globu yenu hii ya jamii ina furaha kuwatakia wadau wote siku njema ya wapendanao. tukumbukue tafsiri ya kupenda sio kwa ngono bali ni mapenzi ya dhati kwa watu uwapendao ikiwa ni pamoja na ndugu, jamaa na marafiki bila kusahau mai hazbendi ama mai waifu wako, kadhalika na wadau. na mapenzi hayo yasianzie na kuishia leo tu. yadumu milele....

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Guys lets be for realy!!!! i think kwenye life yetu ya sasa kila siku inatakiwa iwe Valentaine especially kwa wife or Hub!!! hizi kasumba za kudanganyana kwa siku moja no way....

    ReplyDelete
  2. Asante Michuzi. Tunakutakia Valentine Njema wewe na Wifi yetu!! T-Shirt imekauka?? Naona ndo kivazi cha leo night!!

    ReplyDelete
  3. Kaka michu na KP nawatakia sikukuu njema ya wapendanao. Ila kaka michu sijui utakuwa na nani maana mikonozizzzz ilizidi kwa sana wakati fulani sijui kama unawakumbuka wote, anyway jipe raha mwenyewe kama ulizojipa Sauti ya busara.

    ReplyDelete
  4. Kaka sikukuu ya wapendanao naiona ila mimi sina hata pesa ya kununua ROSES ila nilichokifanya nimeanzisha songombingo na mchumba wangu tumenuniana, ila sikukuu tu ikiisha namfuata tena na mwangukia miguuni.

    ReplyDelete
  5. Anon. wa Feb 14 10:12. kanifurahisha sana yaani kaamua kuanzisha zali ili valentine wake asiombe amtoe out na baadaye a apologise. Hi kali. Mimi nadhani mapenzi ni ukweli hasa kwenye kipindi cha uchumba. Ni vizuri mchumba yako ajue mapema hali ya kiuchumi sasa ili msijeanza kusumbuana baadaye. Mwambie kuwa leo huwezi kumtoa au kumnunulia ua kwa sababu huna pesa akivumilia - haya akikuacha -haya ,utapata mwingine atakaye kuvumilia. Mimi sasa hivi ninapata shida ya kupata mchumba kwani sasa nina hela na kila mwanamke ambaye nampata huwa siamini kuwa ananipenda au kwa kuwa anafuata pesa zangu. Kipindi kizuri cha kupata mchumba mzuri ni wakati ambao huna kitu. Namalizia kwa kusema happy valentine kwa wote wenye mapenzi ya dhati.

    Livison@yahoo.com

    ReplyDelete
  6. Hey,acheni kuleta zenu za kizungu eti valentine day ....unatakiwa umpende ndugu yako na jirani yako kila siku ya Mungu,tuache kujidanganya kuwa kuonyeshana upendo ni tarehe 14/2.......Tungekuwa tungefanya hivyo hii dunia ingekuwa mahala pazuri pa kuishi na hata mafisadi wasingekuwepo
    Naomba kuwasilisha wadau

    ReplyDelete
  7. Brother Michuzi, Happy Valentines!!
    naomba kutuma ujumbe huu mahsusi kwa mpenzi wangu aliyepo masomoni Ukerewe (UK)akisoma yeye ataelewa kua ni muhusika.

    Heri ya siku ya wapendanao mpenzi wangu Mansour R., japokua uko mbali lakini mawazo yangu yote yapo kwako na natamani tungekua wote siku hii muhimu, ila naamini kila siku kwetu ni Valentines nakupenda sana Man na unajua hilo, tumepita milima na mabonde na leo bado tuko pamoja naamini tutaendelea kua pamoja Inshaallah,
    Masomo mema kipenzi changu najivunia kua nawe. Niko home nakusubiri tuanze maisha pamoja pale Mungu akipenda.
    Nakupenda sana
    Its me your girlfriend
    Anne.

    ReplyDelete
  8. Happy Valentine my lovely son Ibrahim, i will be with you shortly. just hang in there.Mummy is going to be home soon, i promise

    ReplyDelete
  9. Naam! Leo ni siku ya kupeana mavituuz hasa! Asubuhi mtakuwa hoi. Muandae chocolati, whipped cream, fukizia udi, nk. leo mambo yanoge!

    ReplyDelete
  10. Asante kwa salamu zako lakini kwangu mimi valentine ni kila siku. Si mtreat mume, watoto, familia yangu au marafiki zangu extra special today, kwa vile ni valentine's day. Mimi naona tunatakiwa kutreat watu wote vizuri kila siku.


    Upendo ni kila siku....kama ni kawine au chocolate sio leo tu uwaletee nyumbani... do that often whenever you can afford. Mpeleke mkeo au mume wako out whenever you can afford. Usisubiri mpaka valentine's day ndio ukumbuke kununua perfume au kuosha viombo.

    Ukitaka life iwe nzuri tunatakiwa tufanye vitu hivyo vinavyofanywa na wengi leo kila siku....The little litle things are the ones that keep any relationship or friendship.

    ReplyDelete
  11. Hapi valentino tu yu tuu michu
    bora hata nimepata kutoka kwako
    maana siku ilikua inakaribia kuisha bila ya kupata hata moja

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...