Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Amos JumbeMay 16, 2009

    Dear Wasomaji
    hicho kibali cha kuruhusu mtu kufuga simba katika maeneo ya makazi ya watu kilitolewa na nani?

    Je kulifanyika hali ya kuangalia adhari endapo huyo simba ataruka ukuta?

    Je wizara ya maliasili na utalii na wanyama pori wanampango gani

    Je huyu aliyeadhirika kwa kugongwa na bajaji aliposikia simba na kukatwa mguu atalipwa na insuarance gani?

    Kuna aliyejiuzulu kuhusu sakata hili?

    Wasomaji, msiokuwa mnafahamu hii siyo issue ya simba na yanga, ni kuwa kuna mtu alikuwa anafuga simba huko tegeta!

    Tanzani kazi ipo

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 17, 2009

    Hivi mkuu wa wilaya ya nanihii...ina maana katuni za kipanya ndo umezipiga buti? Tuambizane mwanakwetu!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 17, 2009

    sawa MK ubigwa wenu safari hii, ila Barca watawatoa.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 17, 2009

    Sisi wakazi wa tegeta tumeshagundua kuwa habari za simba katoroka Zoo ni za uzushi mtupu.
    Inaonekana huyu mzushi ana tofauti zake binafsi na wamiliki wa hiyo Zoo.
    Huyo mzushi ndiye wa kutafuta na alaaniwe kwa sababu ametoa taarifa za uongo za kutisha watu.
    Mimi jana nimetembelea pale Zoo na familia yangu hao Simba wapo, Twiga , Zebra, Nyumbu, Makobe makubwa, mamba nk
    Ni bahati tumepata Zoo sehemu ya karibu kwenda kutembea na Familia zetu kuliko mfumo dume wa akina Baba kushinda Baa.
    Nashauri hawa wazushi wa simba katoroka waende kiungwana kwa mmiliki wa Zoo wamuulize yeye alifanyaje akafanikiwa ili wapate mwanga ili nao waanzishe ili ziwepo Zoo nyingi hapa DAR kama ilivyo nchi za wenzetu.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 17, 2009

    hahaaaha kweli sasa vipi walimuona au kakimbilia Bagamoyo

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 17, 2009

    Mimi pia nilikuwa nina hamu ya kujuwa kulikoni mbona kp hatumuoni? This doesnt mean kwamba dogo wa uswazi hayuko ft, no yuko bomba mbaya. Could this be true kwamba ni issue ya terms nini maana kp naye at times ujasiriamali anauzidishaga sana. Its my opinion anyway.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 17, 2009

    Hee! uzushi mwingine hauna mana kabisa. Hivi huyu jamaa aliyeanzisha uzushi eti Simba katoroka Zoo ya Tegeta naamini lengo lilikuwa kumwaribia biashara mtanzania mwenzetu masikini. Leo nilipofika pale Zoo na mke wangu na tukakuta Simba wote 2 wapo tulishindwa kuvumilia tukacheka sana maana duh, huyu mzushi ana roho mbaya sana ana nia ya kutushawishi wakazi wa tegeta tuichukie Zoo. Atafute sababu nyingine hiyo ya uongo imefeli.

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 17, 2009

    Misupu....si vibaya ukitolea majibu suala la kutoonekana kipanya kama baadhi ya wadau walivyokuuliza. Acha kuweka pamba masikioni!

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 18, 2009

    tatizo la Mithupu huwa anaignore sana watu. Akiamua kujibu kuh Kipanya atajibu lakini anaweza akanyamaza hata watu wakianza kumtukana atawalia ngumu. Huyu ndiyo balozi wa Tegeta bwana.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 18, 2009

    Yaelekea mwenye hii zoo anajaribu kujitetea kwa njia nyingine ukweli unabaki pale pale,Hii si zoo labda niite holdling ground ya export.imezungukwa na makazi ya watu,na kibaya zaidi yaelekea hawa wanyama hawalishwi ipasavyo,ukweli haifai kuwa hapa,mimi nimkazi wa hapa Tegeta.hawa wanyama hawapo kwenye hali nzuri,huwezi kueleza habari ya uzushi wakati hali halisi inaonekana,sasa lazima tujue hata Mbagala watu walilalamika hivyo hivyo zamani jamani hii kambi ipo jirani na makazi watawala wakala jiwe,sasa subirini hapa malipuko ya magonjwa.ninavyojua mimi wanyama na ndege wana magonjwa mengi ya ajabu kama mafua nk.hapa sioni huyu jamaa antetea nini?? huwezi kulinganisha hii zoo na za ulaya kama anvyodai.wenzetu wameendelea wapo dunia ya kwanza sisi umasikini mtupu na rushwa za kupewa vibali vya kufungua zoo kwenye mazingira yaliyojaa utata hata environments zenyewe hazipo kwenye standard ni hatari kwa afya za watu.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 19, 2009

    Kweli kuna watu hamtumii akili kidogo kufikiria Annony 11.11 am 17 may.Hapa swala ni kwa nini Zoo(what ever holding export)iweke jirani na makazi ya watu. Leo unashekelea kwenda na familia kuona wanyama unasahau kesho wanaweza kutoroka au kuvunja makazi ukizingatia wanamtu wakuwa hudumia kwa liche, Siku akifanya uzembe wakamtoka wakija kwenye makazi yenu Utaendelea kucheka. Na kama ndio mfumo dume wa kukaa baa kwa mumeo huko Zoo anashinda siku nzima au anaenda kila siku. Kwanini wanyama wakali wakee Serengeti;Mikumi ,Manyara n,k sehemu yao na watu tusiende kujenga kule. Think twice wacha kusupport ujinga huu. kama nikuona wanyama unafunga safari family mnaenda sio iwe hatari kwa mwengine. Unataka tukuchangie michango isiyoyalazima kwa maafa ya kuaribiwa na simba wakati tunaweza yaepuka. Mpaka siku aje kuwa wa watu ndio unagundua hapakustaili pale kuwa zoo. Jingeni mazingira ya kuepuka hatari kabla ya kutokea. bye

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 19, 2009

    huyu jamaa mzushi ana roho mbaya na ni wivu tu ndio unaomsumbua. inaonesha ana tofauti zake binafsi na wamiliki wa Zoo. Mimi sintasahau uzushi wake uliotikisa karibu nchi nzima eti simba wametoroka zoo ya Tegeta ikabidi niwazuie wanangu wasiende shule Alhamisi na Ijumaa kumbe ni upuuzi mtupu.
    Nilipothibitisha kuwa ni uongo nimeshangaa sana na nikawaombea wenye Zoo Mungu azidi kuwapa. huyu mwenye roho mbaya aangalie sana mwenyezi Mungu atampa fundisho kwani wakazi wote wa Tegeta, boko, bunju, Salasala, mbezi nk tumepata ukweli kuwa ni habari za uongo.
    Nina uhakika bahati na mibaraka yako Mwenyezi Mungu atakunyanganya atawapa wenye Zoo kwa vile unatumia uzushi na uongo kuwapiga vita .
    Mzushi jaribu kuzusha jingine kwa hili umenasa watu wanakucheka mitaani kwani umemtangazia kwa gharama ya bure mmiliki wa Zoo biashara yake sasa kila mtu anajua kumbe Zoo iko Tegeta.The impact is positive kwa wenye Zoo!!!

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 19, 2009

    Hivi swala la Simba wametoroka Zoo limeisha vipi. Wamiliki inabidi walipwe fidia na mzushi kusema habari za uongo.
    Pili, inabidi na sisi wakazi wa Tegeta nk huyu mzushi atulipe fidia katuweka roho juu siku 3 bila amani. Hii ni aibu.
    Inabidi huyu mzushi alipe Fidia Mashule kwani masomo yalikatishwa kwa taarifa zake za uongo za kuogopesha watu.

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 20, 2009

    EH! sasa wivu wa namna hii ni uchawi. Mbona wasafirishaji wa NYOKA, ndege, mijusi na vinyonga holding grounds zao tena hazifai na ni chafu kabisa zimetapakaa Dar kote na hazina usalama kama hiyo zoo ya Tegeta?
    Tena inaonesha na wewe mzushi unafanya biashara hiyo, hivyo unampiga vita mfanya biashara mwenzako! Ungeaanza kusakama hao wenzako mnaofuga mitaani nyoka hatari Black mamba na Green mamba tugekuelewa.
    Hoja yako iko weak na bahati mbaya umeanza na uongo wa kuogopesha watu kuwa simba katoroka ZOO kumbe si kweli.
    Makelele yako hayo ya kiwivuwivu yatasababisha nyote mlazimishwe mtafute maeneo makubwa kama Zoo ya Tegeta ya kufugia hao nyoka na ndege wenu mhame,Buguruni,kinondoni
    Mwenge,vingunguti,kurasini,tandale nk ili mwache kufugia uani. tena wengine mnafugia nyumba za kupanga na ni usumbufu kwa wapangaji wenzenu lakini watu wanavumilia.
    Acha wivu na ubabaishaji ila kamwone mmiliki wa Zoo ya tegeta akupe SIRI ya mafanikio yake hadi akajenga ZOO yenye usalama.
    La sivyo utaendelea kuona wivu hadi lini maana Zoo ya Tegeta ndiyo pekee iliyo na uzio imara na usalama hivyo nina imani Serikali itaendelea kushawishika kumpa kila msaada. Wewe endelea kupiga wivu, mwenzako ataendelea kupaa na kuboresha zaidi.
    Watu wengine bwana!!!!!Uongo wako simba katoroka umemtangazia biashara bure mmiliki wa Zoo sasa kila mkazi wa DAR anajua kumbe kuna ZOO Tegeta!!!!!

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 20, 2009

    lakini kweli mbona hayo maholding Grounds ya ndege,vinyonga na nyoka yametapakaa dar nzima tena vichochoroni kwenye makazi ya msongamano ya watu zenyewe hazitaleta mafua ya ndenge ila mzushi anaisema zoo ya Tegeta tu!!

    Huyu mzushi si angeanza kupiga vita hizo holding grounds tungemwelewa kuliko kupiga vita zoo ya tegeta iliyo na uzio imara na majengo mazuri ya kufugia wanyama. ROHO MBAYA NI TATIZO KWA MAENDELEO !!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...