haMWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepewa heshima na hadhi ya kuwa Mtemi wa Sungusungu, jeshi la jadi, kwa mikoa mitano ya Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Geita na Tabora.

Mhe. Rais Dkt. Samia ambaye pia ni Mkuu wa Machifu nchini, akijulikana kwa jina la Chifu Hangaya, ametangazwa rasmi kuwa Mtemi wa Sungusungu kupitia risala ya utii wao kwake, wakati wa hafla ya kumpongeza kwa utekelezaji wa miradi ya kimkakati, iliyofanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, mkoani Mwanza, leo Ijumaa, tarehe 20 Juni 2025.

“Mheshimiwa Rais (Dkt. Samia) kwa kuwa wewe ni Amiri Jeshi Mkuu, na sisi ni walinzi wako, watiifu kabisa, tunaomba upokee hadhi ya kuwa Mtemi wa Sungusungu. Nakukabidhi vifaa vya ulinzi wa jadi, ambavyo vitatolewa maelezo. Aidha, tunaomba tukutambulishe watemi na makamanda wa Sungusungu, ambao tumekuwa tukishirikiana katika mikoa hii mitano,” alisema Ndugu Richard Bundala, kiongozi wa Sungusungu hao.

Mtemi wa Sungusungu Kanda ya Ziwa, Sumbe Martine Mogani alimkabidhi Dkt. Samia silaha za kijadi, ambazo ni upinde na mishale, pamoja na mavazi ya kaniki na kofia, ikiwa ni ishara ya kumpatia heshima na hadhi hiyo ya kuwa mtemi wa Sungusungu katika mikoa hiyo mitano.

Kwa upande wake, Mhe. Rais Samia aliwapongeza Sungusungu kwa kutimiza miaka 42 tangu jeshi hilo la ulinzi wa jadi lilipoanzishwa kwa nia ya kuitikia wito wa kisera wa ulinzi na usalama, uliomtaka kila Mtanzania kuwa mlinzi ndani ya nchi yake, huku akiwataka kuendelea kushirikiana na mamlaka za kisheria, hasa Jeshi la Polisi, kupitia polisi jamii, katika kulinda amani na utulivu wa nchi katika maeneo yao.

Rais Dkt. Samia pia aliwapongeza walinzi hao wa jadi kwa mchango mkubwa ndani ya muda huo wote tangu kuanzishwa kwao, huku akiwataka kuendelea kuwa sehemu ya ulinzi na usalama wa mali na miradi ya maendeleo ambayo nchi imeanzishwa na kukamilishwa kwa gharama kubwa kote nchini.








Na Mwandishi Wetu

UTAFITI uliofanywa na Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kuhusu wahitimu wake umeonyesha kuwa asilimia 59 wameajiriwa katika taasisi mbalimbali za umma na binafsi.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa chuo hicho, Profesa Edda Lwoga wakati wa kongamano la kuimarisha fursa za ajira na maendeleo endelevu ya Tanzania kaulimbiu ikiwa ni ‘ubunifu na ujasiriamali kwa ajira endelevu’

Mgeni mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe, ambaye alimwakilisha Waziri Dk Selemani Jafo.

Alisema utafiti huo umeonyesha kuwa asilimia 20 ya wahitimu wake wamejiajiri wenyewe na asilimia 21 bado wanatafuta ajira.

“La kufurahisha asilimia 96 walionyesha utayari wao wa kuipendekeza CBE kwa wengine na matokeo haya yanatuonyesha kwamba CBE bado tunatoa elimu sahihi na tunaenda kuiboresha zaidi kuendana na wakati,” alisema

“Ufuatiliaji huo umesaidia kutujengea taswira nzuri kwenye jamii kama taasisi bora ya kuandaa wahitimu wenye uwezo chuo hiki pia kinaunganisha wahitimu na waajiri na mfano mwaka jana walipohitimu 100 waliomaliza usimamizi wa biashara waliajiriwa Shirika la Reli (TRC), alisema

Alisema hiyo inaonyesha kuwa elimu inayotolewa chuoni hapo inachochea ubunifu na inahitajika kwenye soko la ajira na wahitimu wengi wanauwezo wa kujiajiri wenyewe.

Prof alisema CBE imeanzisha utaratibu wa kuajiri baadhi ya wahitimu wanaofanya vizuri zaidi kwenye masomo yao kama walimu wa kujitolea chuoni hapo ambao wamekuwa wakifundisha na kusimamia wenzao.

“Wenye GPA zaidi ya nne huwa tunawahamasisha waombe nafasi hapahapa CBE na wakipata nafasi wanachukuliwa kwenye kampasi zetu zote na pamoja na kuboresha mitala yetu tuna uhusiano mzuri na taasisi binafsi na serikali na za nje ya nchi” alisema

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mmoja wa wahitimu wa zamani wa chuo hicho, Maeda Waziri alimpongeza Profesa Lwoga kwa mageuzi makubwa aliyofanya chuoni hapo.

“Mimi nilisoma hapa miaka mingi iliyopita, CBE haikuwa hivi ilivyo leo mambo mengi yamefanyika ya kitaaluma na hata majengo yameongezeka kwa kasi kubwa sana lazima tumpongeze Profesa Lwoga kwa kazi nzuri,” alisema

“Najivunia kusoma CBE kwani nimepata tuzo nyingi sana na kwa sasa Tanzania nzima mwanamke ambaye ni mkandarasi wa barabara daraja la kwanza niko peke yangu. Kwa hiyo mnaweza kuona sikwamba nilipata elimu tu hapa ila niliondoka na msingi mzuri sana,” alisema

Alisema bila kuwa na ujuzi wa biashara ambayo mtu anaenda kuifanya inakuwa ngumu sana kwake kufanikiwa hivyo elimu aliyoipata CBE ilimjengea uwezo wa kutambua fursa, kuzifanyia kazi na kukabiliana na changamoto.

“Elimu ya hapa ilinipa utambuzi wa kufanya mambo sahihi na siyo kwa hisia na ndiyo maana niliweza kufanya mambo makubwa na nimepata tuzo nyingi sana hapa nchini,” alisema 





Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw.Salvator Chuwa ,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 20,2025 jijini Dodoma kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Duniani yanayotarajia kufanyika Juni 25,mwaka huu jijini Dodoma.

....

TUME ya Ushindani (FCC) imependekeza kuanzishwa kwa kozi maalum katika vyuo vya elimu ya juu nchini itakayolenga kuwajengea vijana uwezo wa kitaalamu wa kutambua na kupambana na bidhaa bandia, ikiwa ni mkakati wa muda mrefu wa kulinda walaji na soko la haki.

Hayo yamesemwa leo Juni 20,2025 jijini Dodoma na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw.Salvator Chuwa, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Duniani yanayotarajia kufanyika Juni 25,mwaka huu jijini Dodoma.

Aidha Chuwa, amesema elimu kwa umma ndio silaha madhubuti ya kupambana na biashara ya bidhaa bandia, na kwamba vijana wa vyuoni wanapaswa kupewa nafasi ya kuwa mabalozi wa mabadiliko katika jamii kupitia elimu hiyo.

“Tumeendelea kushirikiana na vyuo vikuu kama SUA, UDOM, UDSM, Mzumbe, St. Augustine, MUST na vingine kwa kutoa semina juu ya athari za bidhaa bandia. Tunashauri elimu hiyo sasa iende kuwa sehemu ya mitaala ya kudumu ya vyuo,” amesema Chuwa

Amesema lengo ni kuhakikisha kuwa taifa linajenga kizazi kinachoelewa thamani ya miliki bunifu, haki za watumiaji na madhara ya bidhaa bandia kiuchumi na kiafya. “Tunataka vijana waelimike kabla ya kuwa waathirika au wadau wa mifumo inayohalalisha bidhaa haramu,” anasisitiza.

FCC imekuwa ikitoa elimu kwa makundi mbalimbali ikiwemo Wakuu wa Mikoa, wabunge, wajasiriamali, vyombo vya habari, na wafanyabiashara wa Kariakoo, kupitia semina, warsha na makongamano.

Ngasongwa amesema elimu hiyo imeongeza ushirikiano baina ya FCC na taasisi kama ZFCC (Zanzibar), ACA (Kenya) pamoja na Chama cha Wakala wa Forodha (TAFA), katika mapambano ya kimkakati ya kikanda dhidi ya bidhaa bandia.

Aidha, amesema wito huo unakwenda sambamba na juhudi za kitaifa katika kukuza uchumi wa ubunifu na kuimarisha nafasi ya Tanzania katika Soko Huru la Biashara Afrika (AfCFTA), ambalo linahitaji bidhaa bora na halali kutoka kila nchi mwanachama.

FCC imetoa rai kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kushirikiana na vyuo husika kutathmini uwezekano wa kuanzishwa kwa moduli au mtaala maalum wa “Uchunguzi wa Ubora na Uhalisia wa Bidhaa” kwa ngazi ya stashahada na shahada.

Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Duniani kitaadhimishwa Juni 25, 2025 katika Ukumbi wa Mabeo, jijini Dodoma na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo,ambapo vijana kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini watashiriki kupitia mijadala na maonyesho ya ubunifu wa bidhaa halali.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw.Salvator Chuwa ,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 20,2025 jijini Dodoma kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Duniani yanayotarajia kufanyika Juni 25,mwaka huu jijini Dodoma.



Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw.Salvator Chuwa ,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 20,2025 jijini Dodoma kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Duniani yanayotarajia kufanyika Juni 25,mwaka huu jijini Dodoma.



Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC Bw.Salvator Chuwa ,akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 20,2025 jijini Dodoma kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Udhibiti wa Bidhaa Bandia Duniani yanayotarajia kufanyika Juni 25,mwaka huu jijini Dodoma.


Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu,akitoa maoni kuhusu shughuli za udhibiti wa huduma za nishati na maji, alipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali,jijini Dodoma.

......

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Mhe. Deus Sangu, amesema Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ni miongoni mwa taasisi za umma zilizofanikiwa kuonesha matokeo ya utumishi wenye tija kwa wananchi kupitia usimamizi makini wa huduma muhimu nchini.

Mhe.Sangu ameyasema hayo leo Juni 20,2025 mara baada ya kutembelea banda la EWURA kwenye maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma.

Ameeleza kuwa EWURA imefanya kazi kubwa kupambana na changamoto zilizokuwa zikiwasumbua Watanzania, hasa tatizo la uchakachuaji wa mafuta ambalo sasa limebaki historia.

“Nawapongeza kwa dhati kwa kazi mnayofanya,zamani wananchi walilalamikia mafuta feki kila kona, lakini leo hatusikii tena tatizo hilo,huu ni ushahidi kuwa EWURA inatekeleza wajibu wake kwa umahiri mkubwa,” amesema Mhe. Sangu.

Aidha ameongeza kuwa EWURA inalo jukumu kubwa la kuendeleza jitihada hizo kwa kuhakikisha walaji wanalindwa zaidi, huku wazawa wakipewa nafasi katika miradi ya sekta ya nishati na maji kupitia usimamizi thabiti wa maudhui ya ndani, ili kuhakikisha Watanzania wananufaika na rasilimali za nchi yao.

Mhe.Sangu amehitimisha kwa kusisitiza kuwa mfano uliowekwa na EWURA unapaswa kuigwa na taasisi nyingine za umma kwa kuwa ni kielelezo cha utumishi wenye ufanisi, uwajibikaji na unaoweka mbele maslahi ya wananchi.

Naye Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa EWURA ,Tobietha Makafu,ameeleza kuwa maonesho hayo yamekuwa fursa ya kusikiliza maoni ya wananchi, kutoa elimu kuhusu haki na wajibu wa watumiaji wa huduma, na kujenga uhusiano wa moja kwa moja kati ya taasisi hiyo na jamii.



Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu,akipata maelezo kutoka kwa Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa EWURA ,Tobietha Makafu,mara baada ya kutembelea Banda la EWURA,katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.



Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu,akitoa maoni kuhusu shughuli za udhibiti wa huduma za nishati na maji, alipotembelea banda la EWURA, katika maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali,jijini Dodoma.



Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus Sangu,akipokea zawadi kutoka kwa Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa EWURA ,Tobietha Makafu,mara baada ya kutembelea Banda la EWURA,katika maonesho ya wiki ya Utumishi wa umma yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.
Namtumbo_Ruvuma.

Serikali inatarajia kuanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji katika Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, mkoani Ruvuma, unaotarajiwa kuongeza uzalishaji wa maji kutoka lita milioni 1.4 hadi milioni 3.57 kwa siku na kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi kutoka asilimia 58 iliyopo sasa hadi asilimia 95.

Akizungumza wakati wa kusaini mkataba wa mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Namtumbo (NAUWASA), Mhandisi Francis I. Meddah alisema kuwa mradi huo unatekelezwa chini ya usimamizi wa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kuboresha huduma za maji kwa wananchi kufatia maono ya Rais ya kumtua mama ndoo kichwani.

Mradi huo utahusisha ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita milioni moja, ununuzi na ulazaji wa mabomba yenye kipenyo cha kati ya inchi 6 hadi 16 kwa umbali wa mita 30,000. Pia, ujenzi wa banio (inteki) katika mto Libula na upanuzi wa chanzo cha maji cha mto Likiwigi vilivyopo kijiji cha Libango ni sehemu ya utekelezaji wa mradi huo.

Kazi nyingine ni pamoja na ununuzi na ufungaji wa dira za malipo ya kabla (prepaid meters), ujenzi wa jengo la ofisi na uzio wake, pamoja na ununuzi wa kompyuta, samani, gari aina ya Toyota Hilux na pikipiki sita kwa matumizi ya ofisi.

Mradi huo mkubwa wa maji wenye thamani ya Shilingi bilioni 6.6. Mradi huu unalenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama kwa wakazi wa Mji wa Namtumbo na unasimamiwa na wakandarasi wawili; M/S GOPA Contractors (T) Ltd kwa kazi za ujenzi, na M/S Pipe Industry Co. Ltd kwa kazi za usambazaji wa mabomba.

Amesema Watendaji wa kata na vijiji vilivyo kwenye maeneo ya mradi wamealikwa kushiriki ili kwenda kuutambulisha mradi kwa wananchi wao na kuwaambia kuwa mradi huo hautatoa fidia kwa maeneo yatakayopitiwa na mabomba au miundombinu mingine, kwani kazi zitafanyika kwenye maeneo ya pamoja.

Mradi huo unatarajiwa kunufaisha wakazi wapatao 45,902 katika maeneo ya Namtumbo Kati, Minazini, Kidugaro, Bomani, Lusenti, Mitalulaya, Magereza, Ushirika A na B, Uyaoni, Kisutu, Tembo, Tigotigo, Nasuli, Tanesco, Gongo la Mboto na Changarawe.

Kwa sasa, NAUWASA huzalisha lita milioni 1.5 kwa siku huku mahitaji halisi yakiwa ni lita milioni 3.5, na huduma ya maji safi mjini Namtumbo inapatikana kwa asilimia 58 pekee. Changamoto nyingine ni uchakavu wa miundombinu, uwezo mdogo wa matenki ya kuhifadhia maji, ukosefu wa mtandao wa mabomba kwenye maeneo mengi ya mji wa Namtumbo na ukosefu wa jengo la ofisi ya mamlaka hiyo.

Mhandisi Meddah alisema usanifu wa mradi huu umezingatia mahitaji ya sasa na ya baadae kwa kipindi cha miaka 20 hadi mwaka 2045, Wizara ya maji ilitoa kibali cha kutangaza zabuni ya mradi huo ili kuwapata Wazabuni wa kutekeleza mradi na utekelezaji rasmi utaanza mara baada ya kusainiwa kwa mikataba na upatikanaji wa msamaha wa kodi ya VAT.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa wilaya ya Namtumbo Ngollo Malenya amepongeza hatua hiyo muhimu, akibainisha kuwa ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya awamu ya sita katika kuhakikisha huduma za maji zinaboreshwa kwa wananchi wa maeneo ya vijijini na mijini. Amehimiza wananchi kutoa ushirikiano wa karibu kwa mkandarasi ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Aidha, DC Ngollo ametoa wito kwa viongozi wa mitaa na vijiji kushirikiana na NAUWASA katika kusimamia utekelezaji wa mradi huo, akisisitiza kuwa maji ni huduma ya msingi na haki ya kila Mtanzania.

Hafla ya utiaji saini imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini, wananchi wa Namtumbo, pamoja na wadau wa maendeleo waliokuja kushuhudia hatua hiyo muhimu ya uboreshaji wa huduma za kijamii.






Na Mwandishi Wetu

MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeingia Makubaliano na Tume ya TEHAMA kwa ajili ya kuendeleza Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika vyuo saba vya VETA vya wilaya kwa kipindi cha miaka mitano.

Akizungumza  mara baada ya kusaini makubaliano hay oleo, tarehe 20 Juni 2025,  Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA. Anthony Kasore amesema kuwa Tume ya TEHAMA itasaidi katika kuongeza ujuzi katika masuala ya Teknolojia kwenye vyuo vya VETA.

Amesema kuwa suala la Teknolojia linakuwa kila siku hivyo ni fursa ya vijana kupata ujuzi wa teknolojia ya TEHAMA kabla ya kuingia katika soko la ajira.

Amevitaja vyuo saba vitavyonufaika na makubaliano ya mafunzo ya TEHAMA ni katika Wilaya za Mpanda, Singida, Njombe, Morogoro, Songea, Mpanda pamoja na Singida.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA, Dkt. Nkundwe Mwasaga amesema kazi ya tume yake itakuwa ni kuweka vifaa vya TEHAMA katika karakana za vyuo hivyo.

Dkt. Masaga amesema kuwa moja ya majukumu ya Tume ya hiyo ni kuendeleza TEHAMA nchini ambapo vijana ndio fursa yao kuingia na kuonyesha ubunifu.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

NAIBU Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Danstan Kitandula (Mb), ameipongeza Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa jitihada zake katika kukuza sekta ya nyuki kupitia uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zenye viwango vya ubora.

Pia ameitaka TFS kuongeza ubunifu zaidi katika vifungashio na taarifa za kitaalamu zitakazomsaidia mlaji kuelewa thamani ya bidhaa hizo.

Akizungumza baada ya kutembelea banda la TFS katika maonesho ya wiki ya utumishi wa umma yanayoendelea kwenye viwanja vya Chinangali Park jijini Dodoma,Naibu Waziri Kitandula amesema bidhaa za nyuki, ikiwemo asali na nta, zina mchango mkubwa katika maendeleo ya kiuchumi na afya ya wananchi, na hivyo zinahitaji mikakati ya kuongeza ushindani sokoni.

“Ni jambo jema mmeweka korosho na asali pamoja, lakini mteja haelewi mchanganyiko huu unamnufaishaje kiafya, wala kiwango cha utafiti uliofanyika. Hili ni eneo muhimu la kuboresha. Toeni maelezo ya kina yanayomsaidia mlaji kufanya maamuzi sahihi,” amesema.

Amesisitiza bidhaa hizo, ambazo hutengenezwa kwa kutumia rasilimali asilia, zinaweza kuwa chanzo kikubwa cha ajira na kipato kwa vijana na wanawake vijijini iwapo zitafungashwa na kutangazwa kwa weledi wa kibiashara.

Kwa upande wake, Ofisa Mwandamizi wa Uhifadhi kutoka TFS, Emiliana Kiwango, amemueleza Naibu Waziri kuwa TFS imejikita katika matumizi ya mifumo ya kidijitali katika kutoa huduma na kusimamia biashara ya mazao ya misitu na nyuki, sambamba na mwelekeo wa serikali ya awamu ya sita ya kuimarisha sekta ya umma kupitia teknolojia.

“TFS tumeweka kipaumbele katika matumizi ya teknolojia za kisasa, hasa mifumo ya kidijitali, katika utekelezaji wa majukumu yetu ya uhifadhi, uzalishaji na biashara ya mazao ya misitu na nyuki. Tunaendelea kuimarisha miundombinu ya utendaji kazi na kuifikia jamii kwa njia rafiki na bora zaidi,” amesema Kiwango.

TFS kupitia Idara yake ya Nyuki imekuwa ikihamasisha wananchi, hasa katika maeneo ya vijijini, kujihusisha na ufugaji nyuki kwa lengo la kuongeza kipato, kuhifadhi mazingira, na kuongeza tija katika matumizi ya rasilimali za misitu kwa njia endelevu.

Maonesho ya wiki ya utumishi wa umma kwa mwaka 2025 yamebeba kaulimbiu isemayo “Utoaji wa Huduma Bora kwa Umma ni Msingi wa Maendeleo Endelevu”, yakiwa na lengo la kuhamasisha uwajibikaji, ubunifu na matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma.

Kwa mwaka huu, TFS inashiriki kwa kuonesha bidhaa za nyuki, huduma za kidijitali kama mfumo wa e-Misitu, pamoja na mafanikio ya uhifadhi wa misitu ya hifadhi za taifa, misitu ya asili, na programu za uwekezaji katika ekolojia endelevu ya misitu na nyuki.



Na Mwandishi Wetu

Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeingia Makubaliano na TanChin International kwa ajili wanafunzi wa VETA kupata ujuzi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu kwa kutumia chuma.

Akizungumza mara baada ya kusaini makubaliano hayo Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA. Anthony Kasore amesema kuwa katika ushirikiano huo wanafunzi wanaosoma VETA watapata mafunzo ya ujenzi wa nyumba hizo pamoja kuwa sehemu ya miradi ya Tanchin katika kujifunza kwa vitendo.

Amesema kuwa moja ya nyumba ya mfano ya Tanchin itajengwa chuo cha VETA Kigamboni na wananchi wa eneo hilo watajifunza kupitia mradi huo.

Amesema kuwa VETA itatoa ushirikiano wa kutosha kwa TanChin katika kufanikisha makubaliano hayo kuwa matokeo chanya.

Aidha amesema ujenzi wa nyumba 

 hivyo ni fursa kwa VETA kupata kozi zinazoendana na mabadiliko ya teknolojia.

Amesema kuwa TanChin itatoa wataalam wa kufundisha wanafunzi wa VETA na baada hapo kupata mafunzo ya vitendo na baadae kuwa fursa ya ajira kwao.

Mkurugenzi wa TanChin Mansoor Khalfan amesema kuwa wanashukuru kuwa na makubaliano na VETA kutokana VETA inq vyuo nchi nzima na ni rahisi kuwafikia vijana wengi.

Amesema kuwa katika mafunzo hayo wanafunzi wa VETA watapata ujuzi wa ujenzi huo wa nyumba za chuma na kuwa na mchango katika sekta ya ujenzi wa nyumba nchini.

Kwa upande Mkurugenzi wa TanChin Paul Hu amesema kazi yao kupeleka teknolojia hiyo kwa watanzania kupitia VETA.
Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Kasore akisaini mkataba  wa Makubaliano na Mkurugenzi wa TanChin International Mansoor Khalfan kwa ajili ya Wanafunzi wa VETA kufundishwa ujenzi wa nyumba kwa kutumia chuma,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Kasore akizungumza mara baada ya  kusaini mkataba  wa Makubaliano na TanChin  International  kwa ajili ya Wanafunzi wa VETA kufundishwa ujenzi wa nyumba kwa kutumia chuma,jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi TanChin International Mansoor Khalfan  akizungumza mara baada ya  kusaini mkataba  wa Makubaliano na TanChin  International  kwa ajili ya Wanafunzi wa VETA kufundishwa ujenzi wa nyumba kwa kutumia chuma,jijini Dar es Salaam.


Na Janeth Raphael MichuziTv -Dodoma

Imeelezwa kwamba vituo saba vya Tanzania Bara vimefanikiwa kuendesha mitihani ya BODI ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) ambapo jumla ya watahiniwa 1,506 walisajiliwa na 1,421 waliratibiwa kufanya mitihani.

Taarifa hiyo imetolewa Jijini Dodoma leo na Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB Godfred Mbanyi ambaye amesema kwa ujumla watahiniwa walifaulu mitihani yao, huku 610 wakitakiwa kurudia baadhi ya masomo na 131 wamefeli mitihani yote.

Amebainisha, “Masomo yaliyofanywa vizuri zaidi ni Michakato ya Zabuni na Majadiliano ya Kimkataba, ambapo watahiniwa walionyesha uelewa mzuri na matokeo chanya,”

Aidha Bodi imeainisha masomo yanayohusisha hesabu yameendelea kuwa changamoto kubwa kwa watahiniwa wengi, hivyo ipo haja ya kuwepo kwa maandalizi mazuri zaidi ili kufikia viwango vinavyokusudiwa.

Katika hatua nyingine, uongozi wa Bodi umewapongeza watahiniwa waliopata mafanikio na kuwataka wahadhiri kufuata maelekezo ya Bodi katika kutoa mafunzo ili kuhakikisha Nchi inazalisha wataalamu bora wenye mchango katika maendeleo ya Taifa.

Huku mkazo ukiwekwa kwa watahiniwa waliopata changamoto katika mitihani hiyo kujiandaa vyema kwa ajili ya mitihani ya marudio itakayofanyika mwezi Novemba mwaka huu, huku wazazi na walezi wakihimizwa kuendelea kuwapa moyo vijana wao.

Ameongeza kusema, "Moja ya changamoto iliyojitokeza katika mtihani huo ni baadhi ya watahiniwa kujihusisha na vitendo vya udanganyifu kutokana na maandalizi duni, hali iliyotajwa kuwa kinyume na maadili ya taaluma hiyo inayohitaji uadilifu wa hali ya juu,”


Na Mwandishi wetu - Dodoma

Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya jiji la Dodoma Joseph amesema vikundi 467 vinatafutwa na halmashauri hiyo kwa ajili ya kurejesha mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na Serikali kwa vikundi vya wanawake,vijana na watu wenye ulemavu hapa Nchini.

Fungo ameyabainisha hayo leo jijini Dodoma katika semina ya mafunzo yaliyoandaliwa.na Benki ya CRDB kwa vikundi vilivyokidhi kupata mikopo ya asilimia 10,toka isimamishwe na Serikali kutolewa na halimashauri, badala yake itatolewa na Benki zilizoidhinishwa.

Fungo amesema fedha hizo ni deni ambalo liko mikoni mwa vikundi ambavyo vimekopeshwa na kukimbia na mikopo bila kuirejesha kwa wakati ili watu wengine nao wakopeshwe kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao.

"Deni la shilingi bilioni 1.2 liko mikononi mwa vikundi ambavyo vimekopeshwa bado tunaendelea kuwatafuta ili wazirejeshe na wengine wapate mikopo,"alisema Fungo.

Aidha amesema hivi sasa Halmashauri hiyo imetenga shilingi bilioni saba kwa ajili ya kuvikopesha vikundi ambavyo vitakidhi vigezo kutokana na kutembelewa na Benki ya CRDB ambayo imo kwenye orodha ya utoaji mikopo hiyo kwa makundi hayo.

Aidha mpaka sasa vikundi 12 kati ya 126 vilivyokabidhiwa kwa CRDB vilivyofuzu kupewa mikopo ni vikundi 12 huku vingine vikikutwa na kasoro ndogo ndogo ambazo benki hiyo kupitia wataalam wake wa utoaji elimu kuhusu matumizi ya fedha lakini pia kuwakagua biashara wanazofanya kama inakidhi mikopo walioomba.

"Naomba nyie mliokidhi vigezo vya kupata mikopo mkairejeshe kwa wakati tunahitaji kuona mtiririko wa urudishaji unakuwa bora kulingana na masharti ya uchukuaji kuboreshwa,"alisema Fungo.

Naye Bahati Atanasio mwanakikundi cha vijana kutoka Kata ya Chihanga ameiomba serikali kupitia halmashauri kutoa mikopo sahihi ilioombwa na vikundi ili mikopo hiyo iweze kukidhi mahitaji yao ya biashara walioiombea.

Atanasio amesema chanzo kikubwa cha vikundi kukimbia na mikopo ni kutokana na vikundi kupata mikopo midogo tofauti na ile ambayo wameomba kitendo ambacho kinapelekea wanakikundi kugombana na kila mmoja kutoweka.na kuacha kurejesha mikopo.

Kutokana na hilo,ameiomba Serikali kupitia halmashauri zake kutoa mikopo kiasi kamili ambacho kikundi kimeomba ili waweze kutimiza malengo ya kikundi kitendo ambacho kitaepusha watu kukimbia na mikopo.

Naye Mkuu wa Kitengo wa Idara ya biashara ya biashara cha CRDB Benki Foundation Fadhili Bushagoma amesema wametembelea vikundi vote 126 kwa kushirikiana na ofisi ya halmashauri ya jiji la Dodoma,lakini vilivyo kidhi vigezo mpaka sasa ni vikundi 12 ambavyo viko tayari kupewa mikopo.

Bushagoma amesema vikundi vingine vimekutwa na changamoto mbalimbali ikiweno biashara waliotaja ni ndogo kuliko mkopo walioomba na kuongeza kuwa ambao hawajakidhi vigezo bado wana nafasi ya kujirekebisha ili wapate mikopo hiyo.

Mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri mbalimbali ilisitishwa kutolewa na Serikali ambapo hivi sasa imeaanza kutolewa na benki zilizoidhinishwa lengo ikiwa ni kupata walengwa wenye vigezo kutoka kwa wataalam wa fedha wa Benki.









Top News