azikiwe avenyuu


hapa ni samora avenyuu. atm za bongo zina karaha zake, hasa ukizingatia uchache wa mashine hizo na wingi wa wateja. wadau kifanyike nini kupunguza ama kuondoa adha hii??

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 22 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2007

    Mr. Michuzi asante sana kwa umakini wa blog yako.
    Tatizo kama hili litaweza kupunguzwa kwa kuweka hizo cash mashine katika sehemu muhimu kama vile main post office,some hotels, na katika maduka na hizo mashine ziwe rahisi kuonekana kwa watumiaji.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 01, 2007

    Duh utazania miaka ile watu wakiline up kununua sukari au sabuni

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 01, 2007

    Tatizo la tanzania ni kuwa watu hawamweshimu mteja due to lack of competititon. Hiyo ni hela yake kaiweka na bank inaitumia kuinverst na kupata faida kila siku. Mteja akija kuchukua hela yake asimame mda wote huu.

    Kuondoa mushki huu kungetakiwa kuwa na nyingi za bank tofauti . Ili kama huna good service wateja hupati lakini kama sio hivyo basi line zitakuwako kila siku

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 01, 2007

    kaka michuzi mimi nashangaa kwanini vitu kama hivyo navyo vinakuwa na msongamano kama barabara za bongo?hizo ATM zinatakiwa ziwe kila mahala kwenye mkusanyiko mwingi wa watu sasa hizo atm zimewekwa mijini lazima kutakuwa na msongamano,hao wamiliki wa mabank lazima waongeze hizo machine.(saddiqj)toronto CA

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 01, 2007

    Kaka Michuzi, tatizo letu wabongo huwa tunavamia kuandaa kitu kwa kufuata mikumbo tu ili nasi tuonekane tunakwenda na wakati lakini akchuali kunakuwa bado hakujafanyika maandalizi ya kutosha ya kuweza ku-sastein hayo mabo tunayoyaanzisha au kuanzishiwa na wafadhili.
    Hapo unaweza kukuta ni kwamba mashine zilikorofisha hapo siku hiyo, au umeme ulikuwa umekatika kwa masaa kadhaa! Vandumwe!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 01, 2007

    ma benki yanatakiwa kuweka ATM's ili kurahisisha na kufanya huduma za benki ziwe sio za usumbufu (jinsi ya kutoroka foleni ndani ya benki na kutumia atm)..yani making baking services more convenient and user friendly. Sasa unaonekana bongo ni opposite kabisa, badala ya ATM's kurahissha huduma za benki watu wanapigwa jua wakiwa foleni. sasa benki za na weka hizo atm za nini kama situation bado ni ni sawa tu kwanza its even mbaya zaidi kwasababu ya jua, na haamna AC mtaani.. waki taka kuondoa hilo tatizo wasambaze ATM zaidi, tena wa weke strategically yani sehem watu wako kwa wingi kama stendi za basi za mikoa, mwenge, au hata petrol stations. yani uk kuna ATM 30,000 tanzania hazi zidi 150. si semi tuwe na 30,000 ila tuongeze idadi kidogo maana haina maana kuwa na ATM'S KAMA WATU WATA PIGA FOLENI TENA!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 01, 2007

    HAPO NI KUSOMANA NA KUIBIANA KWA KWENDA MBELE NIKIMSOMA DADA WA MBELE HAPO NIKAPANGA MISSION NA MTU KWA SIMU AMVIZIE MAHALA FULANI SITAPATA HELA YOTE YA HUYO DADA? MBONA WATZ HATUJUI TUNAKOKWENDA NA TUNACHOTAKA?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 01, 2007

    hizi cash point ziko chache na ni maeneo ya mjini ambapo usalama kidogo ni mwingi, kwa mitaa ya uswahilini usalama mchache naona zitazidisha vitendo vya ujambazi, mashine kama hii kuiweka mitaa ya manzese si hatari? tusisahau bado wa-tz tuko mbali kimaendeleo na umasikini bado upo kiwango cha juu, mitaa mingine bado jambazi anaweza akakukaba kwa kuiba alfu ishirini yako!!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 01, 2007

    Bado tunasafari ndefu kwani ATM inabidi ziwe nyingi karibia kila mahali hadi kwenye grocery stores, lakini kwa nchi ya waungwana kama Tanzania usalama ni tatizo. Hiyo foleni yenyewe inavutia vibaka na ni hatari kwa wateja. Lakni ufumbuzi ni kuwa na mashine nyingi iwezekanavyo.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 01, 2007

    Watanzania kwa kuiga mambo tu hatujambo. Sasa maana ya ATM ni kurahisisha uchukuaji wa hela ili usiende bank kupnga foleni lakini matokeo ya hizi ATM za Tanzania ni kinyume yaani foleni kuliko Bank. Hatuna uandaaji wa makini, alitokea mtu tu akasema tuwe na ATM basi wakakurupuka tu na kuweka ATM bila kuangalia maeneo, au umeme ukikatika, utengenezaji wa hizo mashine zikikorofisha etc..hakuna plan iliyotumika matokeo yake ndio hzi foleni...mtu mzima hovyoo. Sijui tutaendelea lini?

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 01, 2007

    Hizo cash machines zinaweza pia kuendeshwa na makampuni binafsi. Sijui kwa Tanzania kama hilo litawezekana kutokana na maendeleo ya teknolojia hiyo. Sehemu zingine duniani mfano UK utakuta hizo cash machine zipo kwenye petrol stations, super markets, mitaani na sehemu nyingine zenye mkusanyiko mkubwa wa watu na zinaendeshwa na makampuni binafsi. Mtu unaweza kuchukua pesa from any cash machine bile ya kujali wewe ni mteja wa bank gani.

    Suala la miundo mbinu la Tanzania linaweza kuchangia hali hii ya kuwa na foleni kubwa kwenye ATMs. Mfano umeme usio na uhakika ni sababu mojawapo. Pia suala la mabenki mengine kuwa na link kwanza na ofisi zao Afrika ya kusini au Nairobi pia inachangia. Kukiwa na tatizo dogo tu utaambiwa ngoja tuwasiliane na watu wa Nairobi au Afrika ya kusini ili watatue tatizo.

    Bado tuna safari ndefu kabla ya kufika tunapotaka ila ninaamini kuwa ipo siku tutafika tu!!

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 01, 2007

    Mimi nashauri tusiwe tunaweka hela Bank, sababu kwenda kuiweka ni folen ya kutisha kuichukua folen pia, sasa ukiangaliua unachokifanya ni kupoteza muda.

    Lakini kuna Bank kama NBC shida yake huwa ni wakati wa kudeposit lakini kwenye ATM zake folen huwa sio kali, lakini hizi Bank nyingine ni Balaa tupu

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 01, 2007

    Utadhani watu wanaenda kuchukua sukari ugawaji

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 02, 2007

    First you have to find out why people are getting money from ATM's. I was back there in 2005. Non of the stores accept those cards. So, people have to get cash to buy almost everything. The first thing, financial institutions have to work with retailers to install machines at the point of sell so that people should not have to get cash frequently. Who ever brought this idea didn't understanding very well the reason for this ATM centers. The banks need to work together with retailers and other cooperations involved in payments in order to minimize this issue. That's the key. The way the system works now , to me,is same as carrying cash. It is less work for bank tellers, but more assle for customers. Is even riskier because you are getting money outside, infront of everybody.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 02, 2007

    ASANTE SANA KWA KULETA HII KWENYE BLOGU YAKO, HAKYA NANI YANI HAWA WATU WA ATMS HAWANA MPANGO KABISA UTAFIKIRI HAWANA MARKETING MANAGER?? YANI TAREHE 30.YA MWEZI ULIOPITA NILIPATA TABU KWELI, TENA KAMA ULIKUWEPO HAYO HAYO MA - ATM ULIYOYATOA NDO YALINTOA JASHO BASI NILIANZA KWENDA APO SAMORA AVENYUU ATM IKAANDIKA SORRY OUT OF SERVICE, NIKAJA HAPA ASKARI MONUMENT LIKAWA LIMESTUCK YANI LIMEGOMA, ILE FOLENI KUBWA TULIOKUWA NAYO IKAANZA KUJADILI KWENDA KARIAKOO DDC AU MILENIUM TOWER, NIKAANZA SAFARI YANGU YA DDC -KARIAKOO, LIKAANDIKA YOUR TRANSACTION CANCELLED, SIO MIMI TU WENGI WETU ILIJIANDIKA HIVYO, BASI BILA KUPOTEZA TENA MUDA NA SAA ILIKUWA SAA 12 ZA JIONI, IKABIDI KUCHUKUA TENA BASI LA MWENGE, NDO KUSHUKIA MILENIUM TOWER, FOLENI NILIOIKUTA HUKO BALAA TUPU NILITOKA PALE SAA MOJA NA NUSU USIKU, SITASAHAU SIKU HIYO. HIVYO MICHUZI KUBORESHA JINA NA BLOGU YAKO NAKUOMBA NENDA OFISINI KWAO UKIWA UMEPRINT HAYA MAONI YETU ONGEA NAO KUHUSU SUALA HILI NA WATU TUNAVYOTESEKA JUU YAO HAO WAPENDA KUCHUKUA HELA ZA WATU BILA KURIDHISHA WATEJA. WAZO LA HAPO JUU ZURI SANA KUWA WAYAWEKE SEHEMU KAMA HOTELINI, SHOPS, SUPERMAKETS MA KWINGINEKO.
    YANI AKILI ZAO HAZIFANYI KAZI, NA LAITI WANGELIKUWA NA MASANDUKU YA MAONI PALE KWENYE HAYO MA- ATM YAO, SIKU ILE WANGEKUTA MAVI ZAWADI YAO , TULICHUKIA SANA.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJuly 02, 2007

    HII Mistari ni ya Posta za USA. Ukienda posta especilly jumamosi ni tabu tupu...msitari kama huu. lakini uzuri ndi ndani na AC. Kila kitu chenye monopoly taabu sana

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 03, 2007

    Mheshimiwa Issa AKSANTE KWA LUGHA YA PICHA...SASA KAMA MWANAMUME AKIPANDWA NA "..MARADHI GHAFLA.." SIATA PELEKWA JELA..INCHI YETU INABIDI "..USTAHIMILI.."..Hiyo foleni inahitaji uvumilivu mkubwa

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 03, 2007

    Wahusika wa ATM hizi wanatakiwa kutafuta suluhisho la tatizo hili. Naamini shida siyo namba ya watumiaji ila ni kasi ya kufanya kazi kwa ATM hizi. Mtandao wao upo slow sana.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 03, 2007

    wee hapo uliyesema hiyo ni mistari ya posta USa ...unaishi US ya wapi? seems unaishi korea wewe huku States hakuna shida kama hizo na ukienda bank kama US bank ukikaa zaidi ya dakika tano kwenye foleni wanakulipa dola na misamaha mingi sana...inaitwa 5 star service na posta hakuna foleni kama hizo za mdau wa north korea....jamani Bank ongezeni hizo ATM ni faida kwenu na wateja wenu au na watu binafsi waanzishe za kwao ni rahisi sana

    ReplyDelete
  20. AnonymousJuly 04, 2007

    Walivyowapumbavu hao watu wabank, ukikuta ATM haifanyikazi, ukienda ofisini kuchukua pesa wanakukatalia wanakuambia uende sehemu nyingine, Mimi hata siwaelewi hapo.
    Kuweka wala hawakusumbui, kwavile wanapata faida, pumbavu kabisa.Huu usemi wamteja ni Mfalme wanajifanya hawaujui kabisa, kwenye kuchukua pesa yako.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 04, 2007

    Jamani naishi USA New York City. Na mnaobisha kuhusu mistari basi hamtumii posta mara kwa mara kumail packages. Posta hawaruhusi package zinazokwenda nje ya nchi kutumia self service machine.. Hivyo ni lazima u line up. Na mimi ninaendaga kama ninashida ni jumamosi....Bwana foleni ipo ingawaje posta zote zina teller zaidi ya madirisha 10 lakini foleni sana. Na tunaline up hivi hivi na hamna cha msamaha wala lini.


    Na hata USA mwanzo wa ATM zilikua chache hivi hivi. Hata TZ miaka ijayo labda zitaengezeka. Zilikua za kutafuta na zilikua zinawekwa ndani ya bank na bank ikifungwa service haipo. msione ziko kila mahali mkazania zilikua hivyo toka zilivyoanza

    ReplyDelete
  22. AnonymousJuly 05, 2007

    Hizi ATM ni zile zilizotumika ulaya miaka ya sabini, wale waliotumwa kwenda kununua kama unavyojua ujanjaujanja wa bongo kutaka kuweka kitu kidogo mfukoni wakazinunua ndio maana haziishi kusitisha huduma kwa muda kila zikihudumia watu watatu, pia ziko taratibu sana mtu mmja anahudumiwa kwa zaidi ya dakika tano na kubwa zaidi umeme hukatikakatika.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...