Bodi ya wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Novemba 21, 2025 imefanya ziara Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza namna Mamlaka hiyo inavyofanya kazi kama wadau muhimu katika masuala ya uchunguzi wa kisayansi kwa wanyamapori.
Wajumbe wa Bodi hiyo walipokelewa na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, na kupewa maelezo kuhusu majukumu yanayofanywa na Mamlaka hiyo yenye jumla ya maabara 7 za vipimo, uchambuzi na utafiti.
Ziara hiyo iliambatana na kutembelea Maabara ya Vinasaba vya Wanyamapori “Wildlife DNA Laboratory” ambapo maabara hiyo ina jukumu la uchunguzi wa vinasaba “DNA” vya wanyamapori, kutoa ushahidi wa kisayansi kwa kesi za ujangili, kutoa mafunzo juu ya ukusanyaji na uhifadhi wa sampuli, kuhifadhi na kusaidia ushirikiano kati ya taasisi hiyo na wadau mbalimbali katika kukabiliana na ujangili.
Wajumbe wa Bodi hiyo walipokelewa na Mkemia Mkuu wa Serikali, Dkt. Fidelice Mafumiko, na kupewa maelezo kuhusu majukumu yanayofanywa na Mamlaka hiyo yenye jumla ya maabara 7 za vipimo, uchambuzi na utafiti.
Ziara hiyo iliambatana na kutembelea Maabara ya Vinasaba vya Wanyamapori “Wildlife DNA Laboratory” ambapo maabara hiyo ina jukumu la uchunguzi wa vinasaba “DNA” vya wanyamapori, kutoa ushahidi wa kisayansi kwa kesi za ujangili, kutoa mafunzo juu ya ukusanyaji na uhifadhi wa sampuli, kuhifadhi na kusaidia ushirikiano kati ya taasisi hiyo na wadau mbalimbali katika kukabiliana na ujangili.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...