Wiki ya Maadhimisho ya Chakula Duniani Kitaifa imefunguliwa rasmi leo tarehe 11 Oktoba 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Balozi Batilda Buriani, katika viwanja vya Usagara jijini Tanga.
Maadhimisho haya yataendelea hadi tarehe 16 Oktoba 2025, yakihudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya chakula kutoka ndani na nje ya nchi.
Kauli mbiu ya mwaka huu “Tuungane Pamoja Kupata Chakula Bora kwa Maisha ya Baadaye” inaweka msisitizo wa kitaifa juu ya mshikamano, ubunifu, na uwajibikaji wa pamoja katika kujenga mifumo endelevu ya usalama wa chakula kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), kama mdau muhimu wa sekta ya chakula, inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuhakikisha taifa linajitosheleza kwa chakula.
Kauli mbiu ya mwaka huu “Tuungane Pamoja Kupata Chakula Bora kwa Maisha ya Baadaye” inaweka msisitizo wa kitaifa juu ya mshikamano, ubunifu, na uwajibikaji wa pamoja katika kujenga mifumo endelevu ya usalama wa chakula kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), kama mdau muhimu wa sekta ya chakula, inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuhakikisha taifa linajitosheleza kwa chakula.
Kupitia mikopo nafuu kwa wakulima, waongezaji thamani, na watoa huduma katika mnyororo wa thamani ya kilimo, TADB inachochea mapinduzi ya kilimo cha kisasa kilimo chenye tija, chenye thamani ya kibiashara, na chenye kuleta ustawi wa jamii.
Katika maadhimisho haya, TADB imesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika kilimo kinachojenga uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
Katika maadhimisho haya, TADB imesisitiza umuhimu wa kuwekeza katika kilimo kinachojenga uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...