warembo wakipata maelezo juu ya nyumbani kwa mwalimu butiama
chifu wanzagi akiongea na warembo butiama
mamiss na msafara wao wakipata maelezo ya nyumba za butiama
mamiss wakizunguka kuangalia mandhari nzuri ya kijijini butiama
warembo wakiweka mashada ya maua kwenye kaburi la baba wa taifa butiama
hii ziara ya butiama ni mojawapo ya shughuli ambazo watembo hawa wamekuwa wanazifanya katika ziara yao ya wiki moja jijini mwanza wakati wakijiandaa kupanda jukwaani kesho usiku kwenye ukumbi wa nssf kushindania taji la balozi wa redds. ziara hii imefadhiliwa na kuratibiwa na kilaji cha redds premium cold kinachotengenezwa na tanzania breweries limited



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 18, 2008

    Mwalimu kama ninavyomuelewa angewatoa baruti. Yeye alikuwa ni mjamaa shika jembe ukalime mambo ya uzuri alikuwa haendekezi hivyo!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 18, 2008

    Bwana Michuzi, naomba nikurekebishe kidogo. Hayo maelezo yanayotolewa na Chifu Wanzagi, hayatolewi "juu ya nyumba" ila ni maelezo "kuhusu nyumbani".

    Wote wanaonekana wamesimama chini au uwanjani na siyo juu ya nyumba.

    Nashukuru kiswahili bado kinapanda pamoja na miaka hii kibao niyotokomea ughaibuni na kujifunza na kuzitumia lugha kadhaa.

    Mdau.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 18, 2008

    Hahahahaha...kweli kabisa. Kwanza wasingewaza hata kufunga hiyo safari ya kwenya huko. Labda kama wangetumia kisingizio cha kwamba wanaenda kumsaidia kupalilia mashamba yake.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 18, 2008

    huyo dada kaweka goti kwenye kaburiii, au nina malienge?

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 18, 2008

    Angewahenyesha shambani toka saa mbili hadi saa tisa alasili bila kupumzika wakipalilia au kuvuna "obhuyemba, amalingwa, obhukanhu" na mazao mengine, hasa ulezi!

    Huyo "Muswati" wa Uzanaki anaweza kujipatia mchumba...(Cheka!

    ReplyDelete
  6. Mimi bado najiuliza.
    Mara ghafla mwl anafufuka hapo sijui hao warembo wangemwambia nini.Yaaani sipati picha.Nakumbuka utu tujineno wakati uleee wa nanii wakati nanihii anataka kugombea uraisi "....Yaani Tanzania,Kenya,Uganda tuwe na vikao vyetu vya maraisi.Mara inatokea udhuru kuwa samahani ndg wajumbe rais wa Tanzanai hatofika kwa sababu ana mimba.Sitaki na nimesema sitaki.Kwetu ni Butiama bwana....."yaani wewe hapo bana tu sauti itoke orijino.Yego
    Majita

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 19, 2008

    Kwani si alipiga hii biashara vita miaka ya sitini kutokana na maadili? Au mnataka tu kumdhihaki, tumerudi!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 19, 2008

    Hivi si wanalipia hapo kwenda kupaangalia au ni bure. kama panalipiwa basi hamna hoja lakini kama ni bure na wameenda ni kumdhalilisha mwalimu. Sera yake na haya mambo ilikua kama maji na mafuta. Kwanza akiangalia kanchi bado kanajisukuma halafu leo unaleta warembo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...