Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii,wanawake na Watoto Lucy Nkya akimnadi Mgombea wa CCM Lolesia Bukwimba katika moja ya kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Busanda wilayani Geita. Picha na mdau David Azaria.
---------------------------------------------------------------------
Ombi: Globu ya Jamii inakuomba mdau 
David Azaria na wadau wengine watuletee picha 
za kampeni za wagombea vyama vingine.
Ahsante ya mapema kwa Ushirikiano
-Michuzi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 11, 2009

    Ah Michuzi Umeiyona iyo eh,kumbe bado uhitaji mawani. te eh te

    ReplyDelete
  2. MagazetiMay 12, 2009

    Mkuu, Geita ni jimbo ambalo linaitaji zahanati, shule, and miundo mbinu. Mimi kwa sasa ninaona watu wageita wachague mwamama katika jimbo hili.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 12, 2009

    JIMBO LILIKUWA CHINI YA CCM NA HAYO YANAYOAHIDIWA LEO NA CCM HAIKUYAFANYA SIKU ZA NYUMA SASA AHADI HIZI ZA SASA NI ZA NINI, AU CCM HAUKUONA HAYO MAHITAJI INAYOAHIDI SASA? KWELI SIASA NI UONGO NA UTHIBITISHO MUANGALE TAMBWE ALIYEVAA NGUO ZA KIJANI NA TAMBWE ALIYEVAA NGUO ZA BULUU, NI YULEYULE ISIPOKUWA ANABADILIKA KAMA KINYONGA KUTEGEMEA MASLAHI, DU! Eee BWANA Eeeeee! nyie akina mama mkizomewa msisingizie mlipoteza na cheni za dhahabu, simu na pesa, bali mvumilie tu kwani kuzomewa kwenye siasa ni jambo la kawaida.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 12, 2009

    Lolensia Masele haitaji utambulisho zaidi. Ni mgombea wa CCM katika uchaguzi utakaofanyika mwishoni mwa mwezi huu huko Busanda. Moyo wake wa kujitoa kwa ajili ya maendeleo hauna shaka. Uadilifu wake, ucha mungu na utu wake unampa nafasi za juu kabisa kuweza kuchaguliwa kuwatumikia watu wa Busanda. Hivyo wana busanda naomba msishindwe na upepo uvumao. Aangalieni kwa makini nayi mtaona ya kuwa katika binti yenu mnayo hazina ambayo itakuwa msaada wakati wa shida. Mungu awabariki na kuwatangulia mnapofanya uamuzi na uchaguzi siku ile ya siku. Siku ya kupiga kura utakuwa peke yako. Uwapo chumba cha uchaguzi tafakari kwa mara ya mwisho tena kati ya wagombea je ni nani utakayependa awasilishe mahitaji na mipango ya kimaendeleo katika jimbo lako. Mimi ningemchagua Lolesia J.M. Bukwimba pasipo kupepesa macho.
    NI MIMI JP

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 12, 2009

    wewe JP(JITU PUMBAVU)we unamchaguaje hapa wakati haupo busanda.we kaa Mwanza mjini ule raha wenzako huko Busanda hata magari hayapiti.
    mvua ikinyesha ni kero madini wagawia shemeji zako wazungu we uko huko kwa kuwa dada ako kawekwa kimada na kaburu we unashangilia ili ufisadi uchukuwe nafasi yake ki sawa sawa ila jina lako ni kielelezo Tosha,.
    HII NI BLOGU YA WENYE AKILI TOA UJINGA WAKO HUMU.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 12, 2009

    yani jp (jitu pumbavu) umefungua blog ya jamii kuinadi ccm na mgombea wake, busanda unapajua wewe, mvua hizi zinazo endelea tu hatupiti, kwa sasa busanda tunataka mtu mchapa kazi kwa vitendo na muwajibikaji na c kiongozi kalamu

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 12, 2009

    weweeeee huyu dada mwenyewe kajichokea maskini si bora apewe mtajia akafanye kazi yake ya amama lishe?.
    acheni kumdanganya dada wa watu,najua wazee wanata ka tu kumvunjia ndoa maaana akienda bungeni ni ngono tu kwa haya mabunge ya C C M

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 12, 2009

    Tangu Tanzania ipate uhuru,Geita haijawahi kutoa waziri hata naibu waziri.Ni wiraya yenye utajiri sana ila haina msemaji serikalini.Kwa uchaguzi huu mdogo wa Busanda,Busara itumike.Kikwete najua utaisoma hii komenti wakumbuke watu wa Geita.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 12, 2009

    wananchi mimi nafikiri wakati umefika wa kuwapa wapinzani nguvu.
    CCM tangu ishike awamu ya 4 ukweli ni ufisadi, majambazi na shida chungu mbovu ndio tulizopata.

    miaka yote 40+ nini CCM wamefanya zaidi ya kuidudumiza nchi na wachache kunufaika.

    mahakama itafanya nini wakati jaji anachaguliwa na raisi.

    jaji mkuu wa polisi achaguliwe na wananchi hapo utaona kazi.

    mahakama na vyombo vyote vya sheria viko chini ya serikali.

    njia ya kuinyima nguvu serikali ni kuwanyima kura zetu na kuwapa wapinzani ili waweze kuwa na sauti.
    tanzania oyee mafanikio ni sisi wananchi wenyewe ama serikali ya 4 ni mlo na kujitajirisha wenyewe na watoto wao ambao wako nje.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 13, 2009

    annon wa 1058 hapojuu safi sana kweli hilo jamaa ni JP kweli asante sana kama vile uko kichwani kwangu

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 13, 2009

    wizara ya huyu mama ni Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, si Maendeleo ya Jamii, Wanawake na Watoto, tunapotosha wasomaji wageni michuzi uwe makini

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...