Na Mwandishi Wetu, Handeni TC
Madiwani wa Halmashauri ya Mji Handeni wameaswa kuzingatia miiko ya viongozi wa umma na kudumisha uadilifu katika utekelezaji wa majukumu yao.
Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa Baraza la Madiwani Desemba 4, 2025, kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Bakari Mussa kutoka Ofisi ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma amewataka madiwani hao kuzingatia maadili, kuepuka mgongano wa maslahi, na kushirikiana kikamilifu na Mkurugenzi wa Halmashauri katika kusimamia shughuli za maendeleo.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Maryam Ukwaju, amewahimiza madiwani kufanya kazi kwa kuzingatia maslahi mapana ya nchi na ya Halmashauri.
Amesisitiza umuhimu wa uwajibikaji na kujiepusha na vitendo vinavyohatarisha uadilifu wa utumishi wa umma.



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...