Mshindi wa Mashindano ya @missuniversetanzania mwaka 2025 mwanadada @naisae.yona, amekabidhiwa rasmi gari jipya aina ya Hyundai kutoka kwa @hyundai_tanzania lenye thamani ya shilingi milioni 49.

Hafla ya makabidhiano hayo imefanyika leo Oktoba 22, 2025 ambapo @naisae.yona ametajwa kuwa si mrembo tu, bali ni kielelezo cha kizazi kipya cha wanawake wa Kitanzania wenye nidhamu, maono, ujasiri na moyo wa kujitolea kwa jamii.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Millen Prive Co. & Lifestyle na Muandaaji wa Miss Universe Tanzania, Millen Magese amesema;

“@naisae.yona si mrembo tu, ni kioo cha kizazi kipya cha wanawake wa Kitanzania wenye maono, nidhamu na ujasiri, wenye mioyo mikubwa ya kutoa na kusaidia jamii, kupitia ushindi wake tunaiona sura mpya ya Tanzania inayokwenda kuwa kioo cha urembo duniani.”

Kwa upande wake, @naisae.yona amesema leo ni siku yenye maana kubwa kwake, akieleza kuwa amefanikiwa kutimiza ndoto yake kubwa maishani na kwamba ataendelea kuwa mfano na sauti ya kuhamasisha wanawake na wasichana kuamini katika ndoto zao.

Miss Universe Tanzania, Naisae Yona ataondoka nchini Jumatatu ya October 27,2025 kuelekea nchini Thailand yatakapofanyika mashindano ya Miss Universe.

Aidha @hyundai_tanzania wameahidi kutoa magari ya msafara utakaomsindikiza Naisae Airport wakati akiondoka nchini.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...