dk. gerald misinzo wa SUA, Morogoro, siku ya kutetea Ph.D. thesis yake yenye jina "Entry of porcine circovirus 2 and porcine reproductive and respiratory syndrome virus in their host cells" jumatatu novemba 26th, 2007 katika auditorium Hoogbouw, Faculty of Veterinary Medicine, chuo kikuu cha Ghent University, Salisburylaan 133, 9820 Merelbeke, Belgium.
habari njema ni kwamba dk. misinzo alifanikiwa katika utetezi huo na kujizolea jinondozz la Ph.D. kiulaini na hivi sasa kesharudi kuendeleza libeneke mji kasoro bahari.
KWA NIABA YA WADAU WOTE NAPENDA KUKUPONGEZA DK. GERALD MISINZO KWA MAFANIKIO HAYO NA KUREJEA NYUMBANI KUZUNGUSHA GURUMU LA MAENDELEO

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Hongera Dr. mmh! mi sijui nitafika ini huko du!

    ReplyDelete
  2. Huyu Jamaa tulisomanaye Kibaha Secondary. Hongera kwa kuukwaa Udakitari wa falsafa

    ReplyDelete
  3. Doctorz hongeraz kwa nondoz Pia Hongera kwa Leboooooz kwene sutiz

    ReplyDelete
  4. Mshikaji siungekakaa kaa ukapiga boksi kidogo bwana,na hiyo PhD yako ungeiweka pemebeni kwanza!! maana kazi huku shida sana.Mimi kuna jamaa ya Ghana anafanya PhD ya Strategic Investment,lakini tukiwa mafactory huko yeye ni mpigaji boksi kinoma,sasa tutafanya nini haya ndiyo maisha tunayojidai nayo na kuogopa kupigwa vumbi la mahome,Anaway Am on my way to the next flight to my dreamland i.e Tanzania even Madiba recognise it!I will come soon after defending my thesis as well in Confusion and irrational Idiosyncratic behaviour. Because the issue of cross culture has great impact in perceptiveness view, I have tried to reviews range of hypothetical clues in regarding to the identified facts. Predominantly, most of Bloggers are fraught with similar problems that is why they tend to react vigorously in range of articles.Hey Guy! Don’t be perplexed with the sort of liberal issues.Ugenini ni ugenini na nyumbani ni nyumbani,You can be a British but not English!!! Ha ha ha ha,wajeruman husema Einmal Ausländer - immer Ausländer ha ha ha.Therefore we need to integrate this distinctive multilinking approach. However, I don’t discourage for those with white colour job with their skills and those with no skill and enjoying blue colour job, my real concern is with the group of lost intellectuals’ way of thinking.

    Dr Confusion aka mzee wa kuchanganyikiwa

    ReplyDelete
  5. Hicho ulichosomea utafanyia nini Morogoro? Rudi huku ufanya vitu vya maana halafu ulete matunda ya matokeo Tanzania. Usiogope maneno ya watu eti boksi, njoo Marekani watu wakurushie deal za ajabu. Watu wa fani yako huku wanalipwa milioni za Tanzania zaidi ya 100 kwa mwaka. Shauri yako, unaona sifa kurudi kwenye vumbi, haya!

    ReplyDelete
  6. Wewe Misinzo ulipita pale Kibaha Secondary? Nafikiri ulinitangulia mwaka mmoja. Ulikuwa CBA pale na Kina Ibrahimu Mahumi? Mie nilkuwa PCM Pale.

    ReplyDelete
  7. Hongera sana Gerald.
    Dr. Misinzo alikuwa anauza duka la shule, siku moja form one akatumwa na jamaa kwenda dukani bila kujua akaambiwa akanunue vimisinzo vitatu na vinyaulolo viwili na salio litakalobaki anunue kihabili kimoja. LoL hii ilikuwa kizunguzi. Allawi

    ReplyDelete
  8. Hongera sana Dr. Misinzo, kawapige shule vijana pale Moro, ila usiwe mnoko kama wazee utakao wakuta pale Mji kasoro bahari.

    ReplyDelete
  9. Hongera sana kwa kumaliza PhD, baada ya kurudi nyumbani wembe ule ule. Wandugu wenzangu tupunguze kulala na kuendekeza mapenzi tu. Morogoro kumetulia sana tu, ila naona wachangiaji wenzangu wameloea huku ulaya kwenye utumwa daima.
    Tanzania oyeee!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...