Na Said Mwishehe,Michuzi TV

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais,Mipango na Uwekezaji Profesa Kitila Mkumbo ametoa rai kwa vyama vya siasa nchini kuzingatia Dira 2050 wanapotoa Ilani zao.

Akizungumza leo Julai 8,2025 jijini Dar es Salaam mbele ya wahariri na waandishi wa habari ,Profesa Mkumbo amesema kuwa mchakato wa Dira 2050 imehusisha watanzania wa makundi mbalimbali na miongoni kupitia vyama vya siasa.

“Vyama vya siasa 19 vimeshiriki kikamalifu,vyama vikubwa na vidogo vyote vimepata nafasi.Tulimuomba Msajili wa vyama vya siasa atuaandalie mkutano na vyama vya siasa wametoa maoni yao.

“Tumekubaliana kwenda safari moja ya Dira 2050 ya Tanzania Tuitakayo . Hivyo wanasiasa hatutabishana kuhusu dira ya maendeleo ila watapishana wanatumia usafiri gani kuifikia hiyo dira.

“Vyama vya siasa wamekubaliana kuweka Ilani inayoakisi  Dira 2050 na hata ccm Ilani yetu tumezingatia dira hiyo Hivyo  tunatarajia na vyama vingine vya siasa Ilani zao zitaangalia dira 2050.”





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...