Na Said Mwishehe,Michuzi TV-Geita
MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk.Samia Suluhu Hassan, ameahidi katika miaka mitano ijayo Serikali itajenga kiwanja kikubwa cha michezo Geita mjini mkoani Geita.
Akizungumza leo Oktoba 13,2025 mbele ya maelfu ya wananchi wa Jimbo la Geitq Mjini katika Uwanja wa EPZA Bombambili mkoani Geita Mgombea Urais Dk.Samia amesema katika katika kukuza utamaduni, sanaa na michezo Serikali imeanza ujenzi wa viwanja vikubwa vya michezo.
Amefafanua kwamba mchezo wa mpira wa miguu Serikali inaendelea kujenga uwanja Bukombe na kwa Geita Mjini pia utajengwa Uwanja mkubwa wa kisasa.
Pamoja na mambo mengine Mgombea Urais Dk.Samia amesisitiza kwamba Serikali yake itaendelea kuwekeza kwenye michezo kwani sekta hiyo inatoa ajira nyingi kwa vijana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...