Manyoni, Singida, Januari 18, 2026
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Kenani Labani Kihongosi, ameanza rasmi ziara yake ya kimkakati leo tarehe 18 Januari 2026 mkoani Singida, ambapo ameanzia Wilaya ya Manyoni.
Ziara hii ni ziara maalum ya Chama Cha Mapinduzi inayolenga kuhakikisha Chama kinawafikia wanachama wote nchini sambamba na kusikiliza kero za wananchi, kuzifanyia kazi na kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi kwa wakati.
Akizungumza na wanachama walio jitokeza, Ndugu Kihongosi aliwasilisha salamu za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Alisisitiza umuhimu wa umoja, mshikamano na upendo.



.jpeg)


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...