Na. Faraja Mbise, DODOMA

MIAKA 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara yavuka mikoa katika Jiji la Dodoma baada ya Muendesha Baiskeli kutoka Mkoa wa Kigoma, Wenseslaus Lugaya kuendesha baiskeli hadi Mkoa wa Dodoma ikiwa ni ushiriki wake katika Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara leo tarehe 9 Desemba, 2024.

Akiwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Lugaya alimkabidhi Bendera ya Taifa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule tukio lililoshuhudiwa na mamia ya wakazi wa Jiji la Dodoma wakiongozwa na mkuu wa mkoa.

Viongozi wengine walioshuhudia tukio hilo ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaj Jabir Shekimweri, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Fungo na maafisa waandamizi wa serikali na sekta binafsi.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...