Kampuni ya QYT inayojihusisha na huduma za tiba mbadala pamoja na kutoa fursa Kwa vijana, imeendelea kupanua miradi yake Kwa kufunga tawi jipya katika kata ya mwananyamala wilaya ya kinondoni Jijini Dar es salaam.

Ufunguzi wa kituo hicho umeambatana na semina za Afya Kwa wakazi wa eneo Hilo namna ya kujikinga na maradhi yasiyo ambukiza kama kisukari na pressure ambayo yamekua yakiongezeka Kwa Kasi kubwa nchini.

Mkurugenzi wa QYT Tanzania Bw. Laurence Steven amesema kampuni hiyo imelenga kutoa huduma Bora zaidi za kiafya na elimu Kwa umma kuhusu kutambua wajibu wa kujikinga na maradhi yasiyo ambukiza yanayoongezeka Kwa Kasi kubwa nchini hasa Kwa watu wazima.

Kwa upande wake Judith Mwaheleja Kwaniaba ya kituo hicho amewakaribisha wananchi wa wilaya ya kinondoni na maeneo mengine kupata huduma Mahali hapo ikiwemo vipimo vya mwili mzima (Body Checkup) Kwa gharama ya elfu ishirini pekee.

Huduma zingine ni pamoja na matibabu ya maradhi yasiyo ambukiza Kwa kutumia virutubisho vya asili na huduma zingine za kutoa sumu mwilini. Amesema Bi. Judith







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...