya madhara ya kutumia bidhaa ambazo hazijathibitishwa ubora wake na TBS.













Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...