Mambo Michuzi,
umenibaninia mail zangu nyingi mno.
sasa napenda kuuliza wadau swali hili kuomba ushauli.
Nilikuwa ulaya muda mrefu kwa masomo & kubeba box baada ya kutoka ulaya nikaamua kuwa na urafiki wa kawaida na kufanya uchunguzi wa kina wa kama mwaka 1 nikichunguza Tabia ya wasichana kama watatu nipate mmoja wapo wakuoa.
nikapata kujua tabia na sifa zifuatazo:-
Wakwanza: Msichana analipa waswahili wanasema ila tatizo mwongo sana na ni proffessional cheater "just my friend anatumia neno hilo". lakini pembeni mambo mengine.
Wapili: Ni Msichana mtulivu lakini tatizo dogo sio msomi kihivyo ila tabia yake imetulia, ila sio mzuri kihivyo kwa sura. ila anajali hapo ndipo penyewe,
watatu: Yuko kawaida ila nikionana nae kazi kweli kweli waswahili wanasema "mizinga" naomba pesa kidogo ya chips, nguo hiyo imetoka New fashion huo wengine wanaenda na wakati.
baadaya ya uchunguzi wa tabia na kuwajulisha kati ya hao nimechagua msichana wapili tatizo likaja juu ya tatizo kwanza hamuendani, halipi kwa sura, elimu ya mh! hapana, ila naona ungemchukua yule wa kwanza anaelimu nzuri mtasaidiana kwa mambo mengi kwa sababu wewe ni msomi pili, wazazi wao wana tabia njema, usipomkubali hatuta hudhulia harusi yako kama ukimwoa huyo namba mbili ulio mchagua.
je wadau mnanisaidia ushauri gani katika hili?
Uzuri wa mwanamke ni tabia, na kumbuka ww ndio muoaji na muamuzi wa mwisho. Hivyo ndugu sioni kama kizuizi cha ww kuoa huyo wa pili. ww ndio utakaa na huyo mwanamke ktk ndoa yenu siku zote, wala sio ndugu zako. Kumbuka uzuri wa mwanamke ni kujipamba tu , hakuna mtu mbaya hapa duniani, ni ww mwenyewe ujue kujiweka vizuri.Jitahidi kumuelimisha huyo mdada ili ajiweke sop sop, nadhani atakuwa mzuri tu.
ReplyDeleteKama si msomi ni kiasi cha ww kuchukua uamuzi wa kumuhimiza kusoma.Hakuna aliozaliwa na kusoma.Mapenzi hayana utajiri wala umasikini ilimradi uwe umeridhika naye.
MH....
ReplyDeleteWaswahili wanasema DUME LA MENDE HALIHOFU KINYESI na kwatafsiri yake kwako nikwamba hustahili kuoa kwani hujakomaa kuweza kuwa na uwamuzi wako kama dume.
so keep listening to your mom and dad.
kidume
anza upya, waache wote.
ReplyDeletepumbavu sana,,,
ReplyDeleteivi kwanini mnapenda kutukana/kukashifu wanaowatoa tumboni???hamna jipya??
wee michu ndo nini izi uzushi?
km hujazaliwa na mwanamke,tukaneni tu
HUYO WA KWANZA HAFAI KABISA
ReplyDeleteWA PILI HUYO NDIYE MKE TENA KAMA WEWE NI MSOMI NDIYO VIZURI MUENDELEZE TU UTAPATA FAMILY YENYE ADABU SIO ILE YENYE TAMAA KAMA YULE WA TATU AU WA KWANZA YEYE KILA MTU ANATAKA AMJUWE KISHA AKWAMBIE JUST A FRIEND UZEENI ATAKUUWA NA PRESHA
HAYO NDIYO MAONI YANGU
Hivi kuna uhusiano au mantiki yoyote ya ushauri unaouomba na au umuhimu wa wewe kusema kwamba:"Nilikuwa ulaya muda mrefu kwa masomo & kubeba box baada ya kutoka ulaya nikaamua.....?" Ushauri wa bure kwako ni kwamba: Yeyote utakayemchagua hatakufaa kwasababu hao wasichana wote ni wa kawaida na hawana matatizo, ingawa wewe tayari umeshawaona kwamba wana matatizo, lakini ukweli ni kwamba mwenye matatizo ni wewe. Ili uwaone kwamba wasichana hao wanakufaa inabidi kwanza ujitazame wewe kama unawafaa? Unachokiangalia ni; Yupi anakufaa, lakini JE WEWE UNAWAFAA????
ReplyDeleteMsema Kweli
SIKILIZA MWIMBO HUU KWANZA
ReplyDeleteNIMEZUNGUKA TANZANIA NZIMA,UGUJA PEMBA NIMEFIKA NIMEWAONA WAREMBO WENGI WENYE KUJIPAMBA WAKAPAMBIKA
SIWEMA MAMA SIBABAIKI NA SURA NA PENDA TABIA NJEMA TABIA NJEMA NDIYO SIRAHA
WEWE PIA SIO MSOMI UNGEKUWA MSOMI UNGEPATA MCHUMBA HUKO KTK SHULE ZAKO ACHA KUBABAISHA
ReplyDeleteKWA MFANO OBAMA KASOMA NA MICHELLE KAMPATIA SHULE WASOMI HUPATAGA WACHUMBA HUKO MASOMONI HIVYO KAMA UNATAKA UBISHOO OWA HUYO WA KWANZA ILI UWE UNASAIDIWA
inabidi uchukuwe huyo mgoga virungu ili hata ukichacha atagonga virungu mkala na wanao
ReplyDeleteNdio maana Michuzi amekuwa akikubania. Bila aibu unatuambia ulikuwa eti unachunguza wasichana watatu kwa mkupuo. Uchunguzi gani huo? Ukishaoa utaacha tabia za kuchunguza? Unatuuliza sisi umuoe nani kwani atakuwa mke wetu au wa kwako?
ReplyDeleteKama umeamua kuoa au kutooa kila la heri na uamuzi utakaofikia.
Hi,
ReplyDeleteUnachotakiwa kujali kuwa, unatakiwa ufunge ndoa na mwanamke unayempenda na uliyemchagua kwa sababu zako binafsi na siyokufuata matakwa ya wazazi wako, ndugu na marafiki. Hiyo ni ndoa ya watu wawili, ukiangalia maslahi yao na kuacha ya kwako ndoa itakushinda. Utajikuta umeoa mwanamke anayependwa sana na ndugu lakini wewe ujaridhika naye. Hivyo angalia wewe binafsi unataka yupi kati ya hao then atakayesusia harusi achana naye.
Regards
Pole sana wewe kaka ila kama hauna haraka sana endelea kutafuta.Ndoa siyo elimu,ndoa siyo suraa.Ndoa ni pana mno.Vile vile wasichana wakiwa wanataka kuolewa wana tabia ya kuficha tabia.Utakayemwoa hayupo kati ya hao.Research yangu imeonyesha,yule ambaye unadhania ndiye mtaoana anakuwa siye!
ReplyDeleteNdg yangu unachesha kweli usawa huu mzazi akuchagulie mke!! kwani ni yeye anaenda kuishi na yeye? lazima uonyeshe msimamo wako kama mwanaume bwana la sivyo basi ujue hata ukishaoa bado watakuingilia kwenye baadhi ya maamuzi ndani ya nyumba yako, nikuulize pia mwanamke wa kuoa unaangalia nini?kama utangalia sura na pesa za kwao utaumia kaka, nafikiri huyu wa pili anafaa kwani umeshasema huyo wa kwanza ni bonge la cheater na watatu ni mzinga kila siku, ukichukua huyu wa tatu ujue kila siku hapo ndani hutapumua!!!
ReplyDeleteMwanamke angalia tabia bwana!!!!!
nkya
a-town
Kama hana Elimu na wewe umesoma mchukue UKAMSOMESHE kama unapenda na mnataka kuwa na future inayoeleweka,Pia mke utaishi nae wewe so chagua kutokana na jinsi inavyofeel usitegemee wengine KUKUAMULIA KUHUSU MAPENZI.
ReplyDeleteKwanza KOMA Kwa kudhalilisha dada zetu, Pili, Mapenzi hayaombewi jopo likachagua, hii sio tume ya rushwa. Hizo ni dalili za kutojiamini, na zitakucost sana maishani. Mpaka leo hujajua vigezo gani unataka mkeo awe navyo??? are you serious?? Kabla hujaacha kuwachambua dada za watu kama karanga. Jitazame mwenyewe mwanamke gani atakukubali wakati hata confidence Huna? Ushauri wangu ni kwamba. Kwenye swala zima la kuoa usisikilize la mtu, kwani yatakayotokea nyumbani kwako hakuna atakayekuokoa wala kukunyooshea. Ndio nyie mkitoka nje mnaanza kusimulia anavyofanya mkeo.. Huo ni Utoto wa kupindukia na ni ishara tosha ya kutokuwa. Sikiliza Hisia na moyo wako, Mwisho usiamue kutokana na Hisia bali tumia akili kufanya maamuzi. Mungu akusaidie umpate mwanamke atakayekufaa.
ReplyDeletetabia njema ndio hujenga nyumba, sio sura wala kipaji hakuna mtu mbaya duniani utakavyomueka ndivyo atakavyokua,bora tafuta huyo mbaya mtengeneze atakuwa mzuri kila mtu atampenda wewe angalia tabia kama unaangalia vizuri utabadili maana kila siku wanazaliwa, acha upumbavu wa kimjini. nawachia wengine wakushauri umekaa kama hukusoma bwana au hukutembea
ReplyDeleteUsuri wa mtu ni tabia, wapo wasomi wapumbavukwa maana kuwa wamefuta ujinga na wala siyo upumbavu.kwa hiyo tofautisha kuingia kwako darasani na kuelimika.kama wote walioingia madarasani wangeelimika matatizo tuliyonayo yasingekuwepo.
ReplyDeleteHivyo tafsiri ya elimu ni kujua maarifa /ujuzi ambao hukuwa nao na unapotumia ujuzi huo katika maisha ya kila siku ndo inajengeka hekima.
Kigezo kisiwe huyo kuingia darasani.Mwisho mke mwema hutoka kwa Mungu na mke msomi huchaguliwa na wewqe.
We bwana sema tu una lako jambo sijui kubaba mabox kunahusiana na nini na sual unalotaka ushauri ebu tuwe na busara bwana na hata mzee michuz ebu vitu vya kipuuuzi kama hivi usiwe unaviweka hata na pia kwa ulilazimishwa kuowa waschana walio huku ulaya wanawake ni wengi tu dunia nzima wewe inaonekana kwanza bado ni mshamba na ndo unazibukia mambo haya na kama unakiu unataka kukisema sema tu moja kwa moja sio kujizungusha pia bwana michuzi achana kbisa na watu kama hawa maaana anataka kuifanya blog hii ya jamii kuwa na majungu na mambo ya kipuuuzi yasio saidia jamii.
ReplyDeleteUZURI WA MKE NI TABIA NA ELIMU KWA PAMOJA.
ReplyDeletemdau.
DUDE,
ReplyDeleteMKE NI WAKO AU UNAOLEA WATU WENGINE MZEEE?
UKISHAJUA HILO UTAKUWA UMEPATA JIBU.
SIKU NJEMA
HAPA HAKUNA MUOAJI.
ReplyDeleteKATIKA ELIMU YAKO YOTE SIJUI YA DARASANI NA UBEBAJI BOX BADO TU HUJAJUA MKE MWEMA ANAPATIKANAJE?
PO DUNIA YA NGAPI WEWE JAMANI,
ACHAKUCHAMBUA AKINA DADA WE VIPI? WEWE NANI KAKUCHAMBUA? MKISHATOKA KUBEBA BOX BASI NDO MNAJIONA MSHAFIKA, KILA MWANAMKE ATIE AKILI? ELIMU YAKO HAIJAKUKOMBOA?
HAPO NDO UTAONA BONGO ULOIACHA ZAMANI SIO ILE, WASICHANA WAKO JUUU! KAA CHONJO UTASIKIA NINA MIMBA YAKO, TEH TEH......
MIMI SIMO.
safi sana umekutana na wanaokudanganya........maana wewe mwenyewe unacheat....kwa nini unakuwa na watatu? wewe mwenyewe ni muhuni kwa hiyo hustaili ushauri.....
ReplyDeletemke mwema mtu hupewa na BWANA Yesu.....
ReplyDeletemdau unayeomba ushauri yaani wewe ni bwege kweli kweli.ndo maana Mithupu alishakubania post zako kadhaa.
ReplyDeletewatu wanasoma hata ukubwani.kama kweli ulikuwa Ulaya basi ilikuwa uwe umeona ni jinsi gani siku hizi elimu inavyosomeka kwa urahisi.kama huwezi kwenda darasani basi online classes can be taken.
nina mashaka na elimu yako anyway,sababu kama kweli ungekuwa umeelimika ingekuwa rahisi kujua ni jinsi gani ya kutatua tatizo la huyo asiye na elimu.
tafadhali nenda shule na ukimaliza masomo rudia tena msako wako wa wachumba.you're not ready to marry.
KAKA KWANZA WEWE INABIDI UJIANGALIE TABIA PIA MAANA KAMA UMEAMUA KUWA NA WATATU NA HADI LEO HUJAAMBULIA BASI
ReplyDeleteNAWE JIREKEBISHE
UKIMWI nao kweli ukuufikiria wakati unaamua kutoka na wanawake wote hao, na ukaendelea kwa mwaka mmoja sasa nakushauri uende ukapime
uhakikishe kuwa hauna virusi vya UKIMWI ili usije ambukiza wanawake wengine kama hao hawakufai
Elimu ya majuu ulienda isomea nini as kwa akili ya maisha hauna? hata ufikirii magonjwa, wewe mwenyewe hujiamini hadi unakuja tuuliza maswali humu
Nawaomba wanaume na wanawake hii ya kuchang'anya wapenzi haisaidiii mtaenda futi sita kabla ya muda wenu.
Mwisho kama huyo hajasoma, basi anza kumpeleka shule akasome anachokipenda na mtajenga unyumba pamoja, anaweza akawa na akili kuliko hao walioenda shule na kufanikiwa pia kimaisha na atakusaidia wewe na hao ndugu wanaosema watasusia harusi yako.
follow your heart, ila usirudie mchezo wa kuchang'anya wapenzi
Watanzania wa kibongo mnaboa sana. Tabia gani mpaka leo ya kuchagua wanawake kama nyanya sokoni? Mnaboa sana. Ndio maana mapenzi yanaisha siku mbili tu baada ya kuoa. Ati nina wanawake watatu ninachagua yupi nimuoe. Roho yako haina penzi la kweli kabisa. Wewe una wanawake watatu unawatupia macho mpaka leo na utu uzima wote huo?
ReplyDeleteKwanza ni ulaya ndio inakufanya uweze kuchagua wanawake kama nyanya vile bila mapenzi? Mchezo hauendi hivyo siku hizi.
Kwanza wewe uko ready kuoa kweli au unataka kuolea watu? Unataka kuplease watu tu wewe?
Kaa chini kwanza jifunze kupenda, jiulize kwanini unataka kuoa au kama unampenzi wako then mambo mengine yatakuja polepole. na umwoe umpendaye....sio kwa ajili ya material things....
Tatizo watanzania wengi huoa na kuolewa just b'se fulani ameoa, shule keshamaliza, na watu waliolingana nae wanaolewa au anayemuoa au kuolewa naye ni so and so au ana mahela mengi. Ndio nyie mnaoa jina tu....kwa makeke ....harusi kubwa mapenzi hamna......siku mbili maukimwi na kila mtu analala kitandani kwake.....yaani bongo mapenzi ya kweli hamna kabisa bado watu wanatreat wanawake kama commodity? .watu vichwa havibadiliki ...utumwa hauishi......kila siku tunaona mail order bride tu huku na hao wanawake wakishasikia mwanaume yuko huku nje ya nchi hata hawajiulizi anatabia gani, ni mtu gani, ni mkarimu au ni mchoyo. Wakisikia tu mwanaume anatafuta mke wanakuja tu....halafu wanaanza kulalamika wakiona things are not the same as they were hoping.....na kuanza kucheat na black Americans.....I hate this....
Wewe hao wanawake hutachukua muda wakudate.... kujua kama mnaclick au mna something in common? Wewe wanawake watatu mpaka leo yaani huna girl friend? Mhhhh unaonekana kwanza mchoyo. Usije ukatesa watoto wa watu....ohhh msomi tutasaidiana....mwanamme gani weee. Mwanaume wa kweli anatafuta tabia akijua yeye ni sole provider of the familly. Kama mke akija na package akaongezea unga poa akikaa nyumbani poa. Acha uchoyo na uvivu.
Na wanawake wakibongo amkeni...anzeni kujishughulisha na kuchacharika na maisha. Sio kukaa tu kusubiri a fairy tale life hapa....kusbiri prince charm aje akubadilishe maisha yako. Ndio mwanzo wa kuonewa humo ukishaolewa na kuteseka. Try first to make something out of your life na mwanaume atakuheshimu....Gold digger is so out nowadays
Ni hayo tu
Hivi nyie kina nshomile ulimbukeni utawaisheni lini?
ReplyDeletemdau maJ
Wewe wa kwanza ni saizi yako kwani mnaendana kitabia, elimu ya darasani, na uwongo na nanihii vile!
ReplyDeleteNadhani siku hizi tunaangalia zaidi PESA katika maisha sio mapenzi tena maana kama unataka mke na ana tabia nzuri mara ohh hajasoma ya nini yote/ SISI WANAUME WA kibongo TUMEGEUKA WAPOPO?? wanawalazimisha wake zao wawe manesi ili walete pesa nyumbani, Msomeshe mkeo, kama hapendezi mrembeshe, USIONE VINAELEA.......
ReplyDeletekwanza umewazalilisha dada zetu KWA NINI UNA WANAWAKE WATATU kwa MPIGO???? Nyie ndio mnaoeneza magonjwa, Hapo ndo uelewe si lazima usome uwe na busara, mfano ni wewe mwenyewe. Dada zako wakiwekwa katika hali hiyo UTASEMAJE BWANA MSOMI, HAA????????
UNAOA MKE MWEMWA AU WAOA ELIMU?WATAKA MKE AU SURA,WAOA KWAAJILI YAKO NA MKEO KWAAJILI YA MARAFIKI ZAKO BETTER STAND ALONE THAN IN ILL COMPANY
ReplyDeletewewe jee una vimada wangapi? anagalia upande mwengine wa shilingi
ReplyDeletetatizo ni kwamba wanaume wengi siku hizi wamekua selfish sana na hawana mapenzi ya kweli. hivi wewe unachagua mwanamke kisa amesoma au mzuri? ndio maana hua mnachunwa kama majinga. hamna lolote.halafu kama nimesoma ukoo wenu ndio uje unitegemee mimi? tafadhalini sana wakina dada msijikufanya kosa kama nililofanya mimi.mwanzoni niliona ananipenda lakini nimekuja kupata kazi ananigeuza kitega uchumi.wanaume lini mtajua tofauti kati ya true love na opposite? siku hizi unakuta umekaa na mwanaume karibu miaka 3 lakini hata siku moja hajawahi kukununulia hata gauni la elfu 3. wewe ukimpatia zawadi haonekani kuapprecite. ukiumwa hakujali, hajui umekula umepata dawa, yeye anachotaka kwako ni ngono na umpikie.akina dada amkeni.kuweni waangalifu na wanaume wanaowapa misaada na kuwaonyesha kuwa wanawapenda kumbe kuna kitu wamefocus.kuweni waangalifu jamani kina dada.
ReplyDeleteRafiki yangu umechemsha. Swala kama hili hukupaswa kuomba ushauri kwenye blog, utapewa ushauri mwingi na wa ajabu mpaka utachanganyikiwa. Je huna marafiki au watu wengine wa karibu? hasa watu wazima wenye familia, hao ndo wangekupa ushauri mzuri, lakini humu utapata ushauri mwingi wa ajabu na mpaka wa wavuta bangi na mafataki, je ushauri wa nanmna hii unategemea utakuwa mzuri kweli?
ReplyDeleteBigsam
we ni pimbi kwel kwel,kwanza hao wenyewe unawaomba ushauri wamepinda na hayo maisha ya mapenzi,wewe ulipotoka bongo kabla hujaenda beba mabox inaelekea ulikua hupati madem wewe sasa ndio umewapata kwa kujitangazia ujiko nimetoka ulaya kubeba box nna dola,we mwanaume vimizinga vya madem wa kibongo vinakushtua?basi hapo usitegemee kudumu na dem km hutaki mizinga kwani hapo kila demu utamgusa mizinga lazima,na wewe unaonekana mtoto wa mama mpk mke unachaguliwa,eti mbayaa,hajasoma,cheater.we fala nini wewe,hao madem hapo bongo wote tabia hizo kawaida asa wewe kinakushtua nini?na hao wazazi kumkataa mke unaemtaka wewe ndo nini au ndo kwa sababu umetoka ulaya?ngoja upigwe vumbi hapo na hivyo vidola vikate ndo utaona km utapeleka mke kwa wazazi wakuchagulie mama wee.
ReplyDeleteKwanza kabisa niwashukuru waliyotoa maoni kwa mjamaa. Lisha ya kumsema au kumueleza ukweli natumai kashapata mwanga. Ushauri wangu. Wacha tabia ya kujisifia kwa wanawake, Umeanza vibaya Eti umetoka Ulaya na mabox na sasa unatafuta wakuoa ktk ya watatu hao. Mfanye mwanamke akupende jinsi ulivyo kwa mapenzi ya kweli. sio ya pesa wala elimu ya juu. Akubaliane na Uwezo wako naye Umkubali wa uwezo wake, Halafu mnaelimishana unaweza kumpeleka shule akazoma ili Aweze kupapanua jambo Unapo mshauri. Asije akawa wakuburuzwa na elimu yako kwa kila kitu.Sawa Mume wangu mtarajiwa. Pili kuchagua Wife Material kunaitaji mda na busara bila kupapalika. Ujue unavyomsoma mwenzio nawe anakusoma. Hakuna mtu anayetaka kuumizwa kwenye mapenzi. Mke bora anatakiwa kuwa Mvumilivu, Kwenye Mapenzi ya kweli,Mcha mungu na elimu ya kupambanua jambo sio lazima Awe na master au Degree. Kumbuka ukichemsha kuoa umechemsha maisha. Njia nzuri ya kumpata mke au Mume Mfanye rafiki kwanza kwa mda usiomugua mwaka au miaka miwili nakuendelea. Itakuwa rahisi kujua tabia yake kwani atakuwa huru kujiachia kwa kuwa hamuogopani. Ila utakapo mtamkia Unampenda tayari ataanza kukuogopa na kuficha tabia zake usimjue. Kati ya watatu namba mbili ndio anaonekana Mke kwa tabia zake swala la elimu utasomesha kama kweli unapenda maendeleo yake. Ila bado una nafasi ya kumtafuta unayempenda naye kwa vitendo utamjua kama kweli anakupenda. Epuka sana kujisifia wkt unaongea nao atakupendea mali, elimu na Pesa na sio mapenzi. kila la heri. mdau Gerald
ReplyDeleteIVI KWANINI MNATUKANA SANA mama zenu/wanawake waliowaweka tumboni miezi yooote iyo???
ReplyDeleteivi unamanisha nini kusema unafanya "reserach?" ilhali nawe apo NI ZINGA LA MUHUNI/CHEATER KIKONGWE,wanawake 3???
nataka mmojawapo akutie adabu wee ndoani,kati ya hao mana umezidi sana,,,
sipendi watu wanaowaongelea wanawake vibaya ivo!!
mnaboa sana
Wewe mhuni, kwani nani kakwambia mke unachagua kama maembe au nazi? mke mwema mtu hupewa na Bwana. We hapo tu hujaoa usha shortlist na kudownsize to 3, walikua wangapi? bado hujatest na kuwapima utafikiri unga! we si wa kuoa msanii tu.
ReplyDeleteJamamni wachangiaji mbona mnatoa hasira zenu kwa huyu mtu? kama huna jibu nyamaza. Huyo alosema mambo ya kubeba mabox yeye yamhusu nini? Maneno ya wakosaji hayo.
ReplyDeleteKuhusu jibu naona kama wachangiaji wengine, sikiliza moyo wako wala usifuate ya watu. Kwani harusi unawafanyia watu wewe na mwenzio. funga ndoa kama kanisani au kwa DC na mashahidi wako, halafu nenda kazini au nyumbani. sura na elimu vinatengenezwa lakini si tabia.
WEWE A ACHA UFALA, KAMA MDAU ALIVYOSEMA HAPO JUU, ''hustahili kuoa kwani hujakomaa kuweza kuwa na uwamuzi wako kama dume''
ReplyDeletewatu wengine bwana, wewe unajiona wewe ni nani hasa mpaka kuwachambua (ANALYSE) wenzako eti kama wanakufaa au hawakufai!!!!!! Who do you think you are??????? soma tema ushauri huu uliokuwa hapo juu:
ReplyDeleteUshauri wa bure kwako ni kwamba: YEYOTE UTAYEKAYEMCHAGUA HATAKUFAA, kwasababu hao wasichana wote ni wa kawaida na hawana matatizo, ingawa wewe tayari umeshawaona kwamba wana matatizo, lakini ukweli ni kwamba MWENYE MATATIZO NI WEWE. Ili uwaone kwamba wasichana hao wanakufaa inabidi kwanza ujitazame KAMA WEWE UNAWAFAA? Unachokiangalia ni; Yupi anakufaa, lakini JE WEWE UNAWAFAA????
on behalf ya wasichana wasomi, wasio wasomi, wazuri, wabaya, warembo, wasio warembo, cheaters, non-cheaters, liars, non-liars, what the heck..
Kwa mtu kama wewe inaonyesha una list (size ya world encyclopaedia) inayo wa-describe wanawake... Men like you have no respect for women, you think you can analyse them the way you do material possessions... get real...
1.muomba ushauri sina uhakika kama lengo lako ni kutaka uambiwe mke gani anakufaa!!!
ReplyDelete2. walioshauri kuoa kisha ukasomeshe mke pia sijawaelewa vizuri,nadhani pia sio tatizo lao ni tatizo la kimazingira,natambua kuwa sio watu wote wenyeuwezo wakujisomesha shule,lakini hili la kuowa ukasomeshe ni hapo tanzania nadhani lipo sijui kwingineko kama kunakitu kama hicho.
3.wanaosema kipato sio cha msingi ktk maisha ya sikuhizi siwaelewi pia,maana hakuna mwenye bima ya maisha,hivyo kama kweli unataka maisha mazuri pesa haikwepeki kuhitajika kuyapendezesha.hii nipamoja na kutambua kuwa kama wewe ukifa ukamuacha mkeo atawatunza na kuwasomesha watoto kwa kipato chake!sasa kama kipato chake kinategemea elimu,basi elimu ni lazima,ila ataipataje kama hana hilo mtajuwa wenyewe ila mimi sitoowa kisha nikasomeshe,mimi sio baba wa mke wangu,jukumu langu ni kusomesha watoto na sio mke,mke aje na elimu yake tayari.
BONGO AMKENI,MSIPENDE KUISHI KTK MAISHA YALIYOPITWA NA WAKATI,najuwa africa haina historia (hatujui historia yetu kabla ya kuja kwa mkoloni wa kwanza karne za 16).
3.marrige is based on love and trust!what is love,you have your own definition,some says is the pain that hurts so sweet!! what is trust,you have your on answer!!!
vikipendeza ujue vimeundwa na wazazi au vime jiunda!!mme anaendeleza tu tena kwa upendo na moyo safi.lakini kama hakuna msosi ndani hamtapika mapenzi mle!!!
akili ku kichwa))))))))))!!!!pra!!!!!!!!
eh jamani, mimi ni yule WAKWANZA, ambaye analipa lakini ni proffessional cheater, nataka tu kusema kwamba wala SIMTAKI tena huyu mwanamme anayechambua wanawake kama nyanya, kwanza kweli roho yake sio nzuri na ni mchoyo sana, elimu/akili ya darasani anayo/ipo, lakini ya maisha ni bongolala, social interaction and confidence ni zero, heshima kwa wanawake hana, huyu kazi yake ngumu kweli kweli. aha nawaachia WAPILI na WATATU kama mtayaweza maisha na huyu mwanamme, kwani itabidi mkubali kila jambo kwenye maisha yenu liwe linapitishwa kwenye analysis software! good luck!
ReplyDeleteWANAJAMII TUNAPOTEZA WAKATI WETU KUMPA USHAURI MTU AMBAYE UBONGO WAKE UMECHEZA! SWALI LENYEWE NI UZUSHI MTUPU!, MWANAMKE ANAYEMTAKA HAYUPO HAPA DUNIANI, USHAURI WA BURE NI KUWA PATA MWANAMKE UMPENDAYE HALAFU JIFUNZE KUPAMBANA NA HAYO MAPUNGUFU.
ReplyDeleteHuyu bwaba achaneni naye anawapotezea muda, huyu hatakiwi kuoa akatulie kwanza maana atawatesa watoto wa watu bure, labda baba au mama anamuambia anataka mkwe naye basi anajiona yuko tayari kuoa.
ReplyDeleteMwanaume gani unaomba umma ukuchaguli mke, mke ukimpata wala huombi ushauri bali unatoa taarifa kuwa naoa. Kwanza huna upendo bali uroho wa nini hao wanawake wanayo, elimu, pesa, sura nk. ukimpenda mtu wala huulizi hivyo vitu maana umeshaamua.
Mimi nawashauri hawa akina dada kama wanamjua huyu jamaa wamteme kabisa asije kuwapa shida maana huyu anapenda ma-celebrity wa kujionyesha nao, hawezi kutulia hata akioa.
Tunakuombea huyu pepo uliye naye akutoke kabisa usije kuwapa tabu wasichana wa watu
MY CONCLUSSION NI KWAMBA HAO WASICHANA WOTE HAWAJAFIKIA UZURI WA KUKUCHANGANYA.KAMA MSOMI U SHOULD KNOW KWAMBA 90% YA RELATIONSHIPS ZILIANZA NA UZURI NA UVUTIANO KATI YA WATU WAWILI NA MENGINE YANAFUATA BAADAYE. AS A MAN U KNOW KUNA WANAWAKE WAZURI UNASEMA AKINIKUBALI TU HUYU NDOA MOJA KWA MOJA WALA SIJALI KUCHUNGUZA MAMBO MENGI. WEWE HUJAFIKIA HAPO,ATTRACTION LEVEL YAKO KWA HAO WASICHANA BADO IKO CHINI HAIJAGUSA MSHIPA WAKO WA MOYO BADO.
ReplyDeleteUSA1