Pichani juu ni mmoja wa walezi akiwa na watoto wa Makalala. Picha ya chini wa kwanza ni Rogger mgeni kutoka bongo, wa pili ni dada Malaika mwanzilishi wa kituo cha Makalala, wa tatu ni Anko Chibby mwenyewe, wa nne Ivani mdau mkubwa wa Makalala, wa tano Rafaeli mdau mkubwa wa Makalala. Siku hiyo ilikuwa ya kuwa pamoja kwa ajili ya Makalala.
Mdau Baraka Chibiriti ambaye hivi karibuni alikuwa vekesheni bongo baada ya kuchanga karata kwa sana huko ughaibuni ambako kwa sasa ndio anakoishi, kati ya mambo aliyoyafanya ni kutembelea kituo cha watoto Yatima cha Makalala huko Iringa, ikiwa ni jitihada za kuwatunza na kuwaenzi watoto ambao wamepoteza wazazi wao kwa njia moja au nyingine.Chibiriti hakuishia hapo tu bali amewafungulia globu mahususi ya watoto hawa nia ikiwa ni ku "Creat Awareness" kwa jamii popote ilipo kusaidia kwa hali au mali watoto hawa ambao wanahitaji faraja na kuishi kwa upendo kama watoto wengine.
mtembelee
http://www.makalala-chibiriti.blogspot.com/


Uncle Chibby, kaka mfano wako ni wa kuigwa na napenda nikupongeze mkuu... Pia napenda nimpongeze kaka Michuzi kwa kuwezesha watu kama sisi kufahamu movement yako through mtandao wake wa kutisha!!
ReplyDeleteJamani waTz hii ndio inaitwa mifano ya kufanya kwa vitendo ari na nia ya kuwawezesha na kwasaidia wale waliokuwa hawana bahati kama wengi wetu!
Mola azidi kuwaongezea ninyi na wote wenye nia na pia utendaji wa anga hizi.
Ramadan Kareem!!!
kaka hongera
ReplyDeleteMwanangu nimekukubali maana watu wengi wakioa wazungu hawakumbuki nyumbani kabisaaaa!!
ReplyDeleteTunahitaji watu kama nyinyi,mwingine angejifanya hataki tena uafrika ndo wanavyofanyaga wapumbavu wengine.
HONGERA SANA.
mambo ndio hayo....naona motivation ni kali...huyu akitoa mablangeti na mwingine kituo.....
ReplyDeletekweli tutafika ....tuuuuuu....na wengine msikate tamaa pole pole ndio mwendo
Mbona sasa watu hawasemi kuhusu Chibiriti?
ReplyDeletewatu kusema wenzao hata bila kuwajua
yan km hawa watoto wa MAHENGE,,Iringa ni hamu yangu sana nipate upenyo nisaidie pale ngaa watoto wachache
ReplyDeletetatizo ukikutana na awa viongozi wanasiasa kila mtu ataka ulaji kwanza kabla ujaingia kazini,,,JAMANI WANABOA WANAUDHI WAWEZA PIGA MTU
yan hawa watoto wamekua mtaji kwa wengine
hongera kaka