KAMISHNA wa Kamisheni ya Polisi Jamii, CP Faustine Shilogile, amewasili mkoani Mwanza leo, Januari 07, 2026, kwa ziara ya kikazi ambapo anatarajiwa kufungua mafunzo ya siku moja kwa Maafisa wa Polisi Jamii kutoka mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Mafunzo hayo yatahusisha washiriki ambao ni maafisa wa Polisi Jamii kutoka Mikoa ya Mara, Tarime, Rorya, Simiyu, Geita, Tabora na Shinyanga.

Lengo kuu la mafunzo haya ni kuimarisha mikakati ya kuzuia uhalifu kabla haujatokea na endapo utatokea, usirudiwe tena, kwa mujibu wa mipango iliyowekwa na wadau husika.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kuongeza ufanisi wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha usalama na kuendeleza ushirikiano na jamii katika kudhibiti uhalifu.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...