Wajasiriamali nchini wanakabiliwa na changamoto kadhaa zinazowazuia kufanikisha malengo yao, zikiwemo ukosefu wa mitaji, ujuzi wa biashara, nidhamu ya biashara, kukosekana kwa taarifa sahihi kuhusu soko, na changamoto za ubora wa bidhaa.

Hayo yamebainishwa jana jijini Dar es Salaam na Ofisa Mtendaji Mkuu wa AVODA Group, Jun Shiomitsu, wakati akieleza mkakati wa kampuni yake kuwainua na kuwawezesha wajasiriamali kupitia ubia wao na Unleashed Africa Social Enterprises.

Shiomitsu amesema kuwa licha ya wajasiriamali wengi nchini kuwa na biashara zenye mwelekeo mzuri, wanashindwa kuzikuza kutokana na ukosefu wa mbinu za ukuzaji wa biashara na uelewa mdogo wa masoko.

“Biashara zina changamoto nyingi sana, ili kuzikuza lazima wajasiriamali wajifunze mbinu bora za kuhudumia wateja, kutangaza bidhaa kwa ubunifu, na kushirikiana na wafanyabiashara wengine,” amesema Shiomitsu.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...