Na Bakari Madjeshi, Michuzi TV

Rais wa Heshima na Mwekezaji wa Simba SC, Mohammed Dewji (Mo Dewji) amethibitisha kuwa kutoka mwaka 2017 hadi mwaka 2024 ametumia zaidi ya Shilingi Bilioni 80 (Tsh. 87 B) kwenye masuala mbalimbali kwa ajili ya Klabu hiyo.

Mohammed amesema hayo kupitia ‘video’ yake aliyoichapisha kwenye mtandao wa ‘Instagram’. Amesema kiasi hicho cha pesa ametumia Shilingi Bilioni 45 kwenye kulipa mishahara,usajili, maandalizi na mengine ya uendeshaji wa timu.

Mo Dewji amesema kiasi cha Shilingi Bilioni 20 amekitoa kama sehemu ya ununuzi wa hisa (49%) ndani ya Simba SC. Pia, amesema mara nyingi ametoa msaada nje ya mfumo rasmi kila palipohitajika uhitaji wa dharura ambapo ametoa Shilingi Bilioni 22 kuanzia mwaka 2017 hadi 2024.

Kupitia taarifa hiyo, Mo Dewji amesema kuwa dhamira yake ni kuiona Simba SC inatwaa ubingwa wa Afrika, hivyo amewaomba wanachama na mashabiki kuwa kitu kimoja ili kutimiza malengo.
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...