Na Mwandishi Wetu,Michuzi TV

WATALAAM zaidi 1500 wawekimo Wanasayansi, watunga sera kutoka sehemu mbalimbali duniani wanatarajiwa kushiriki Kongamano la Kimataifa la Kilimo na Lishe linalotarajia nchini Tanzania.
Akizungumza leo Juni 22,2025 jijini Dar es SalaamNaibu Makamu Mkuu wa SUA anayesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaalamu, Prof. Maulid Mwatawala, alisema kongamano hilo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Shule ya Lishe na Tiba za Magonjwa ya Kitropiki ya London (LSHTM).

Amesema katika kongamano hilo washiriki watajadili namna ya kuimarisha sekta ya kilimo na lishe duniani na kwamba limekuja wakati muafaka, kwani Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejipanga kuboresha sekta ya kilimo na kuhakikisha wananchi wanakuwa na lishe bora.
Awali  Mwenyekiti Mwenza wa Kongamano hilo kutoka SUA, Prof. Joyce Kinabo, ameeleza kongamano hilo linafanyika wakati dunia ikikabiliwa na changamoto kubwa ikiwemo ya mabadiliko ya tabianchi, upungufu wa chakula, na utapiamlo. 

“Jambo la kushangaza ni kwamba licha ya Tanzania kuwa na mikoa inayozalisha chakula kwa wingi, bado kuna maeneo yanayokumbwa na utapiamlo au uzito kupita kiasi.”

Kwa upande wake Profesa Suneetha Kadiyala, mtaalamu wa kimataifa wa lishe kutoka LSHTM amesema kongamano hilo linatarajiwa kutoa mapendekezo ya kisera na kitaalamu yatakayosaidia mataifa wanachama kupambana na changamoto zinazoikumba sekta ya chakula na lishe, hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko ya tabianchi na ongezeko la idadi ya watu.

Pia amesema  kongamano hilo linaunganisha nia ya kisiasa, uongozi wa kikanda na jamii ya kimataifa katika kuboresha mifumo ya chakula duniani.”Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2016, jukwaa hili limekuwa likiwakutanisha wadau mbalimbali na limechangia kwa kiasi kikubwa kusaidia watunga sera kuboresha hali ya lishe.”


Sehemu ya waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo ulifanyika leo Juni 22,2025 jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MASSSAKA, MICHUZI TV)

 

MENEJA wa Mfuko wa Self MF Kanda ya Kati Dodoma na Singida Aristid Tesha amesema kuwa kwa sasa mfuko huo umeanzisha bidhaa mpya ambapo wanatoa mikopo kwa wajasiriamali wanaojihusisha na Nishati mbadala,Nishati safi wanajikita katika kuuza bidhaa za gesi na vifaa vyake.

Aliongeza kuwa wanaangalia kwa waliojikita kwenye mambo ya vifaa vya umeme wanazitumia kama Nishati mbadala.

Alisema hiyo yote ni nia ya serikali ya kumfanya Mtanzania apunguze matumizi ya mkaa,kuni katika eneo linalomzunguka.

"Hawa wanaofanya Nishati mbadala tumewalenga na tunawapa mkopo wenye riba nafuu ili waweze kupanua wigo kufanya shughuli zao na kuweza kuwafikia wananchi," alieleza.

Alifafanua kuwa kwenye Nishati mbadala wamejikita kwa wanaosambaza sola za umeme waliopo vijijini na mijini wanaowauzia wananchi kwa bei nafuu.

Aidha akizungumzia mikopo ya watumishi wa Umma alisema kuwa wanatoa mikopo kwa watumishi kupitia mishahara yao ambapo huduma ya mikopo hiyo inapatikana katika matawi yaliyopo mikoa 12.

Hata aliwahimiza wananchi kutembelea banda la Self MF ili waweze kupata maelezo ya huduma mbalimbali zinazotolewa na mfuko huo.

Naye Meneja Rasilimaliwatu na Utawala Johari Magara alieleza kuwa lengo kuu la kushiriki maadhimisho hayo ni kuwapa huduma wananchi ya kuwapa taarifa ya huduma za mikopo zinatolewa na mfuko huo.

Alieleza kuwa mfuko wa self MF ulianza rasmi 2014 ambapo lengo kuu ni kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapatia mikopo yenye unafaa.

"Mikopo ya Self MF ya aina mbalimbali ikiwemo mikopo ya watumishi wa Umma, wafanyabisahara, wajasiriamali wadogo na wa kati, mikopo ya wakulima, mkopo wa wazabuni pamoja na Nishati safi,"alisema.

Alieleza kuwa mbali na mikopo hiyo pia mfuko huo unatoa mkopo wa bima za gari,nyumba, za wizi na nyingine zote.


 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya waratibu, waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma. 
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya waratibu, waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma. 

Meza kuu ikiwa katika mkutano huo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Ramadhani Kailima akizungumza jambo wakati wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma.

Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma. 


Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma.
Hakimu Denis John Mpelembwa akiwaapisha washiriki 

Washiriki wa mafunzo ya siku tatu ya Waratibu, Waandishi Wasaidizi na Waendesha vifaa vya Bayometriki wa Magereza kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 mkoani Dodoma wakila kiapo cha kutunza siri kabla ya kuanza mafunzo hayo.
Mratibu wa Uandikishaji ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mafunzo , akizungumza jambo.
Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji, Caroline Ruben akiwasilisha mada kuhusu uraia kwa washiriki wa mafunzo hayo. 
******
Na. Waandishi Wetu
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewaasa watendaji wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwenye Magereza kwa Tanzania Bara na Vyuo vya Mafunzo kwa Tanzania Zanzibar kufanya kazi kwa weledi.
 
Wito huo umetolewa wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu kwa watendaji hao ambayo yameanza leo tarehe 22 Juni, 2025 Mkoani Dodoma kwa Magereza sambamba na Unguja kwa Vyuo vya Mafunzo. 

Akifungua mafunzo kwa watendaji hao yaliyofanyika Mkoani Dodoma kwa watendaji wa Magereza, Tanzania Bara, Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mhe. Jacobs Mwambegele amesema Tume imewateua watendaji hao kutokana na weledi wao.
 
“Sina shaka kuwa kuteuliwa kwenu kunatokana na ujuzi, uwezo na weledi mlionao katika kutekeleza majukumu ya kitaifa likiwepo zoezi la uboreshaji wa Daftari ambalo ni sehemu ya maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025,” amesema Mhe. Mwambegele.
 
Amewahakikishia watendaji hao kuwa kwenye mafunzo hayo ya siku tatu Tume itawapa ujuzi wa kutosha kwa nadharia na vitendo kuwawezesha kutekeleza jukumu lao kwa weledi.
 
Akifungua mafunzo kama hayo Kisiwani Unguja, Zanzibar kwa watendaji wa Vyuo vya Mafunzo, Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji wa Rufani Mstaafu, Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk ametoa wito kwa watendaji hao kuvitunza vifaa vya uboreshaji wa daftari.
 
“Ninatoa wito kwenu kuhakikisha mnavitunza vifaa vyote vitakavyotumika katika zoezi la uboreshaji wa Daftari na kuzingatia maelekezo yote yatakayotolewa na Tume ili muweze kuyafanyia kazi kwa usahihi wakati wote wa utekelezaji wa zoezi hilo,” amesema.
 
Jaji Mbarouk pia amewahakikishia watedaji hao kuwa maafisa kutoka Tume watakuwepo muda wote wa zoezi na kwamba endapo watapata changamoto ya aina yoyote wasisite kuwasiliana nao.
 
Kwa mujibu wa ratiba zoezi hilo la uboreshaji wa Dafatri kwenye Magereza na Vyuo vya Mafunzo linafanyika kwa siku saba kuanzia tarehe 28 Juni hadi tarehe 04 Julai, 2025 ambapo watakaohusika ni mahabusu na wafungwa walihukumiwa kifungo chini ya miezi sita.
Makamu Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe, Jaji wa Rufani (Mstaafu), Mbarouk Salim Mbarouk 
akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu ya waratibu, waandishi wasaidizi na waendesha vifaa vya bayometriki wa Vyuo vya Mafunzo kuhusu uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura yaliyoanza leo Juni 22 -24, 2025 Mjini Unguja Zanibar. 
Mkurugenzi wa Ofisi ya Zanzibar, Ndg. Adam Mkina akizungumza wakati wa Mafunzo hayo.
Meza Kuu ikiwa katika mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea 

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Edward Mpogolo (wa tatu kushoto) akiwa na Meneja Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Julius Mnganga (wa pili kulia) wakiwa na mfano wa cheki ya shilingi milioni 735 ziliztolewa kwa vikundi 25 vya wajasiriamali waliokidhi vigezo vya kupata mikopo shirikishi itokanayo na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri inayotolewa na CRDB Bank Foundation na Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Wengine katika picha ni Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Mheshimiwa Omary Kumbilamoto (katikati), Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya (wa tatu kushoto). Wengine ni Meneja wa Tawi la Benki ya CRDB Gongolamboto, Wemaeli Msechu (wa kwanza kushoto), Meneja wa Tawi la Benki ya CRDB Ilala, Mariamu Mrema (wa pili kushoto) na Mchambuzi wa Ruzuku wa CRDB Bank Foundation, Frank Kahatano (wa kwanza kulia).

=====   =====  =====

Dar es Salaam: Baada ya kukamilisha maandalizi yote muhimu ya kuwawezesha wajasiriamali wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Taasisi ya CRDB Bank Foundation kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imezingua utoaji wa mikopo itokanayo na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri.

Uzinduzi huo ulioongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mheshimiwa Edward Mpogolo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mheshimiwa Albert Chalamila, ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita umekuja baada ya kukamilika kwa mchakato wa kuwashirikisha wananchi kwa kuwapa mafunzo ya ujasiriamali na elimu ya fedha.
“Miaka minne iliyopita, Ilala ilikuwa inakusanya shilingi bilioni 61 kwa mwaka lakini sasa mapato yamepanda mpaka shilingi bilioni 138 hivyo fedha zinazotengwa kwa ajili ya wajasiriamali ni nyingi na zitaendelea kuongezeka kila mwaka. 
Tunashirikiana na CRDB Bank Foundation kuwafikia wananchi wengi kadri iwezekanavyo. Niwaombe wajasiriamali walio tayari, jitokezeni ili kunufaika na mikopo hii,” amesema Mheshimiwa Mpogolo.

Akieleza utayari uliopo, Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Dar es Salaam, Elihuruma Mabelya amesema jumla ya shilingi bilioni 18 zipo tayari kukopeshwa hivyo akawataka wananchikujitokeza akibainisha kuwa kuna vikundi 945 vilivyojitokeza mpaka sasa.

“Asilimia 4 ya fedha hizi ni kwa ajili ya wanawake na asilimia 4 nyingine zimeelekezwa kwa vijana na asilimia mbili zilizobaki ni za watu wenye ulemavu. Wanawake mmepewa nafasi kubwa zaidi kwani ndani yenu kuna vijana na watu wenye ulemavu pia hivyo ukichambua kwa umakini unaweza kukuta ninyi mnapata mpaka asilimia 80 ya kiasi chote kilichopo hivyo niwasihi muichaangamkie fursa hii iliyo mbele yenu,” amesema Mabelya.

Hata hivyo, walengwa wa mikopo hiyo walikumbushwa umuhimu wa kutimiza wajibu wao kwa kueepuka udanganyifu wanapotoa taarifa zao, waunde vikundi kwa nia halisi ya ujasiriamali, kusajili biashara zao na waombe mkopo kwa biashara wanazozimiliki.

Akimwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, Meneja Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Julius Mnganga amesema mpaka sasa wameshavifikia vikundi 120 ambavyo vimewasilisha maombi ya mikopo yenye thamani ya jumla kiasi cha shilingi bilioni 3.

Hata hivyo, Mnganga amesema baada ya kuvitembelea vikundi hivyo pamoja na wanachama wake wamekuta vikundi 25 ndivyo vinakidhi vigezo vya kunufaika na mikopo hiyo kwa sasa.

“Vikundi hivi 25 vimeleta maombi yenye thamani ya shilingi milioni 735. Tunaendelea kutoa elimu ili kuviwezesha vikundi vyote vilivyoleta maombi ili vikamilishe vigezo vinavyohitajika kunufaika na mikopo hii nafuu. Nitumie fursa hii kuwakaribisha wajasiriamali wengine ndani ya Manispaa ya Ilala kuja kuomba uwezeshaji huu ili wakuze biashara zao,” amesema Mnganga.

Katika vikundi 120 vilivyojitokeza, Mnganga amesema 75 ni vya wanawake, vikundi 43 vya vijana na vikundi viwili ni vya watu wenye ulemavu. Kuhusu vikundi 20 vilivyokidhi vigezo, amesema vikundi 13 vya vijana, vimeomba jumla ya shilingi milioni 532 huku vikundi 11 vya wanawake vikihitaji shilingi milioni 198 na kikundi kimoja cha watu wenye ulemavu shilingi milioni 5.

Taasisi ya CRDB Bank Foundation imeahidi kuendelea kushirikiana na maafisa maendeleo wa Manispaa ya Ilala pamoja na viongozi wa vikundi husika kuwasaidia wanachama wao kurekebisha kasoro zilizopo ili wote wenye nia njema wanufaike na mikopo hii.

“Jambo muhimu kulizingatia muda wote ni kurejesha fedha hizi kwa wakati. Wote mtakaopewa mikopo hii msisahau kuirejesha kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tunatoa nafasi kwa wengine nao kukopa,” amesisitiza Mnganga. 
Na Mwandishi wetu

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt Stergomena Tax (Mb,) amefunga rasmi mafunzo ya mwaka mmoja ya Ukamanda na Unadhimu, katika Mahafali ya 39 ya Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Tanzania yaliyofanyika katika Viwanja vya chuo hicho, Duluti Arusha

Mahafali hayo ambayo Waziri wa Ulinzi na JKT alikuwa mgeni rasmi yalihusisha jumla ya Maafisa wahitimu 71 toka Jeshi la Wananchi la Tanzania na Maafisa wahitimu toka nchi marafiki.

Katika Mahafali hayo wahitimu hao pia wa kozi ya Ukamanda na Unadhimu pia walitunukiwa Shahada za Umahiri na stashahada ya Masuala ya Ulinzi na Usalama, mafunzo ambayo yaliendeshwa sambamba na kozi ya ukamanda na unadhimu.

Katika mahafali hayo, Waziri wa Ulinzi alisema amefurahishwa kupewa nafasi ya kuongoza Sherehe za Mahafali ya 39 ya Ukamanda na Unadhimu chuoni- Duluti na akatoa pongezi kwa Maafisa wote Wanafunzi 71 waliohitimu mafunzo hayo.

Waziri Stergomena Tax akawapongeza kwa bidii, ustahimili wa mafunzo makali na kuonyesha nidhamu, ujasiri, uthabiti na kujitolea unaohitajika ili kupata kumaliza kozi hiyo mashuhuri ya kimataifa. Na akawaambia wahitimu hao wanapaswa kujivunia sana mafanikio hayo.

Kwa Upande wa Maafisa Wahitimu wanawake, Waziri wa Ulinzi amewapongeza na kuwaambia wahitimu hao kuwa, wanawake ni sehemu muhimu ya jumuiya ya kijeshi, Uwepo wao katika kozi ya 39 ya ukamanda na unadhimu ni ushuhuda hai kwamba wanajeshi wetu wameunganishwa zaidi kulingana na jinsia kuliko hapo awali.

Waziri Tax akaongeza kwa kuwaambia wahitimu hao wanawake kwamba, kuhitimu mafunzo hayo ni kielelezo tosha cha kuonyesha kuwa wanawake wanaweza kutimiza majukumu yao katika kada sekta ya Ulinzi na Usalama kwa ufanisi na weredi bila kujali jinsia.

Amesema Tanzania kuongozwa na Rais wa Kwanza mwanamke Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni hatua muhimu kwa wanawake katika uongozi wa juu, na kama Amiri Jeshi Mkuu, Uongozi wake bora unatuma ujumbe mzito kuhusu uwezo wa uongozi wa wanawake, na umuhimu wa kuwapa fursa sawa ili kuchangia amani, usalama na ustawi wa mataifa.

Aidha, Waziri Tax amewaambia wahitimu hao wa kozi ya Ukamanda na Unadhimu, “natambua mmepewa dhamana kubwa ya uongozi, mawazo ya kimkakati, na ustadi wa kufanya maamuzi, na mpo tayari kukabiliana na changamoto ambazo ziko mbele yenu.

Nyinyi ni viongozi wa baadaye wa Majeshi yetu ya Ulinzi, walinzi wa usalama wa Mataifa yetu, na walinzi wa uhuru wetu unaothaminiwa.

Waziri wa Ulinzi na JKT akawaambia wahitimu kuwa kama viongozi wajao watakabidhiwa majukumu ya kufanya maamuzi muhimu ya ulinzi na usalama wa mataifa yao akawaambia ana uhakika kwamba Elimu na ujuzi walioupata umewatayarisha, na utatumika kama msingi wa utekelezaji wa majukumu yao na kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Waziri Tax akawakumbusha Maafisa wahitimu hao kwamba uongozi hauhusu vyeo na nyadhifa, bali ni kuonyesha na kuongoza njia, kuwatia moyo wengine kwa uwezo wao kamili na kufanya kazi pamoja kufikia lengo linalotarajiwa. Kwa hivyo akawataka kudumisha maadili ya heshima, uadilifu, nidhamu katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Ulimwengu tunaoishi, unabadilika mara kwa mara na changamoto tunazokabiliana nazo zinazidi kuwa ngumu na zisizotabirika, akawahimiza wahitimu wa kozi hiyo adhimu kwamba wamepewa zana na uwezo unaohitajika ili kukabiliana na changamoto hizo zinazoendelea kwa ujasiri na uthabiti.

Vile vile Waziri wa Ulinzi akazishukuru nchi marafiki za Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Jamhuri ya Shirikisho la Ethiopia, Jamhuri ya Kenya, Ufalme wa Eswatini, Jamhuri ya Malawi, Jamhuri ya Msumbiji. , Shirikisho la Jamhuri ya Nigeria, Jamhuri ya Rwanda, Jamhuri ya Uganda, Jamhuri ya Zambia na Jamhuri ya Zimbabwe, kwa urafiki na ushirikiano wao katika kutoa maafisa kushiriki katika kozi hii ya Ukamanda na Unadhimu.

Waziri Stergomena Tax akawaambia nchi marafiki kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inathamini uhusiano wa kirafiki uliopo na nchi zao na ana imani uhusiano wa muda mrefu utaimarishwa kwa ushirikiano unaoendelea, ikiwa ni pamoja na ushiriki katika kozi zinazotolewa na Chuo Duluti.

Mahafali ya 39 ya Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Duluti yamehudhuriwa pia na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Luteni Jenerali Salum Haji Othman, Wakuu wa Kamandi za Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Wakuu wa Vyuo ya Ukamaanda na Unadhimu vya Afrika Mashariki, Wakuu wa Vyuo ya Kijeshi ya Jeshi la Wananchi la Tanzania, Waambata Jeshi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, Maafisa wakuu Majenerali toka Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Makamanda vikosi vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.











Balozi wa India nchini Tanzania, Bishwadip Dey amesema Tanzania iko katika hatua za mwisho kutengeneza magari yanayotumia Umeme na Gesi nchini kupitia kiwanda cha kampuni ya GF kilichopo Kibaha mkoani Pwani.

Akizungumza na Waandishi wa Habari wakati wa hafla ya uzinduzi wa gari ya Mahindra Scorpio uliofanyika jijini Dar es salaam, Balozi Dey amesema kutokana na mahusiano mazuri ya kibiashara kati ya serikali ya Tanzania na India,imesababisha wawekezaji wengi kutoka nchini India kuja kuwekeza nchini  Tanzania,hali inayoendeleza mahusiano mazuri yaliofanywa na Waasisi wa Mataifa hayo mawili.

"Miongoni mwa kampuni hizo ni kampuni ya magari ya Mahindra ambayo imetambulisha gari mpya katika soko la Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki,lakini niseme tu kuwa magari haya kuanzia mwakani yatakuwa yakitengenezwa nchini Tanzania katika kiwanda cha GF Kilichopo Kibaha mkoani Pwani",amesema Balozi Bishwadip Dey.

Nae Mtendaji Mkuu wa kampuni ya GF Mehboob Karmali alisema ujio wa Mahindra nchini ni ukombozi, kwani leo wametambulisha Gari sokoni na baadaye watazindua gari za umeme na gesi zitakazotengenezwa nchini Tanzania kupitia kiwanda chao Kilichopo Kibaha mkoni Pwani.

"Kwa kuanza tutaanza na magari madogo 'pickup- double cabin' maalumu kwa shughuli za kilimo na wajasiliamali wadogo hasa mashambani" alisema Karmali.

Pia alizitaka tasisi za umma na serikiali kwa ujumla kujenga tabia ya kununua bidhaa kutoka kwenye  viwanda kwetu ili kuvilinda na kuongeza pato la taifa na kuokoa pesa ambayo ingetumika kuagiza bidha nje ya nchi.
 
Kampuni ya GF Automobile imezindua gari aina ya Mahindra Scorpio kwa ajili ya matumizi katika bara bara za mazingira tofauti hasa vijijini na mashambani na gesi kukabiliana na mazingira tofauti.
Balozi wa India nchini Tanzania, Bishwadip Dey akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya GF Automobile, Mehboob Karmali ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa gari mpya ya Mahindra Scorpio uliofanyika jijini Dar es salaam.Kulia ni  Mtendaji mkuu wa Mahindra,ukanda wa  Africa, Bobby Salwan
Balozi wa India nchini Tanzania, Bishwadip Dey akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa gari ya Mahindra scorpio
Gari aina ya Mahindra Scorpio ikitembea wakati wa uzinduzi huo

KIKAO CHA WAFANYABIASHARA WA USAFIRISHAJI WA MIZIGO MAALUM NA WAMILIKI WA MAKAMPUNI 

Je, wewe ni mfanyabiashara au mmiliki wa kampuni unayetuma mizigo kati ya Falme za Kiarabu (Dubai) na Tanzania?

Je, umekuwa ukihangaika kupata njia bora, ya uhakika, na nafuu ya kutuma mizigo yako kutoka Dubai kwenda Tanzania?

Je, umekuwa ukipitia changamoto za Mizigo yako ya Biashara kuachwa, Mizigo Kuchelewa na changamoto za MCO?

SASA TUMEKUFIKIA NA TUNA HABARI NJEMA JUU YAKO!!!


TAREHE 22/06/2025 SIKU YA JUMAPILI MNAKARIBISHWA KWENYE KIKAO CHA WAFANYABIASHARA CHA UFUNGUZI WA HUDUMA MPYA YA NDEGE YA MIZIGO. KWENYE KIKAO HIKO MTAWEZA KUJUA HUDUMA MBALI MBALI ZINAZOTOLEWA ZIKIWEMO , RATIBA YA NDEGE, AINA YA MIZIGO NA BEI KWA KILO

KARIBUNI SANA KWENYE KIKAO HICHO AMBACHO KITATOA FURSA KWA WAFANYABIASHARA NA VILEVILE KUJENGA UHUSIANO
KITAKACHOFANYIKA:
SIKU YA JUMAPILI
TAREHE 22/06/2025
UKUMBI: LANDMARK HOTEL, BANIYAS DEIRA
MUDA: KUANZIA SAA 8 MCHANA

👉 Usikose fursa hii adhimu kuleta mapinduzi halisi kwenye biashara yako!

🔔 Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa zaidi.

Kwa mawasiliano: +971504295744

 


Top News