WADAU KUNRADHI,
KULE MTAA WA PILI (JAMII FORUM) KUNA MADA AMBAYO IMERUSHWA KWA MDAU ANAYEDAI KUUMIZWA SANA NA VEKESHENI ZA NANIHII, NA KUMSHAMBULIA SANA SANA. WADAU NAOMBA MCHANGIE HOJA HIYO BAADA YA KUISOMA KWENYE LINKI HIYO HAPO CHINI.
KWA UPANDE WANGU MSIKONDE WALA NINI. LIBENEKE LA VEKESHENI LITAENDELEA KAMA KAWA. MIE NARUDI MWEZI UJAO. HIVI SASA NAELEKEA UJERUMANI KISHA NTAENDA AUSTRALIA NA KUMALIZIA JAPAN.
-MICHUZI
Kaka michuzi pole na Starehe hivi mtikila akishika Nchi utaendelea kuwa na vekesheni zako? hehehehe MUNGU IBARIKI TANZANIA
ReplyDeleteRoho zawaumaaaaaa! wabongo bana, kwa roho za korosho hawajambo. Nanihii eeh, kula bata mtu wangu, endelea kukamua na zidi kutuletea matukio ya vekesheni kama kawa.Wenye roho za kwanini wataendelea kuchomwa na jua!
ReplyDeletewashamba wapo wengi achana nao
ReplyDeleteme naona ungefafanua kwaza madai na hoja zilizotolewa kama unatumia gharama zako kwa shughuli zako binafsi au za walipakodi kwa shughuli zako binafsi au zote kwa pamoja na pia ungejibu ni namna gani unavyo pangilia muda wako katika kufanya shughuli za serikali na zako binafsi pasipo kuathiri makubaliano yako na mwajiri wako.
ReplyDeleteKILA LA KHERI MKUU NA VEKESHENI
Nadhani majibu aliyoyapata yanaweza kuwa yanamtosha. Kaza buti ndugu yetu endeleza libeneke.
ReplyDeleteNdiyo ile-ile aina ya watu wanaosema sheria ya Dual Citizenship ikipitishwa "watu watafaidi huku na huku." Kani nani amekatazwa kujakuishi nje? Wakitaka na wao wachague nchi waende wakaishi.
Nguvu nyingi wanazitumia kuhakikisha "kizuri hakionekani kwa jirani", kwa sababu jirani hastahili. Wakipata wao wanaona wana-deserve.
Sijui tuite WIVU au MTIMANYONGO. Nguvu hii kama wanayo kwanini wasimsaidie JK na kuielekeza kwa mafisadi wa kweli, ambao bado wamepachika mirija/ mabomba kwenye nchi yetu na wanaendelea kufyonza.
Huyu mlalamikaji nadhani ana-matatizo binafsi ambayo bahati mbaya mpaka anaandika hiyo hoja alikuwa hajayagundua.
Mdau,
London.
Usijali Michuzi, Jamii forums watamuelewesha na ataewlewa, kama ni muelewa. Tatizo langu, kwanini umealika wadau wa hapa waende kukutetea huko?
ReplyDeleteDear Michuzi,
ReplyDeleteHongera na mafanikio na pia pole kwa kuwa target ya watu wenye "vijiba vya roho". Nakupa hongera kwa sababu kwa kutumia blog hii umeweza kusaidia watanzania wengi sana, lakini these mindless..non nonsensical people kwa sababu ya upeo wao mdogo wanashindwa kuliona hili. Hawa waungwana hawataki kukubali kuwa vidole siku zote havilingani.
So long as you stay humble ...mimi sina shida mkuu..endelea kutumbua raha acha "wachawi" wapige ramli. Hii ndio ile mijitu unapofanya vizuri badala ya kukupa "good job" inakuendea kwa waganga. Roho mbaya kabisa. Tell them hukuanza leo...hapo ulipo ulikuchukua muda kufika and the kind of struggles you went through labda wanaweza kuelewa. Tafadhali usipoteze muda wako kufikiria these IDIOTS.
Safari njema Japan.
--Phatlorenzo, Minnesota-
Kaza buti mzee achana na wenye wivu.
ReplyDeletemdau Trondheim
KUNDI LOTE LIKO VEKESHENI LIKIONGOZWA NA MARCOPOLLO, HATA HIVYO BADO HAWAJAMALIZA KUVUMBUA NCHI NA WANASEMA WATAELEKEA MASHARIKI YA MBALI.
ReplyDeleteMichuzi, ngoja twende kule tukakuunge mkono. Binafsi naelewa kuwa vekesheni ni lugha unayotumia kutupasha habari za sehemu mbali mbali. Ni sawa kusema na abiria wa basi wanaposimama na dereva akasema wakatufute dawa au kuchimba mzizi. nadhani walio wengi tunnafurahia kupata mbalimbali kwa kuwa unafika sehemeu mbali mbali duniani na inakuwa sio manneo tu ilapicha ambazo wenzetu wa huku wanasema (a picture speaks thousands words).
ReplyDeleteLa zaidi sana ni jinsi wewe unavyoweza kuhimili mails nyingi ambazo zingine zinakuwa ni za kukudhiaki lakini unaendelea tu na kazi/libeneke lako. Poa kabisa. Mdau Reading
Anko Michu, upo juu juu saana. Yaani nakupa high HIGH five, wewe ni bonge la selebriti wa kibongo. Hata waseme vipi, karibu saaaaana Australia. Zamu yetu na sisi mikonozzzzzzz.
ReplyDeleteMichuzi, mdau wa Reading tena..Sina haja ya kuchangia kwani mdau mwingine kaweka bayana kile nilitaka kuseam
ReplyDeleteNam-quote:
"Sasa mnataka kuchemka, kama mmekosa thread za kuanzisha bora mtafute wimbo mmoja hapa tuujadili.
Hiyo lugha ya vekesheni ni humour anayoitumia michuzi kama msanii katika fani ya ku-blog. Kama unashangaa kutumia vekesheni mbona huulizi kwanini anajiita ''nanihii'', au unadhani 'h'ana jina?
"
Michuzi naona hawa jamaa wa jamvini sasa wanakuonea wivu, nani kawakataza kujifunza uandishi wa habari labda kingeke kingewaangukia wao kuwa kwenye misafara ya wakubwa ili watoe tongotongo. Mjomba lakini viwanja unavitembelea naona bado vekesheni za space tu.Usikonde tanua kwa raha zako nasi tunakufagilia mhabarishaji wetu tulio mbali na nyumbani.
ReplyDeleteMheshimiwa mkuu wa wilaya, umeomba tuchangia hoja hii hapa kwenye blog yako au kule jamii forums.
ReplyDeleteKama ni kule jamiiforums, unaweza kunipa maelezo jinsi ya kuchangia kule na ni mchango gani hasa unataka niutoe?
Kama ni hapa kwenye blog yako, utabandika maoni ya aina yeyote au kuna mengine utakayoyabania (hata kama sio matusi).
Asante.
Balozi wa naniii, mie sidhani ni shida na wala ikusumbue. Maana nadhani wewe ni miongoni mwa watu unaopenda uhuru wa maoni, as mie naona aliyetoa hoja hiyo kwenye JF anataka kujua kama uko kwenye msafara wa raisi au la!! Sasa,kama waona kawazo kangu kanakugusa, wewe respond kuwa uko vakasheni na haukwenda na msafara, vinginevyo pia uhuru ni wako.
ReplyDeleteBro Michuzi!!Achana na hawa watu wenye wivu!! kama unalipiwa na Serikali , wananchi!!!? wao tatizo lao nini? unafanya kazi iliyokupeleka na pia unafanya mambo yako.. sioni kuna tatizo gani! hao ni watu wako wa karibu wenye wivu na wewe..Waambie na wao watafute kazi zitakazo wapa Vekesheni...au wasage chupa wanywe..Mdau Midland uk
ReplyDeleteSamahani mkuu wa wilaya ya nanihii,haihusiani na mada iliyopo hapa juu.
ReplyDeleteNamtafuta rafiki yangu wa miaka mingi anaitwa ELISHA NGONDO tulisoma chuo kimoja IFM.
kama anasoma ujumbe huu naomba aniandikie rdor7819@hotmail.com
Asante sana.
Haters Tu hao michuzi! we kamua kama kawa na Vekesheni kula Tu!
ReplyDeleteJust for fun in ze majunguz!
ReplyDeleteMichuzi ni msanii wa bongo flavor na ana promota mzuri kuliko wa Ali Kiba ndio maana ana safiri sana
Hongera Michuzi na tunasubiri Album mpya
Life kila mtu na zali lake wanga
Peta bro
JF ni miongoni mwa mitandao niliyokuwa naipa credit lkn kwa hili nadhani wamechemsha. Mithupu ndio yupo kwenye msafara lkn asitumie fursa hiyo kuwasabahi ndugu na jamaa, ina maana mithupu amekuwa mlinzi wa rais kiasi kwamba kushow luv na wadau imekuwa nongwa? JF zungumzieni mambo ya msingi acheni udaku wa GP, Mara ngapi JK anaenda kwa shughuli za kitaifa na tunaona anashow luv na ndugu na jamaa, anatumia kodi ya nani? ina maana JK akienda Bagamoyo kuwapa Hi ndugu zake asitumie msafara wa rais? JF kimeo, mnatamani muwe Michuzi, mnatamani maisha yake, mnatamani muwe DUNIA na Michuzi awe ndani yenu lkn msiache kuongea ongeeni mnavyoweza sie tupo tutawasikiliza tu.
ReplyDeleteKatika dunia ya sasa, watu hawataacha kuongea. Si kila mtu anapenda mafanikio ya watu wengine. Cha msingi ni kutojali yasemwayo na kusonga mbele.
ReplyDeleteKeep it up the good work.
Mdau
Sawasawa Unaringa Sana Na Hela Za JK Muandishi Gani Aaandika Uongo
ReplyDeletepapa na nyangumi wameharibu watu!
ReplyDeletemithupu achana nao kama ulikuwa hujui hao ndio wabongo bwana!washaona unakula kwa ubua mbona ulipokuwa bongo walikuwa hawasemi hivyo?wanakufuatilia hadi chooni jamani tuache majungu michuzi hajaharibu kitu anatusaidia sana kutupa nyepesi za bongo pamoja na nje ya nchi hv kwanini hatupendani jamani????wewe hujui huyu michuzi anafanya muda gani kazi za blog na muda gani kazi za serikali ila bosi wake ndiye anayejua na kumsimamia kama bosi wake kayakubali yote anayofanya michuzi wewe kinakuuma nini mpaka uanzishe hoja na kumpaka mithupu wetu???mithupu nyamaza usiogope wazalendo tupo na tutakulinda milele kwa hoja nzito hata kama jamaa akakuchomea utambi ukafukuzwa kazi wafadhili tupo na tuna nguvu zaidi ya serikali utakula kulala na kuanzisha blog nyingine kwa nguvu yetu sisi!!!kuna watu kama kina mjengwa,msangi na wengineo wengi tu ni wafanyakazi wa serikali na wanafanya kazi za blog binafsi mbona hao hajawaona?hizi ni hila mithupu mie nakupa 5 tena udumu na nawashukuru sana mabosi wako kwa kuwa wanakujali sana ndio maana wakakupa na hiyo nafasi ya vakesheni USA!!ungekuwa sio mchapa kazi usingepata nafasi hiyo pia hawa wenye wivu wafahamu kuwa muda wa kazi serikalini mwisho ni saa 11 jioni!!!michuzi chapa kazi wenye wivu wajinyonge!!!waambie nao wazitangaze blog zao kama wewe unavyojitahidi sio kukuanzishia majungumajungu tuuuu baada ya kuona neema inakuangukia!!!bro michu endelea tu kutuhabarisha upepo uko kwako na ukiwaogopa hao ujue unajipotezea bahati ujue mara nyingi penye mazuri huwa hapakosi majungu wewe huoni hata mheshimiwa wetu kikwete anajitahidi sana mpaka kina Obama wanamsifia ila kwa bongo walivyo na wivu eti wanasema hajafanya kitu na kutengeneza majungu mithupu funga maskio chapa kazi!!!neema ipo kwako na kama hutojenga mwaka huu jua bahati hairudii mara mbili hongera sana mie nafurahia sana maendeleo yako na nashukuru sana unatupa mambo mengi sana hasa kwa tulio mbali na tz!
ReplyDeletenamingwea!
Balozi Usikonde, ni kawaida ya Watanzania wengi kupiga domo. Sisi tujajua upo kikazi na msafara wa Raisi. Tuliokaa nje tunajua kuwa una muda wako binafsi na unautumia unavyopenda. Kama hawapendi bora wajinyonge tu.
ReplyDeleteMdau, Tokyo. Japan
VIVA Nanihiiiiiiiii wa nanihiii
ReplyDeleteHao wameanza kublog juzi, hata lugha zetu hawazijui, vekesheni, ze fulanaz, mikonoz, wamekosa la kujadili. Endeleza mikonozi Nanihii wa Nanihiii bwana.
usikonde bro michuzi, tunajua kama wewe si fisadi endeleza libeneke kama kawaida, lakini pia uwe unatoa picha za viongozi wa upinzani.
ReplyDeleteNinashangazwa binafsi na watu wanaoanzisha mada hii,
ReplyDeletekwa kifupi...wewe uko kwenye msafara wa rais,na wewe Michuzi ni mpiga picha wa gazeti la serikali.Kiongozi wa nchi anpokuwepo nje nawe inabidi uwepo,au waandishi wa magazeti ya serikali inabidi wawepo,hii haimaanishi kwamba masaa 24,inabidi uwe na kiongozi,...katika square time yako,unaweza hata ukaenda mjini kutembea na kufanya vtu vingine,kutembelea ndugu zako na ha marafiki zako.
sababu wewe ni mwanajamii,na unapenda kutupa habari motomoto,unatuelimisha sana,pale unapofanya mahojiano na watu mbalimbali...
Michuzi,usiumizwe kichwa,na wanaojadili wasichofahamu.
Je ni nani amekwambia ni kosa,hata kama mimi ni waziri wa mambo ya nje,ninapoenda kenya,nisimtembelee rafiki yangu aliyepo mtaa wa pili.
We tena unaangaika,kutafuta watu na kupiga picha,badala ya kukaa hotelini na kula na kunywa.
Endeleza libeneke,na ninakurabisha pia hapa Ujerumani,karibu Mannheim,na sasa jua linawaka ni safi sana.
Mdau wa Mannheim,Ujerumani
Mheshimiwa nanihi wa nanihi, mie naona huyo jamaa alieanzisha huo mjadala either ana wivu ama hatambui utani uliopo kwenye neno vekesheni! Naona haina hata haja kujadili hili suala wewe endeleza libeneke kama kawa. Kwa maneno mengine - upo juu! Haisumbui kabisa!
ReplyDeleteTatizo bwana Michuzi sio kupigwa vita. sijaisoma hiyo habari lakini hata mimi kilichonisikitisha kutuonyesha raha za marekani wakati kuna watanzania wanatundikiwa dripu juu ya miti huko Geita, kuna shule huko Mikese ina miaka 7 sasa ina walimu watatu na darasa moja tuu. Tuleteee habari za nyumbani zaidi. Ulaya ulaya hakuna jipya. Au na ww mekuwa fisadi kaka. Mdau Ireland.
ReplyDeleteHata mimi nimejiuliza swali kama hilo!!maana naona michuzi picha zote ni kujirusha tuu!!nimejiuliza mbona akiwa kariakoo hapigi picha au akiwa kwenye msafara wa raisi nchini hapigi picha zake na kuziweka kwenye blog!!mie naona michuzi ni fisadi na anatumia hela za walala hoi kwa kujinufaisha mwenyewe..mie sijaona kaweka picha yeyete ya maana kwenye ziara ya raisi yeye anapiga picha tuu kwenye matanuzi yake...ISA MICHUZI FISADI.MDAU
ReplyDeleteHEHEEE NIMECHEKA BAADA YA KUSOMA COMENTS ZA WATU SASA NDUGU YANGU WEEE MKUU WA NANIIII ITABIDI UTUMIE LUNGHA FASAHA SLENG ZINAWAZINGUA WATU UNAJUA WATU WANAKAA NJE HAWAJUI LUNGHA ZA MISIMU POE NDUGU YANGU WAELEWESHE MAANA DUU UMESHAMBULIWA WANGU MBONA DENMARK SIJAKUSIKIA MAANA JK ALITINGA HUKU DK HUKUPENDI?? KARIBU SANA MIMI NI MSOMAJI MZURI WA GLOB YAKO
ReplyDeleteNDUGU YANGU MKUU WA NANIHII KATIKA KITENGO CHA NANIHII,UNAWEZA KUONA MWENYEWE WALA VUMBI WALIVYO NA ROHO ZA KOROSHO,HATA SISI WA UGHAIBUNI TUNAPIGWA VITA HIVYO HIVYO NA WALA VUMBI WA BONGO,WAKIKUONA UMEKULA PIPA TU ROHO ZITAANZA KUWAUMA ILE MBAYA NDIO MAANA SISI WALA KUKU TUKITIMBA KWA WALA VUMBI TUNAKULA STAREHE ZETU WENYEWE TUKIMALIZA TUNAKULA PIPA ILE MBAYA,NA HATURUDI NG'OO HATA WEWE MICHUZI KAMA WANAKUZINGUA KIMBILIA UGHAIBUNI SI UNAONA HATA MKWERE MWENYEWE AMESEMA KAMA UNATAKA KUKAA MAMTONI RUKSA,MWANANGU NANIHII ENDELEZA LIBENEKE KWA KWENDA MBELE ACHANA NA WAJINGA NDIO ZAO KUWA NA WIVU.UKIONA HIVYO UJUE SUCCESS IMEKARIBIA AU UMESHAIPATA SO LAZIMA WANYANYUKE KUKUPINGA.MIMI NAONA WAJINGA TU HAO WOTE,WATULIE HUKO HUKO KWENYE VUMBI WALE UGALI NA MAHARAGE WATULIE.MWANANGU TENA KAMA UNAWEZA USIISHIE JAPAN TU KAMA UNAWEZA KUMSHAWISHI MKWERE MWAMBIE MKAMALIZIE VAKESHENI VISIWA VYA BAHAMAS ILI WASEME SANA.NA SISI WA UGHAIBUNI HATURUDI NG'OO JK MWENYEWE KASEMA RUKSA.KWA LEO INATOSHA NAKUTAKIA VAKESHENI NJEMA KAMA UTAWEZA KUPITA NA HAPA KWA MALKIA BASI TUTAONANA.
ReplyDeleteNawashangaa sana jamaa nilidhani jamii forums kuna discussion za maana sasa kazi ya misupu si inahusu kusafiri?sasa mwandishi gani wa habari anakaa ndani ya ofisi tutapataje picha?
ReplyDeleteMheshimiwa Mkuu wa nanihii na balozi wetu...
ReplyDeleteMimi nakupa pongezi sana kwa kuwa unashirikiana na sisi wote unapokuwa kwenye hizi vakesheni zako! Ungekuwa fisadi ungetuficha kwamba uko wapi na unafanya nini. Huyo anayekusakama ni WIVU tu unamuuma! Hicho ndiyo kilichotuondoa BONGO Mheshimiwa. Maana ukifanikiwa tu wengine wanakuendea kwa waganga ha ha haaa!
Umenifurahisha kweli baada ya kumpasulia ukweli kwamba NA BADO una safari za kutembelea nchi lukuki kabla hujarudi bongo. Ale wembe huyo!
Huyu jamaa inabidi ajue kwamba wewe siyo shushushu kama oblangata yake inavyomshauri ingawa hajasema, Pli wewe ni mpiga picha wa gazeti la serikali kitu ambacho yeye hajui therefore popote serikali inapoelekea hasa hii ya mheshimiwa Kikwete lazima uwepo(What a job!!!).Uzuri wako ni kwamba za serikalini unapeleka serikalini na za wadau unaturushia wadau, sasa huyu jamaa HAELEWI NINI?but but but but kama ameuliza kwa nia ya uzalendo ni vizuri na kwa kweli ni hoja ambayo ni ya kimaendeleo otherwise atakuwa anawivu na wala usishangae mtu akama huyu akiwa Mchawi,Mkuu wa wilaya ya nanihiii unajua waganga wanapopatikana hivyo tumia hizo pesa utakazosevu baadas ya vekesheni na ukidharau hiyo ndiyo itakuwa vekesheni yako ya mwisho.
ReplyDeleteMdau ajue neno vekesheni halijamaanisha kuzurura, angeona kwanza lilivyoandikwa na jinsi sentesi zake zilivyo. Lakini hata kama upo kikazi kama mfotoa masnep, kwani unacholeta kwenye globu ya jamii sio masnepu? kama ni masnepu na wabongo tunayafurahia naamini kodi yangu umeitumia vizuri
ReplyDeleteKuna Jamaa mmoja amechangia point kule JF amenichekesha sana,eti kila mbongo aliye nje, anajichukulia kuwa yuko vekeshen, hata mabalozi pia wapo vekeshen!!!!
ReplyDeleteTe he!
Huo ni wivu tu, wabongo ndivyo tulivyo.Ufisadi ni safari za michuzi tu ? mbona kuna mengi tunayafumbia macho?
ReplyDeleteNimesoma, is is a fair criticism, when it comes to tax payer money. Kwa nini unaita vacation ( your at work). I used to ask myself why you call vacation?. Your at work and not vacation( its an insult to taxpayer money). Kitu wanachosema ni cha ukweli na you deserve to be told. Wewe uko kwenye msafara wa raisi kwa nini unaita vacation??? It is arrogant and ignorant about taxpayer money. I dont mean to hurt your feelings . You are really doing a good job to inform us but the word "Vacation"needs to be bunned. Thank you sir,
ReplyDeleteNimesoma, is is a fair criticism, when it comes to tax payer money. Kwa nini unaita vacation ( your at work). I used to ask myself why you call vacation?. Your at work and not vacation( its an insult to taxpayer money). Kitu wanachosema ni cha ukweli na you deserve to be told. Wewe uko kwenye msafara wa raisi kwa nini unaita vacation??? It is arrogant and ignorant about taxpayer money. I dont mean to hurt your feelings . You are really doing a good job to inform us but the word "Vacation"needs to be bunned. Thank you sir,
ReplyDeleteKama Michuzi,
ReplyDeleteHawa ni waosha vinywa tu, achana nao. Usishangae wabongo wengi wapo hivi, roho za korosho na kujiuliza masuali mengi tena mambo haya wahusu.
Sasa wewe kusafiri inawakera, usiposafiri ukae bongo peke yake watakusema kama wanavyosema fulana yako. Wabongo sumu.
Tena mbaya zaidi wanavyopenda kupima uwezo wa wengine. Ukinua shati fulani wataenda kuangalia linauzwaje, ili wahesabu pesa zako. Kama hivi wanahesabu nauli na kujumlisha. Sishangai JK alivyo wapasha wajizatiti na kuendeleza familia zao.
Binafsi nafurahi sana unavyo safiri na kujichanganya na wabongo kila unapoenda na unatuletea habari motomoto kila unapokwenda.
Alafu hawa waosha vinywa hawakujui, kwani umeanza kusafiri leo? Miaka yote/siku za nyuma ulikuwa unasafiri sasa hivi wana bahati kuwa unaendesha blog ya jamii kwahiyo wanaelewa upo wapi kwa picha na maelezo unayotuma.
Endeleza libeneke Kaka watasema watachoka.
knockyourself@hotmail.com
Achana nao. Hawana cha kufanya. Habari wanataka kuzisoma. Halafu wanataka kujua unafanya nini.Waswahili bwana!
ReplyDeleteTanua tu papaa
hanha Barozi wetu, usijali wala nini?Naona ni wale watu waupande wapili wasio takia mema wengine? Kama anataka kupiga vita na MAFISADI kaja upande mbaya,wewe michuzi ni mtu watu hata sijui nani atamsaidia katika hiyo vita?
ReplyDeleteANATIKISA KIBERITI TU.
zidumu vekesheni za kaka Michuzi..!!
huo ni wivu usio na akili, kwa mfano mzuri natoa wewe umetumwa kikazi Tanga na huko Tanga una ndugu na marafiki, na umelipiwa Gharama na kampuni, je ukifika huko tanga usitembelee ndugu na marafiki huko Tanga? eti utafuja hela za kampuni?
ReplyDeletena Je Michuzi amenda huko USA na amefika huko asitembee kwa uhuru wake kutembelea ndugu na marafiki kama muda unamruhusu huo ni wivu usio na kichwa wala miguu, ingekuwa ni mimi ningepiga picha zaidi kuonyesha mfano hapa nilipokuwa natoka hotelini nilikutana na mdau akanikalibisha kwao n.k. tuache wivu angekuwa kaiba sawa.
tatizo baadhi ya watanzania ni wavivu kufikiri.michuzi ni msanii hivyo inabidi uende nae kwa makini katika matumizi yake ya lugha.usipende kutafsiri ki-sisisi.kitu kingine nani asiye jua kuwa muhidini ni mwandishi wa habari wa longi wa magazeti ya serikali.na kuna ubaya gani akifuatana na jk ku-kava stories na kuututumia vizuri muda ambao hayupo mzigoni kuwasiliana na wadau popote anapowaotea?acha wivu na tuachie michuzi wetu aendelee kutupa raha.
ReplyDeleteMheshimiwa Mkuu wa nanihii na balozi wetu...
ReplyDeleteMimi nakupa pongezi sana kwa kuwa unashirikiana na sisi wote unapokuwa kwenye hizi vakesheni zako! Ungekuwa fisadi ungetuficha kwamba uko wapi na unafanya nini. Huyo anayekusakama ni WIVU tu unamuuma! Hicho ndiyo kilichotuondoa BONGO Mheshimiwa. Maana ukifanikiwa tu wengine wanakuendea kwa waganga ha ha haaa!
Umenifurahisha kweli baada ya kumpasulia ukweli kwamba NA BADO una safari za kutembelea nchi lukuki kabla hujarudi bongo. Ale wembe huyo!
LIBENEKE LA VEKESHENE-LIENDELEZWEEE
ReplyDeleteNimepitia link hiyo ya Jamii na kusoma mdau alivyotoa maoni yake ya kutaka uwazi wa vekeshani za Mdau Michuzi kama anajilipia mwenyewe au yupo ktk msafara wa Kikwete nk.
Nadhani inajulikana kabisa kuwa Michuzi ni mdau wa blog ya jamii na pia anafanya kazi kama mwandishi wa habari.Kuwepo kwa msafara wa rais anakwenda kuripoti yale yanayotokea huko.Na ifahamike kuwa Michuzi sio bodyguard wa rais kuwa ni lazima awepo kila anapokuwepo Kikwete.Kuna mwandishi wa habari wa Ikulu ifahamike hivyo.Hivyo kuna picha za matukio ambayo Michuzi ndio anatakiwa kuzitoa mfano yale maelezo na vid clip ya Uraia wa nchi mbili nk.Pia Michuzi kupiga vekesheni inasaidia wadau kujua wanafanya nini na maendeleo yao huko yakoje, wakati mwandishi wa habari wa rais yeye hawezi kwenda kujimix na wadau kila kona.
Mi naona Michuzi piga vekesheni leta mambo ya libeneke huko.
MAKULILO, Jr.
www.makulilo.blogspot.com
Hahahaha pilipili inawashaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa JF huna sera shosisto....... Michuzi kapanda DEGE, PIPA AU KLM haluuuuuuuuuu,,, naona hupati usingizi, hunywi maji yakashuka. Michuzi naomba jinsi ya kuingia JF nipost rasmi maoni yangu maana....mie kwetu.... naomba niuzie kesi....
ReplyDeletewatanikoma JF niliwasubiri muda sasa ni muafaka
ReplyDeleteNaomba kuuliza kwani Busanda matokeo ni aje??? Mbona JF yupo kimya sasa kaamia kwa Michuzi????
ReplyDeleteMichuzi uliza home Busanda vipi???
ReplyDeleteMimi huwa nafurahi kupata habari motomoto ambazo sio rahisi kupewa nafasi ktk vyombo 'rasmi' kama vituo vya redio, magazeti ya serikali au magazeti ya 'wenye nchi',na vituo vya televisheni.
ReplyDeleteGulobu hii ya jamii ni kupashana habari motomoto(haraka), sio kusubiri mpaka baada ya wiki mbili ndio tupewe habari zilizo haririwa kwa sana na 'wahariri wakuu'.
Pia kwa habari hizi tunazidi kufunguka macho kuhusu yanayo endelea ndani ya Tz na nje ya Tz.
Mfano habari ya Da'Rukia Porter Malipula imetuelezea kuwa yawezekana kufanya biashara nje ya Tz na sio wageni tu kufanya biashara kwetu Tanzania.
Balozi, endelea kuendesha Gulobu hii ya jamii tuzidi kupanuka mawazo kuhusu yanayoendelea ktk hii dunia ndogo-global village.
Mdau
Sehemu za Mgeni Nani Mbagala DSM.
Aaah Michuzi bwana... acha kuharibu ratiba, si ulisema kabla ya kuja Australia utapitia New Zealand kisha ndo uende Japan, nafikiri utakuwa umepitiwa kwa bahati mbaya!!lol
ReplyDeleteTo be perfectly honest, I think Michuzi is typically too personal in most postings hence creating a sense of egocentricity. This is just a personal opinion, anyway...
ReplyDeleteni majungu na unafki hakuna kitu kama hicho roho mbaya tuuuu cha msingi ni kuwa UKO JUU SANAA TUUU blog iko na akili zote,na hii ni moja ya changamoto kwako wewe na kila mtu hapa duniani kuwa kuna watu hawapendi kuona mafanikio ya watu bana na kama vipi tunakomaa nao tu.
ReplyDeleteMleta mada hajui kinachoendelea ndani ya Mivhuzi blog. Endeleza ligi huko huko JF sie huku tuachieni mkuu wa wilaya ya Tegeta (a.k.a Naniiii) na vekesheni zake USA.
ReplyDeletePilipili ya shamba.....
Jamii Forum-Home of STUPID thinkers
Michuzi, mtaa wa pili kuna maswali wameuliza hambayo bado hujaya jibu, kwa mfano swala wewe kuwa kwenye ziara rasmi ya Rais, huku ukilipiwa kwa pesa za wananchi je hiyo nayo ni 'vekesheni'?
ReplyDeletehaters hao, hawatakaa waendelee. Huyo kiumbe sijui katokea sayari gani!!kama ni kwenye msafara wa Rais au vakesheni, yeye inamuuma nini? The person should Get a life. Ama kweli waosha vinywa hawakosi cha kusema!! Big up michu wewe endeleza libeneke la vakesheni, hicho ni kijiba. Keep updating..... Enjoy your vakesheni. Wenye wivu wajinyonge.
ReplyDeletemh.........!!!!
ReplyDeleteKaka endelea na veksheni kule mtaa wa pili wanajulikanika (sio wote)jinsi walivyo mahasidi!wanajiona wanajua kila kitu kila mtu kwao mjinga wenye akili ni wao !Tunakutakia kila lililo jema!
ReplyDeleteHUO NDIO MTAJI WETU SISI WAAWEUSI BILA HUO HATUJITHAMINI NA TUNAONA MAISHA YETU NI BURE. UBORA WA MAISHA YETU NI KUKEREKA KWA HATA KACHEMBE KADOGO CHA MAFANIKOI YA WENZENTU.
ReplyDeleteatakufa kwa kiliba cha moyo kaka kula libeneke na raha ndani yake
ReplyDeleteAchana nao hao WAPUUZI.. Tatizo ulipokuwa Vakesheni, ulisahau kabisa kuleta habari za nyumbani. Inabidi uchanganye mboga kidogo, usikolee saaaana na huo MRENDA wa Kikwete.
ReplyDeleteSasa changanya madawa na ulete habari za MATOKEO YA UCHAGUZI BUSANDA then uone watu watakavyosuuzika ROHO ZAO MBAYA.
MlaKuku.
Kaka mithupu mkuu wa wilaya ya nanihii, hao ni waosha vinywa tu hawana watu wa kutembelea forum yao wanatafuta umaarufu. Kaza buti kaka wanataka Mheshimiwa Rais akipumzika ukae miguuni pake?!!!!!!kazana kutuhabarisha tena ziara ifike hadi Dubai wapate cha kusema utujie na picha ya mkoko ulionunua.
ReplyDeleteBest wishes
Mdau
No body can stop you!!
ReplyDeleteHilo ni donge na mwenye wivu ajinyonge!!!
Mdau canada!
Mzee Gadi alimjibu hivi yuke mwananchi
ReplyDelete========Nadhani mkuu wangu utakuwa humtendei haki Michuzi. Hivi ungekuwa wewe umeenda safari, tena nchi za nje, usingependa kuwaona watanzania wenzako huko? Usingependa kupiga picha? Hivi unajua kwamba JK baada ya mikutano yake masaa ya jioni anafanya nini? Ukimkuta anacheza draft au golf utasema kaenda Marekani kutumia hela za wananchi kucheza gofu! Mi nadhani tujadili mambo ya msingi hapa. Sio kujadili masuala ya oo michuzi kanunu soda, sijui kapiga picha na nani. Hili halitusaidii. Kusafiri kwenda nje kwa hela za walipa kodi haimaanishi kwamba ukifika huko hata usizungumze na simu. Maana utaibuka na kusema eti anatumia hela za walipakodi kupiga simu. Kwa taarifa yako tu, ukisafiri kwenda nje hela yako unapewa kulingana na cheo chako ukiwa mfanyakzi waserikali. Kwahiyo kama umepangiwa kukaa kwa siku 10 na alawansi yako ni USD 250 kwa siku, utapata USD. 2500. Sasa utasema nisisalimei marafiki na watanzania wengine ili nirudishe hela za walipa kodi nyumbani! Hapa hutuambii ukweli. lete hari za Busanda, sina maana zaidi.
"MJADALA WA FORUM UMEPOTEZA DIRA"
ReplyDeleteIngawaje tupo katika mfumo wa kuheshimu uhuru wa kila mchangiaji kutoka pande zote za wana-habari,lakini huu mjadala uliokuwepo "Jamii Forum" kuhusu "vekesheni" iwe ya malipo ya kiserikali au kibinafsi umepoteza "dira" ya maendeleo yanayotakiwa na wengi.
Ukumbi huu wa Michuzi ni wa jumuia ya watanzania ulimwengu mzima,ndiyo walipaji wa kodi,sote tunalidhika na "libeneke" ya kazi yake iwe "vekesheni au kikazi"ukumbi unatuwakilisha ki-taifa na ki-mataifa
mickey@mail-online.dk
Michuzi, kuweka hiyo taarifa hapa kumeongeza umaarufu wa hiyo thread kwenye JF ... ebu cheki watu wanaosoma hiyo thread sasa ...
ReplyDeleteCurrently Active Users Viewing This Thread: 567 (49 members and 518 guests)
AbbyBonge, Advocate Jasha, africa6666, Bint, Bluray, Chada, chap, ChingaMzalendo, CottonEyeJoe, Dawson, dlmihambo, Economist, epigenetics, gaijin, gangilonga, Godluck, Hage, Kagoma, kelelee, Kiazi kikuu, Kimambo, kisale, lbjm, Lilian, Magehema, Makaayamawe, mande, Mauza uza, Miwani, Mkora, mnyalandi, Mpiganaji, Mtoto, Mughwira, mwabaudi, Mwanafunzi, Mzizi, Nahene, ngoshombasa, Nguli, Rosemary, Rugishar, sk_mona, SurvivorD, Ulusungu, Wande, Wandugu Masanja, WILE, Yo Yo
Hello kaka Misupuz na wadauz wote. Kwanza nina amini hizo safari unazoziita vakesheni hujipangii wewe, bila shaka unapangiwa na unapopangiwa unapewa majukumu amabayo utatakiwa utekeleze utakapokua safarini. Even though I have no evidence, I am tempted to believe kwamba kazi yako unaifanya vizuri, otherwise usingekua unapangiwa kazi, tena nzito nzito kama hiyo ya kuongozana na rais, vinginevyo usingekua kila wakati unapangiwa. Kwa hiyo based on that, we Bwana Misup huna kosa kabisa, as long as unatekeleza majukumu ya serikali. Hao wanaosema unatanua it's up to them, yaani wao wanakuonea wivu tu. Kosa lako umekua too generous mpaka umeamua ku share na wadau your extra-professional activities. Hata hao kina rais wanatanua, lakini hayo hayaandikwi kwenye blog, ndio maana hawasemwi.
ReplyDeleteLabda hapa niseme tu kwamba sisi waafrika wavivu wa kufanya kazi, yaani kazi ambayo ingefanyika in 2 days, watu wanafanya in one week; na ndio maana unakuta hizo safari haziishi. Kwa mfano tu, nitatolea kwa wabunge wa Ubeljiji walienda safari ya kikazi Marekani majuzi na jamaa waligundulika walitumia muda mwingi zaidi kwenye starehe kuliko kazi. Ishu imekua noma mpaka wametakiwa kujieleza, ikiwa ni pamoja na kurudisha hela walizotumia, maana ni za walipa kodi, sio za kutanulia maisha.(check hapa kama unaelewa ki french - http://www.lefigaro.fr/international/2009/04/16/01003-20090416ARTFIG00288-sept-deputes-wallons-aimaient-trop-le-tourisme-des-canyons-.php )
Kwa hiyo hata we Misup ukirudi, ukigundulika hujafanya kazi uliyotumwa kufanya, ndio ulaumiwe; otherwise live in peace; it's ur time kutesa, na bahati haiji mara mbili.
Mdau, Belgium
Mheshimiwa Balozi wa nanihii pia kumbuka katika ratiba yako Istanbul - Ubatani ilikuwepo. Achana na wapayukaji. Wangapi wanasafiri kila siku na ku-mingle na ndugu na jamaa zao abroad? Si vile tu hatupati picha zao? Hawa JF nafikiri wanaitamani sana nafasi yako maana wameacha ya Busanda ya Mafisadi wa Billions of Shillings Bongo wanakuchambua weye wa kupewa kaposho kadogo ka kusafiri!
ReplyDeletekaka misoup sisi wabongo tuna uwezo mdogo wa kufikiri kwa sababu Michuzi baada ya shughuli za ofice kuna mda wa ziada ndio anautumia kutuhabarisha upandae wa pili na nijuavyo mimi kazi za ofisi ni masaa 8 baada ya hapo mtu anafanya extra milege. huyu mtoa mada anafanya kazi gani isiyo na mda wakupuzika au kufanya shughuli zake binafsi si ajabu huyu ndo akifika ofisini masaa 4 chai masaa 2 dinner la mchana halafu baada ya hapo nyumbani. mbona picha za siku zote za bongo halikuwa hasemi ni hayo tu.
ReplyDeleteMichuzi we endelea kutuletea ma snepu ya vekesheni na tunakusubiri Sydney Australia kwa hamu kubwa
ReplyDeletemdau Sydney
Mdau,
ReplyDeleteSevu kama siku mbili tatu hivi uje kuzimalizia Butiama.
Miye nasubiri picha zaidi za Vekesheni. Kaka Michuzi usitubanie, zimwage. ( BTW: Pale maeneo ya karibu na Ikulu ya Magogoni mchana huu niliona dalili za maandalizi ya ujio wa msafara wa Mheshimiwa Sana)
ReplyDeleteEndelea kukamua vekesheni yako anko michuzi usimalizie Japan njoo Canada.Enjoy your vekesheni,usijali na maneno ya watu!!!
ReplyDeleteAdvance party zote huwa za ma-Protokali/ShuShuShu!
ReplyDeleteProtokali/ShuShuShu Mstaafu (tulikula raha)
Sasa Michu kwa nini unawapa chati wajomba hawa, walikuwa wanatafuta watu kwenye site yao. maana walikuwa wanabishana wao kwa wao na wote wako kwenye payroll za mafisadi pamoja na chadema!sasa hivi ushajaza watu JF na wanatakiwa wa kushukuru kwa hilo.
ReplyDeleteMimi naona hata kama unatumia hela za walipa kodi kazi inaonekana picha zinapigwa habari zinatolewa sasa taabu iko wapi. Huyo atakuwa ni mtu mwenye bifu na wewe kama ilivyokwaida kwa wabongo wengine hawapendi kuona mtu anafnya kitu. Vacation na Nanii ni lugha za utani hivyo vinaeleweka fika unelss ni mgeni humu. Michuzi kama ungekuwa mtu wa hela ungeweza fanya mtandao wa jamii kuwa members only ambapo watu wangelipia/subscribe per year na ungetengeneza ufisadi wa kutosha. Sasa kila kitu unatoa ni free mtu bado anapiga kelele. Inaonekana ni tatizo la mbaya wako mmoja hivyo tafadhali endeleza libenekeke
ReplyDeleteNIBORA UKAJIBU HOJA KWANI MPAKA AMEFIKIA HAPO KUNA LILILOMKWAZA.WAPE MAJIBU WARIDHIKE!
ReplyDeleteWEWE MICHUZI ACHA KUTUZINGUA,MADA INAKUHUSU WEWE UNATUAMBIA SISI TUCHANGIE,TUCHANGIE NINI SASA? WEWE FAFANUA NA UTOE UKWELI MAANA HOJA HII SIO KWAMBA NI YA KINAFIKI WALA CHUKI,JAMAA ANATAKA KUJUA KAMA ULIVYOONA HOJA YAKE JAMAA KAITOA KAMA SWALI LINALOHITAJI MAJIBU. JIBU SWALI BWANA KASANDE!!(FROM THE MOVIE'NELIA') HAHA AHAHA
ReplyDeletemahaters hawana mpango wowote , kaza buti mzee , endelea kutupa masnepu ya vekesheni kama kawaida
ReplyDeleteBÄ°G UP BRO
achana nao mwana kula maisha!!! endeleza libeneke mwanangumwenyewe bongo wanga wengi!! ukisikisia mbongo nuksi ndo hiyo sasa. huko ni kufuatilia maisha binafsi ya mtu. ooh anapiga picha mbona alipoweka picha ya obama na kikwete hamkuchonga wandugu?? sasa nyie mnataka yeye awe binadamu wa aina gani yani hata baada ya mizunguko ya kikazi asi-socialize?? asitembelee nduguze wabongo walioko huko hili ni kosa??? na akiwatembelea mnataka asipige nao picha?? ukweli ni kwamba michuzi baada ya kazi zake hazuiliwi kufanya mambo binafsi, hazuiliwi kupiga picha za streets LA, DC au popote, hazuiliwi kupiga picha na sunday shomari, au na watanzania waliokuwa kwenye mpira, je kama hazuiliwi kufanya yote haya, iweje azuiliwe kuyaweka kwenye blogu yake tena ya binafsi??? huyo aliyeweka hiyo topic pale jamii forums nadhani ana upeo mdogo sana wa kuangalia mambo. kwani yeye akienda sehemu mpya mbali na kazi iliyompeleka anakatazwa kupiga picha, je anakatazwa kuweka picha hizo kwenye album yake, sasa michuzi kuziweka kwenye blogu yake si sawa na kuziweka kwenye album yake???
ReplyDeleteBesides, kwani blogu yake inafadhiliwa na serikali??? kwani ni blogu ya serikali?? hii ni private blog sasa iweje azuiwe kuweka picha za hata anapotembelea nje??? sioni point yake huyo bwana!!
ajue michuzi mjanja na anaendesha blogu yake kwa nguvu zake na kwa ufadhili usio wa serikali so yuko huru na picha zisizo za kiserikali ili mradi tu hajamtukana mtu!!!!
waache wivu, kama na wao wanaendesha blogu basi wachakalike wazifanye blogu zao zipendewe kama ilivyo hii ili nao waweze hata kupata ufadhili wawe kama michuzi sio kukalia majungu hiyo ni dalili ya mkosaji.
Ni mimi niliyewahi kutesa maishani.
MACMUGA.
wabongo kwakuzusha Huyu michuzi yeye ni mpiga picha wa Gazeti za serikali sasa kazi yake ni camera Mkononi.kwahiyo yeye anatembea akisnap taswira za matukio,haijalishi ndani ya msafara wa kikwete au out ya msafara wa kikwete.kwani kupiga picha ktk taswira zitakazo kuvutia lazima upewe ruksa ya walalahoi wakibongo
ReplyDeleteKAMA KAWA MKUU WA WILAYA YA NANIHII, KUMBE WATU WALIKUWA WANAPIGA RAMLI NA NDO MAANA DEGE LA KLM LILIMWAGA WESE,, HIZO NI ROHO MBAYA ZA WATU WEWE KULA RAHA KWA RAHA ZAKO..
ReplyDeleteMDAU LONDON.
Mkuu wa wilaya ya nanii, ujastukia kuwa "vekesheni" ya the STATES na wewe kukutana na wadau wakiwa poa na wanaendeleza libeneke inawaumaa sanaa wapuuzi. Ambao walikuwa wakipondea sana watu wa US wakifikiria tuko ovyo ovyo.
ReplyDeleteBro. sisi tunakupa-tough, pasua mawingu na endeleza "vekesheni" ya kutuhabarisha jinsi wadau wenzetu walioko anga zingine wanaendeleza vipi libeneke.
Kwa hali hii,kuwa makini kabla hawajakupiga juju
ReplyDeleteJamaa eti anasema kwa kipato chake hawezi kwenda vksion, Wewe unajua jamaa anafanya nini? Ina maana mtu hawezi kusave akaenda mapumziko, Mambo si bajet tu bwana! Ok jamaa kaenda USA bado anatupa habari za hapa na pale si tunachojari ni news, anatumia pesa ya serikali ya kwake poa! fine! Si bora ya Michuzi kuliko hao mafisadi wanaotuibia mpaka kwenye mifuko yetu! Kila kitu Tz kiko juu umeme! simu shauri ya hao mafisadi. Watu wengine Bwana! kama unajari si kamhoji Mramba na Kina Lowasa wanaotumia vibaya pesa ya serikali!
ReplyDeleteKiazi cha wapi hiki??????????
MISUPU KAZI NZURI ; USIPOTEZE TIME YAKO KUBISHANA NA WASHAMBA HAO; KAMA WANATAKA KUKWEA PIPA BASI WAWE MARUBANI;
ReplyDeleteKILA MTU ANA KAZI YAKE NA ANAHESHIMU YA MWENZIYE; MBONA HATULALAMIKI KUWA WAFANYAKAZI WA COCA COLA WANA KUNYWA SDA BURE KIWANDANI.
HAO WATU UFAHAMU MDOGO; ETI SECRETARY APIGE PICHA ZA SERIKALI UMEONA WAPI;
HAWAJUWA KUWA PICHA HIZO ZITAWEKWA KWENYE MAKTABA YA SERIKALI NA ZITAKAA KWA MIAKA CHUNGU TELE HIVYO LAZIMA ZIPIGWA NA PROFESSIONAL PHOTOGRAPHER
WIII WATANZANIA.
Watu wengine hawana shukurani hata kidogo. Hawafurahi hata kwamba kuna mtu mmoja anayejitolea kutupasha habari za sehemu mbalimbali. Je Serikali yenu inafanya haya? Siku zote wakubwa wanaenda nje, hawaendi na waandishi? Nani kawaonyesha hapa picha moja? Je nani kawaonyesha ndugu zenu waliopo huko viongozi wanapotembelea? Mnalipia nini kwa kichuzi kuona yote haya? Hacheni kuchonga rather learn to appreciate. Big up Michuzi endeleza libeneke na ukufika Australia usiache kutusalimia NZ ukiwa free.
ReplyDeleteROHO YA KOROSHO, YA KWANINI , NI MUNGU NDIE ANAPANGA WALA SIO MICHUZI,
ReplyDeleteMichuzi
ReplyDeleteNilishakwambia kwa hizi 'vekesheni' zako wadau lazima watakupiga vita .Si unaona mwenyewe sasa.
yaani kweli we Michuzi ni nimekukubali. yaani umeuliza swali ili kujua kama watu wanajua kazi yako. haya bwana umefanikiwa.
ReplyDeleteHATUJUI. hilo ndo jibu sahihi. wewe ni vacation tu.
Busanda-sisi tumeshaoa tayari na mrembo amehamishia matusi nyumbani.
ReplyDeleteWadau wa jamii forums wameuliza tu kwa kuchelea nanihii asije kuwa amefanywa fisadi.
ReplyDeleteYaelekea wadau wa jamii forums hawatambui kwamba vekesheni za nanihii zinategemeana sana na hali ya kisiasa nchini au tuseme raisi aliyepo madarakani. Kwa kipindi chote cha Vasco da Gama kuna uhakika wa vekesheni kuwa bwelele.
Michuzi we endelea tu na shughuli zako - wajinga ndio waliwao. Nimekubali msemo - akili ni nywele, kila mtu ana zake.
ReplyDeleteNadhani hapa brothers and sisters kuna kitu cha kujadili na sipo hapa kumtetea Michuzi au kumtetea mdau wa JF bali nitasimama kwenye hali halisi.
ReplyDeleteKwa mtazamo wangu ziara ya Rais huko America haina manufaa makubwa sana kwetu sisi kwa sasa(naruhusu ukinzani). Sababu kubwa ni kwamba kiuchumi ni sie ndio tulioifaidisha America kwani tumepeleka fedha zetu kule kwa kipindi chote Mheshimiwa alipokuwapo huko.Na sisi tukiambulia ahadi ya misaada toka IBM,Google na chuo kikuu cha ,kwani ilivyo hali halisi wamarekani hali ni ngumu kwa sasa uchumi wao upo kwenye ressesion,hivyo watu wengi wanabana matumizi kwa sasa. Kitu kingine ninachofikiri ni aina ya uwekezaji toka magharibi,binafsi nadhani hatujanufaika nao na zaidi zaidi unatuzidishia umasikini na kutuongezea hali ya kujiona tuna haki ya kuomba misaada.
Binafsi ningependelea kuona mheshimiwa rais akifanya ziara za mara kwa mara katika nchi za Asia hasa Thailand,Malaysia, na Singapore. Hawa jamaa wamefanya mapinduzi makubwa sana kiuchumi tena kwa teknolojia rahisi sana. Kama kuna watu wanaofuatilia records utaona kwamba nchi hizi zinaongoza kwa uzalishaji wa mchele duniani. Wakati huku kwetu tuna mashamba makubwa ya kilimo wenzetu wana arhi ndogo sana ya kilimo lakini mazao wanayozalisha kwa mwaka ni mengi mno kulinganisha na sisi kwani wenzetu wameweza kumudu kutumia tekinolojia rahisi sana ya kutumia kilimo cha umwagiliaji na matreka hata ya kusukuma na mikono.Binafsi nilioneshwa mkulima mkubwa kwa kithai ambaye amefanikiwa sana kwenye kilimo lakini cha ajabu niliambiwa ana shamba la ekari 6 tu! output ya hizo ekari 6 ni sawa na ya mkulima wa mpunga tanzania mwenye shamba la ekari 50 kwani jamaa anavuna mpunga mara nne kwa mwaka.Ukiangalia vizuri teknoloji wanayotumia si kubwa kiasi cha sisi kushindwa kujifunza na kuitumia kuinua kilimo nchini ili kupungua gharama za maisha kwa watanzania.
Pia nchi hizi zipo juu sana duniani kwa mauzo ya madini na vito duniani alihali wao hawana utajiri wa vito kama ilivyo Tanzania. Jamaa wanateknojia nzuri na rahisi inayowawezesha kuongeza thamani madini yetu wanayoshukua huku sasa sie kwa nini tusijifunze technolojia hizi ili kuongeza thamani ya madini yetu?
Jamaa hata kwenye soko la Amerika ni wao wanaoongoza kwa kuuza samaki wa maji baridi na mbogamboga kuliko sisi tulio na maziwa mengi mito mingi na mabwawa ya samaki, tatizo ni nini? kama tunataka maisha bora kwa watu wetu na maendeleo ya nchi kwa nini serikali isiwekeze nguvu kuipata hizi technologies kutoka kwa hawa jamaa? Rais anatakiwa tuelewa kwamba hawa wamarekani hawana lengo la kutusaidia sisi tuondokane na umasikini bali wao wanamalengo yao.
Pia jamaa hawa wameweza kufanya mapinduzi makubwa sana kwenye sekta ya bandari wakati sisi tukiwa ma bandari takribani tatu kwenye bahari ya hindi lakini tunachopata kutokana na utendaji wetu ni aibu.Viongozi wetu wafikie wakati sasa waone aibu kuomba misaada na badala yake wainue jitihada za kuleta maendeleo.
Kwa mdau wa JF kuhoji vekesheni ya Michuzi nadhani alipaswa kuhoji faida na hasara za safari hizi za Rais na convoy nzima kwa uchumi wetu
Mdau toka Mbezi
JK MWENYEWE AMEKIRI KWAMBA KUNA WATANZANIA WAVIMBA MACHO!!
ReplyDeleteKUNA WATU WANA ROHO ZA KWANINI????
MICHUZI WAKATI NI WAKO ENDELEA KUPETA TENA WANAVYOKUANDIKA KWENYE VYOMBO VYA HABARI UJUE NDO UNAZIDI KUJULIKANA. UNAJUA WEWE NI CELEBRITY MICHUZI! ENDELEA KUPETA TUMIA NAFASI HII IPASAVYO KAMA NILIVYOSEMA AWALI ENDELEA KULA MATUNDA YA KAZI ZAKO.
CHA KUWAUMIZA WAVIMBA MACHO ZAIDI NINAFANYA MPANGO WA WEWE KUPATA ZANA MORE ADVANCE NA NITAWASILIANA NA WEWE ILI TUKUPANDISHE NEXT LEVEL YA KAZI YAKO.
ZUNGUKA DUNIA NZIMA KAKA ANAEULIZA PESA UMEPATA WAPI HIYO SIO KAZI YAKE KWANI HAKUNA ANAYEKULETEA KIBABA CHA UNGA NYUMBANI KWAKO WALA KAUZU KUKUPA SUPPORT YA FAMILIA YAKO.
WAVIMBA MACHO ACHENI ROHO ZA KWANINI KWANI KWA ROHO ZENU MBAYA KWA WATU WANAOFANIKIWA MWENYEZI MUNGU ATAWAFUTILIA MBALI NA MTAKUNYWA SUMU NA KUFA KWA ROHO ZENU MBAYA ZA KWANINI??
PETA MWANGANGU TULITEE HABARI ZA KILA SIKU. BLOG HII YA MICHUZI IPO JUU YA VYOMBO VYOTE VYA HABARI TANZANIA.
Ni mimi mdau wa USA na mkereketwa wa Michuzi
DUH!! ebwanaee!! si mchezo! mchangiaji wa 2:08 hicho kiingereza!!! dah!!! kweli kazi ipo!!! si ungetumia kiswahili tu mtaalam tungekuelewa tu. gego mwanangumwenyewe kama halipandi usilipandishe kwa kulifosi inakuwa howcome!!! we kama vipi ungemwaga kiswazi tu tena kile cha nzese darajani tu mwana.
ReplyDeletehaya mtaalam naona na wewe umetoka, lakini ndo mambo hayo watajuaje kama nawe mtaalam upo??
MacMuga.
Achani kushabikia ujinga nyie..! huyu jamaa anajisifia na hela za walipa kodi wa Tanzania, JK akiwa Califonia na yeye vakesheni huko alivyoenda kuonana na Oboma, DC na yeye vakesheni DC. Tutumie vizuri kodi za wananchi, sio kutumia kujifagilia hapa. Najua utabana lakini UKOME. Ungepita huku kwetu tungekulamba stick.
ReplyDeleteMichuzi!! You don't have to explain anything to anybody...if you boss is aware that you are going different states to have fun. That's all matters...others are haters, they wish they can trade places with you. Even if you spend tax payer money, does not exceed $10,000. How many "mafisadi" do we know bongo? And they stole thousands if not millions of dollar. And nobody say anything....they go after small fish (Michuzi), if they want to find corruption go after big fish and we have names...but don't try to use Michuzi blog as your step stone to your success...Quit been Jealousy do your own thing.
ReplyDeletepole sana mdau
ReplyDeletelakini michuzi mi naona ni kweli alichoongea jamaa kwenye jamii forum tuwekee wazi upo huko kwa msafara wa rais au vekesheni je unatumia pesa yako au ndio na wewe ni fisadi unatumia kodi za wananchi
fisadi rtu wewe michuiz na wewe ndio ze utamu wewe
sio vijiba mdau ana haki ya kuuliza kuhusu watumishi wa nchi yake, mseende mbali kwa kuwa nanhii wetu ameguswa, kama kweli yupo na ziara ya mkuu lazima afanye kazi ambazo anatakiwa kufanya na sio kuzungumzia vekesheni.
ReplyDeleteIla swala la kuuliza nanhii anapata wapi hela binafsi za kuwa na safari binafsi si sahihi, kila mtu anajua mwenyewe jinsi anavyocheza na bajeti ya mfuko wake na jinsi anavyotafuta kipato kwa njia zingine baada ya muda wa kumtumikia mwajili.
Nanhii kama upo kikazi fanya kazi na acha habari za kujifanya mtalii wakati walipa kodi wanataabika huku.
Ni hayo kwa sasa
POLE KAKA MICHUZI.
ReplyDeleteMIMI HAO JAMII FORUMS NILIACHANA NAO ZAMANI SANA KWANI KULE NI KUISIFU CHADEMA TU,
WAMEKUTUKANA KWA MUDA MREFU NA KUIKANDIA BLOG YAKO HASA YULE MWANAKIJIJI,
HAWA WALIKUWA WANAITWA JAMBO FORUM WAKAIBA BRAND YAKO YA BLOG YA JAMII WAO WAKAWEKA JAMII FORUMS.
NI KUNDI LA WACHAGGA WA CHADEMA KAZI YAKO KUMTUKANA RAIS WETU,MAWAZIRI NA SERIKALI UKIWAKOSOA WANAKUFUNGIA.
NI FORUMS ISIO NA DEMOKRASIA,KIBAYA ZAIDI HAO KINA MWANAKIJIJI WAKIWA NA JAMBO LAO WANALILETA HAPA HAPA KWAKO.
HUKU WAKIKUONEA DONGE MOYONI.
WALIWAHI KUTUNGA UONGO KUWA ISSA MICHUZI ATAPEWA UPIGA PICHA IKULU WAKATI HANA SIFA,NILIBISHANA NAO SANA JUU YA HILI KUWA KAMA ISSA MICHUZI HANA SIFA ZA KUPIGA PICHA NANI ANAWEZA? HAWAKUHOJI FREDY MARO ANA SIFA ZIPI ZA KUPIGA PICHA UKIGOOGLE UTAONA UNAFIKI WA HAWA KINA MWANAKIJIJI.
MIJADALA YA JAMII FORUMS IMEGUBIKWA NA UDINI LINAPOTOKEA JAMBO KWA MUISLAM BASI WAO WANAMKOMALIA.
UCHAGUZI WA BUSANDA WAO WALISHATOA MATOKEO KUWA CHADEMA ITASHINDA KWA ASILIMIA 55.
AKATOKEA MTU KUPINGA AKASHAMBULIWA SANA.
JAMII FORUMS HAINA UMAARUFU WOWOTE KWANI IMEPOTEZA MWELEKEO,WATU WA MAANA WOTE HAWAPITI KWANI NI KAMA TAWI LA CHADEMA.
HALAFU MTU MMOJA ANAKUWA NA MAJINA ZAIDI YA KUMI KAMA MWANAKIJIJI ANATUMIA MWAFRIKA WA KIKE,BI SENTI 50,MADELA WA MADILU,KOBA,NYANI NGABU,KELLY 01,ANAANDIKA YEYE HALAFU ANAJIJIBU,NI KAMA KARATA TATU MCHEZO WA KITAPELI.
MICHUZI UKO JUU SANA LABDA UWAWEKEE PICHA ZA MWENYEKITI WAO MBOWE ALIPOKUWA DJ AKIWA NA KALIKITI KICHWANI PALE MBOWE CLUB, WAJUE KUWA WEWE NI MKONGWE KWENYE FANI.
KINGINE HAWA WATU WAKO NJE ILA WENGI WAO HAWAWEZI KUSAFIRI KAMA WAKO DETROIT MAREKANI LAKINI VIBALI VYAO HAVIWARUHUSU KUSAFIRI YAANI WAKO CHIMBO AU UNDERGROUND WENGI WAO WANASUBIRI LABDA RAIS OBAMA ATATOA MSAMAHA WA ILLEGAL IMMIGRANTS,
NDIO WAWEZE KUJA NYUMBANI KUSALIMIA NDUGU NA JAMAA AU KUSHIRIKI KWENYE KAMPENI ZA VYAMA VYAO AU KUJA NA MAITI INAPOTOKEA MISIBA,
KINGINE NAULI YA TZ NA MAREKANI NI KUBWA HIVYO KAZI ZAO ZA KUWATAWAZA WAZEE HAZIWAKIDHI KUPATA TIKETI YA KWENDA HOLIDAY,
CHUKI ZAO ZOTE NDIO WANAZIWEKA JAMII FORUM KWA KINA MICHUZI,RAIS WETU N.K
NI MIMI MDAU MSWAHILI NILIYEKUWA JAMBO FORUM KABLA YA KUKOPI BRAND YA MICHUZI NA KUIITA JAMII FORUM, NIMEACHA KUCHANGIA BAADA YA KUONA TUNAJADILI UCHAGGA,UCHADEMA NA UKRISTU TU.
MDAU.MSWAHILI.
Mie nasema huyo vasco da gama bado anavumbua na katika safari zake lazima awe na mtu wa kupeleka ripoti nyumbani... HAPO ndo michuzi chukuchuku anapoingia... kwani wale watalii wenzake mbona hamwataji? kwa hiyo wewe endeleza libeneke na naona safiri hii vasco kamsahau kim mugaya. Nae na mithupu wote jamii moja....
ReplyDeleteKeep on keep going on....
mdau kinondoni
BOTHER MITHUPU, NAIPENDA SANA BLOGU YAKO MAANA INAONYESHA MAMBO YA MAANA KITAIFA NA KIMATAIFA.
ReplyDeleteKULE JAMII NI BLOGU YA WATU WASHAMBA WASHAMBA TU AMBAO NDO WAMEKWENDA KWA MARA YA KWANZA MAJUU.KAZI KUPONDA WA-TZ,UTAFIKIRI WANAJUA KITU KUMBE VICHWA VITUPU.
MARA NYINGI UKIWAPASHA KIAKILI KWA KUWAZIDI WANAKUFUNGIA MTANDAO WAO.
MI NILIKUWA HUKO NAJITOA NA MITANDAO YA WATOTO.
Tena bro Miposi usiwasililize hao Jamiiforums,forum ya watu wanao oneana wivu wenyewe kwa wenyewe,Wivu wao uishie hukohuko, lakini karibu ututembelee Tandahimba,Newala njomba!!!
ReplyDeleteJAMIII FOLAMU ACHENI WIVU ENDELEZENI BLOG YENU VAKESHENI LA MKUU WETU WA WILAYA MH.NANIII LINAWAUMA NA MBADO NA MTAJUUUTAAA KUMFAHAMUUU.
ReplyDeleteHuyo jamaa nimeona post zake ni za hasi. Anafaa aambiwe"pilipili usoila yakwashyani"
ReplyDeleteMichuzi unatakiwa ujuwe kuwa "Kijicho kipo" na "Husuda ipo"
Huwezi kuendelea halafu shetani akuache bila kutumia jeshi lake.
Na ujuwe, Kila ngazi moja juu unakutana na shetani ngazi moja makali zaidi.
Bongo korosho bila mashamba tutaacha lini?
ReplyDeletekwa nini tunauza korosho zisizolimwa?
hajui maana ya neno vekesheni linavyotumika bongo.
ReplyDeleteMISUPU HATA KUIFUTA BLANKET CHAPA MTU NAZO UTUPE TUU HIZO PICHA HUSITUBANIE, MAANA BARIDI HUKO, AU HAIKO KWENYE PADIEM, NAZANI WAKIONA UMEFUTA BLANKET CHAPA MTU BASI WATAANDAMANA ZAIDI HADI KWA MYWIFE WAKO ILI KUSUDI MAMBO YAKO YAENDELE KUWA MABAYA.
ReplyDeleteKULA INCHI MISUPI, SI UNALIPA KODI,SASA KWANINI USIITAFUNE PIA?
Michuzi naona umeingia unatuingiza ktk malumbano ambayo hayataweza kutusaidia, Kumbuka raisi alishaongelea kuwa wabongo ni watu wa wivu (uraia wa nchi mbili) je kwa nini maoni ya mtu mmoja uone kama ndiyo maoni ya walio wengi? mtu mmoja anakulaza mlango wazi je wakiwa kumi utafunga Blog yako? Tafadhali sana sana Michuzi, kuchapisha hii Taarifa itaonyesha kuwa unatafuta huruma ya wasomaji wa blog yako, kwa nini usingepuuza tu? Najua wewe kama binadamu una mapungufu yako na haupo kamili na sahihi kwa kila kitu, na wakati mwingine unapitiliza kuingiza mabo yako binafsi ambayo wadau hatutakiwi kuyajua. Kosa lako kutangaza kuwa BLOG Hii ni ya jamii. na Advet zote unazopata ktk blog hii kutokana na kuwa ya jamii na wala si vinginevyo.Sasa wewe unafanya kosa lile lile walilofanya Papa Na Nyangumi kutumia vyombo vyao vya habari vibaya.Najua labda utakuwa umeumizwa na maoni yale lakini njia iliyobora ni KUPUUZA na wala siyo kutufanya tusome Jamii forum wakati wengine wala hatukuwa na habari nayo.
ReplyDeleteKaka miMichizi mbona nimekualika New york umegoma kuja? Mwenzio macho yamenitoka nilipoona picha zako kila kona. Mie nakutakia kila la heri na mafanikio tele tele maana kila nikiamka lazma nibonyeze blog yao kuona kitu kipya. Achana na na wenye wivu"watasaema sana usiku watalala" Kaka Michuzi huyo! kaka kaka Kaka huyo!kaka kaka huyo! Kaka! Libeneke litamu !litamu litamu jama! litamu litamu jama! litamu tamu jama! Blogu yameremeta! blogu yameremeta jama! Yameremeta jama!
ReplyDeleteJF AMBAO WANAJIFANYA WASOMI WA BONGO, WANA FIKRA POTOFU, WASIOONA MBALI (MYOPIAS) KUJIFANYA WANAJUA SANA VILIO VYA WATU WAKATI WAO WAKO MBALI SANA NA JAMII (NA UHAKIKA UTAPOKUTANA NAO HATA SALAMU ZA MKONO HAWAKUPI, LAKINI WAKO KIMBELEMBELE KUWACHAMBUA WATU NA ELIMU ZAO, NA MAISHA YAO KWA UJUMLA NA KUTUMIA NENO "FISADI" KAMA SILAHA YA KUWADHALILISHA WATU, MNATAKA JAMII IWAONE KUWA "MIUNGU MUTU" KUWATUNDIKA WATU KWENYE MTANDAO WAO WA JF - WIVU MTUPU!!!!
ReplyDeleteWASOMI WA BONGO!!!!! SI NDIYO NYIE MNAMSHAURI JK KATIKA DHANA POTOFU YA MTANZANIA KUTOKUWA NA HAKI YAKE YA KUWA NA URAIA WA NCHI MBILI (SABABU KAMILI HAWANA - "WIVU MTUPU") YOU PEOPLE IN (JF) GET LIFE, MICHUZI INABIDI SOMETIMES USAFIRI NAO KWENYE HIZO VEKESHENI WAKUTANE NA WATANZANIA HUKO UGHAIBUNI NA WAO WAPIGE PICHA ILI WAFUTE TONGOTONGO, NA WAJUE JAMII INATAKA NINI NA SIO WAO (KUNDI FULANI) LINATAKA NINI KWA MITAZAMO YAO. HATUTAKI WATU WENYE MPhD's WASIO NA SIFA ZA UONGOZI "BORA KIONGOZI" WATUONGOZE, TUNAHITAJI VIONGOZI WENYE VISION NA UWEZO WA KUONGOZA "KIONGOZI BORA" KWELI SASA NAAMINI KUWA KUSOMA SIO KUELIMIKA. JF LAZIMA MTAMBUE KWAMBA HATA SISI UGHAIBUNI TUNALIPA KODI HUKO TANZANIA (MFANO TUNAPOTUMA VITU HUKO BONGO TUNALIMWA TAX PIA)NA KUONGEZEA PATO LA TAIFA, HIVYO KAMA NI UCHUNGU HATA SISI TUNAO - MICHUZI ENDELEA NA VEKESHENI YAKO NA ENDELEZA LIBENEKE LA KUTUHABARISHA, HIVYO MSILETE ZA KULETWA KUWA NI NYINYI PEKEE MNAOGUSWA NA KODI (TAX)AMA MATATIZO YA TANZANIA. MDAU BUCKINGHAMSHIRE - UK
PLEASE DO NOT UNDERMINE THE ONE WHO STARTED THIS HUKO JF.
ReplyDeleteANAPIGA JUNGU LA AJIRA YA MICH-USE KWAKUWA PRESIDENTIAL VIP TRIPS HAIHITAJIKI KASHFA YOYOTE
TH3N MWENYE ROHO MBAYA ANATAKA JAMAA ATOLEWE KAZI AMA KUUA BLOG AMA VYOTE.
PLEASE TUMIENI BUSARA KUSHAURI NA HASA KUMWAMBIA JAMAA OPENLY KWAMBA NI MCHAWI NA ANATAKA JAMAA ATOLEWE AMA LOLOTE BAYA LIMTOKEE
NA WADAU TUSALI NA KUOMBA MWANGA AFE KABLA HAJAUA NA KWA SISI WAISLAMU TUMPIGIE DUA MAALUM ATOWEKE AMA AWE CHIZI ASIENDELEE KUSUMBUA WENGINE DUNIANI
NI NYOKA KWAKUWA HAKUNA BAYA MICH-USE ANACHOKIFANYA ILA KAPATA ZALI LA KUWA KWENYE MSAFARA WA MNENE THE PRESEDENT. PIA ANAONESHA NAMNA ALIVYO SOCIAL KWA KUTEMBELEA WATU WA KILA HALI NA NAMNA.
BINAFSI NAMPA SIKU 3 JAMAA AOMBE RADHI AMA HATOKUWA NA NAFASI YA KUHARIBU MAISHA YA MWINGINE DUNIANI. THE WORLD WILL BE THE BETTER PLACE WITHOUT HIM
HE NEEDS TO DIE NA TUUNGANE KWA HILO
NTAONGEA NA BIBI HAPO KOLELO NA NI VITU VIDOGO SANA KUMUADHIBU MJINGA KAMA HUYU ASIYEKEMEA MABAYA ILA CHUKI KWA MAISHA MAZURI YA WENGINE.
MWENYE KALI YA KUUA DAKIKA3 ANIJULISHE. HASA NYINYI WA SUMBAWANGA NA TANGA. VYA MORO NA BAGAMOYO VINATUMIA DAKIKA 6 KUUA
KINDA SLOW
USISUMBULIWE NA WENYE HUSDA MICHUZI. ENDELEA KUTUPASHA HABARI. WE VALUE YOUR WORK AND SENSE OF HUMOUR TOO. KEEP IT UP. WE KNOW IT IS A LOT OF WORK BUT NOW WE CAN'T DO WITHOUT YOU!!! ADA YA MJA HUNENA MUUNGWANA NI VITENDO. WEWE ENDELEZA VITENDO WACHA WASEME. WIVU MTUPU!!
ReplyDeletebro michuzi, achana na wambea
ReplyDeletekwani huyo jamaa alikupa nauli ya kuja huku US.
we kula raha na wabongo wa nje period.
Michuzi hayuko vacation, yuko vekesheni.
ReplyDeleteAsante kwa taarifa zote ya vekesheni.Ni fursa bomba kutunganisha na wadau wenzetu popote waliko duniani. Kwani tofauti iko wapi kuwa vekesheni na kuwa hapa si mradi cha kaisari anampatia na sisi wadau tunapatiwa cha kwetu pia.
Ila kaka matukio muhimu ya bongo yanapwaya ukiwa vekesheni. Kwa mfano safari hii ''ajali'' ya Dk Mwakyembe haijapata coverage kwenye globu yetu. Alafu ile funika funika ya baadhi ya viongozi (RPC Iringa kwa mfano) kusema eti ni ajali tu ya kawaida tu: mara mashimo ya barabarani, mara spidi ya gari ya mbunge, mara taarifa zinaaandikwa za uhakika bila kumhoji mbunge wala dereva wake, mara polisi wachore picha ya ajali bila kuonyesha lori iliyosababisha ajali, mara eti dereva ajitokeze Tanzania Daima kukanusha hakuendesha vibaya wala kugonga gari ya mbunge (lakini Polisi haendi na wala hatafutwi na Polisi na baada ya kuibetua gari ya mbunge kaongeza moto na kutokomea badala ya kusimama lakini anajitokeza Tanzania Daima siku 2 baada ya ajali(sijui Freeman, Slaa na Zito wamewauzia mafisadi lile gazeti?). Tafuta njia hata ukiwa vekesheni matukio muhimu kama haya yaonekane na yajadiliwe kwenye globu yetu- labda klama na wewe umewauzia mafsadikama Freeman.
VEKESHENI njema
Nasikia ze utamu amekamatwa????
ReplyDeleteMDAU MSWAHILI
ReplyDeleteMay 25, 2009 7:21 PM
MDAU UMENIFURAHISHA SANA NA HIO COMMENT YAKO
ITS TRUE HAWA WACHAGGA HAWANA MBELE WALA NYUMA WANATAKA KUSHINDANA NA KAKA MISUPU MZEE MWENYEWE BALOZI a.k.a NANIHIII
AMINIA MICHU NA VEKESHENI NAJIANDAA KUIPOKEA ZAWADI HIO YA MDAU WA MILIONI6
NI MIMI MBEBA MABOX
MDAU BIJO PASUA
tehetehetehe
ReplyDeletemie nasubiria tarakimu zangu kadhaa niwe mdau wa milioni sita.
JF haya mambo hamna nyie sasa donge la nini?
Mimi nilidhani majungu ni Utamu tu kumbe hata JF mnayo, hamna jipya.
Nadhani hiki kirefu cha JF kingekuwa JUNGU FORUM badala ya jamii forum.
Mdau Ukraine.
NB:na wewe mithupu mikonoozzzz tunaitaka huku, usitubanie eeebo!
UPUMBAVU MTUPU!
ReplyDeleteHIVI JAMANI HII TABIA TUTAACHA LINI? KUNA USEMI KWAMBA, 'DUNIA HII SI MBAYA BALI MIOYO YA WATU KAMA HAWA NDIO INAMWANGAMIZA MTU' BONGO KUNA HUSUDA YA AJABU! NDIO MAANA HATUNA MAENDELEO! MICHUZI ENDELEZA LIBENEKE, NA UTULETEE PICHA NYINGI ZAIDI...WATASEMA SANA MWAKA HUU!
MDAU
LONDON
KAMA ANATAKA PICHA ATALETEWA, ZA WAPI? SPAIN? PORTUGAL? UK? STATES? TUZIDI KUMKUNA ROHO!
dah!kaka michuzi angalia waswahili washaanza kukutolea macho,wanaweza kukupiga mbigili hao kwa bibi.WASHIKAJI TUACHANE WIVU BASI JAMANI!!
ReplyDeletehuyu kijana inaonekana ni mdogo haelewi kitu akili zake ziko kwenda ulaya kwanini chanse hii ya michuzi hajaipata yeye ambae siku nyingi anatafuta nafasi kama hio,huo ndio wivu ulipomjia,kama kusafiri tu sio michuzi pekee wanasafiri wengi tu watu blog wanaenda nchi tafauti na wengine pia wanasafiri hapo hapo tz lkn hajapiga kelele kwa vile nihapohapo tu tz lkn kilichomuuma ni kwenda ulaya,na pia michuzi kabla hajaanzisha hio blog alikuwa pia ni mtu wakusafiri,kwa hivyo kijana usijali na wewe utakuja ulaya kutusaidia kubeba maboksi zaid punguza hasira zako usimlaumu michuzi kwani kila mtu ana bahati yake.USICHEZEE BAHATI YA MWENZIO,subiri yako siku itafika na wewe utakuwa kama mwenzio.michuzi ni mtu wa watu sio serikali tu bali ulimwenguni kote michuzi ni mtu wa watu kama baba wataifa
ReplyDeleteI wanna know who's payin' 4all that???????????????????!!!!!!!!
ReplyDeleteJamanieeee mwacheni michuzi ajinome kama nyie mmeshindwa kufika majuuu si basi, ipo siku nanyi mtafika tu inshaallah!!! kama yeye amekuja na trip ya raisi it is non of your business (huyo aliyeanzisha hiyo topic) Michuzi ni mwandishi/mpigapicha na hiyo ni kama assignment yake yaweza kulipwa na yeyote lakini kumbuka kuwa anakampuni anayofanya kazi!!!! As others say hawezi kuwa na rais all the time hata yeye pia ana life bna haki ya kufurahia kama binadamu yeyote. Labda alikosea kuita "vekesheni" angeita safari mngemwelewa .......
ReplyDeleteBaba abdul/michuzi chapa kazi achana na hao ambao walinyimwa viza za kutoka nje ya nchi fanya unavyoweza....
Mdau
HATUWEZI KUNYAMAZA WAKATI ISSA MICHUZI ANAONEWA BURE.
ReplyDeleteHUYU MWANAKIJIJI AU BENEDICT MWAKYANJALA ALIANZISHA BLOG YAKE IMEKOSA WATU NA ALIKUWA ANAITANGAZA HAPA KWA MICHUZI KWELI HANA SHUKRANI.
WIKI ILIYOPITA WALIKUWA NA MKUTANO NA BALOZI AMINA SALUM ALI NA WALIPITISHA BAKULI LAKINI MICHUZI ALIWEKEA TANGAZO LAO HAPA,
BAADA YA MKUTANO WAMEMKASHFU BALOZI AMINA KUWA HAJUI KIZUNGU SOMENI HUKO KWENYE JAMII FORUMS MUONE WALIVYOKOSA ADABU HAWA VIBARAKA WA NGO YA WACHAGGA- CHADEMA.
MWANAKIJIJI KILA MARA ANAFUNGUA BLOG ZINAKOSA WATU.KAMEBAKI KULE JAMII FORUMS AMBAKO NDIO FULL TIME JOB YAKE KANALIPWA NA MBOWE KUWACHAFUA WATU.
WIVU ULIOPO BLOG YA MICHUZI IKO JUU SANA WAMEFANYA KILA WALIWEZALO ILI ISHUKE WAMESHINDWA.SASA WAMELETA MAJUNGU HAYA YA WIVU WA MCHANA.
FIKIRIA MTU KAMA MWANAKIJIJI ANGEKUWA ANA UWEZO WA KUJA TZ HOLIDAY TUNGELALA?CHAGUZI HIZI KAMA ZA BUSANDA ANGEKUWA ANAKUJA.
MASIKINI MAMBO YAKE YA UKAZI YAMEMKALIA VIBAYA AMEJIWEKA JELA YA KUJITAKIA HUKO MAREKANI.HAJUI LINI MAMBO YAKE YATAKUWA SAWA.
AMEJAWA NA WIVU NA MARA ATUMIE MAJINA KAMA LULA MWANA NZELA KULE KWENYE GAZETI LA RAIA MWEMA KUKIPIGIA CHAPUO CHAMA CHA WACHAGGA YAANI UNAWEZA KUIITA NGO YA WACHAGGA-CHADEMA KWANI VITI MALUUM VYOTE WAMEVIGAWA KWA FAMILIA ZA WACHAGGA KAMA MTOTO WA NDESAMBURO LUCY OWENA NI MBUNGE WA VITI MAALUM,GRACE KIWELU NAE MCHAGGA,ANNA KOMU NAE MCHAGGA.
HAWA JAMII FORUMS WANAJIFANYA WASOMI VIPI WATAONGOZWA NA DJ MBOWE KWANI TANZANIA IMEKUWA MADAGASCAR AMBAKO RAIS WAO DJ.
BRAVO MICHUZI TUTALIENDELEZA NA HAWA WACHAGGA WA JAMII FORUMS.
MDAU MSWAHILI.
Kwa upande wangu nimesikitishwa sana na hiyo habari niliyo isoma huko JF, inaonesha kwamba ndugu muandishi wa hiyo habari hakuweza kutafuta ukweli wa habari anayotaka kuandika bali kaweka wazi dhamili yake kwamba ilikuwa kutaka kuchafua jina la ndugu Michuzi na serikali kwa pamoja ili waonekane wabaya ndani ya jamii.
ReplyDeleteNakubali ndio kuna kitu kinachoitwa fredom of expression lakini uhuru huu ukitumika vibaya kunaweza kuleta chuki ndani ya jamii na madhara yake ni makubwa. Watu siku zote wanatumia Freedom of expression kwa kuwa na strong evidences pamoja na facts ambazo zinaweza kutengeneza constructive arguments ambazo matokeo yake yanaleta matunda mazuri ndani ya jamii, ila kwa jamaa wa JF kwa upande mwingine ameshindwa kufanya hivyo wala hana grounds zozote ktk kutengeneza case yake.
1: Michuzi utumia muda wake binafsi baada ya kumaliza shughuli zake zilizo mpeleka popote aendako, Swali je, unataka kusema kwamba baada ya kumaliza kazi zake aweze kukaa tu ndani ya hoteli siku nzima mpaka kesho yake ili aendelee na kazi iliyo mpeleka huko? Jibu ni hapana, Michuzi ana uhuru wa kufanya chochote nje ya muda wa kazi.
2: Muandishi wa JF, hawezi kujua kwamba hizo safari binafsi za Mh. Michuzi zinagharimiwa na mwenyewe, ndugu, au marafiki wa bwana michuzi na SIO kama alivyo sema eti pesa za walipa kodi, kwa maana kuchukua bus, train au tax na kutembelea ndugu na marafiki haiwezi kuzidi dola 15 ambazo ni kama Tsh 19,884, ambazo ndugu michuzi ana uwezo wa kujigharimia mwenyewe... Pia akiwa kama mgeni kwa ndugu au marafiki zake wanaweza kuja kumchukua na kutumia gharama zao kumpeleka popote.
Hivyo basi kutokana kwamba muandishi wa JF hana grounds zozote na kutokana na comment aliyo sema "Je, Issa Michuzi ni fisadi au anafadhiliwa na mafisadi kwenye safari zake?" Ningeweza kusema kwamba anatakiwa kumuomba radhi ndugu Michuzi mapema iwezekanavyo kwa kumchafulia jina, heshima, uaminifu mbele ya jamii pamoja na mwajiri wake. Pia JF iweze kuomba radhi kwa michuzi na kuweza kufuta comment isiyo kuwa na ushahidi wowote. Kama huyu ndugu "Uwiano Maalum" angekuwa anajulikana jina kamili ningeweza kumshauri bwana michuzi afungue case ya fidia maana shutuma alizotoa ni nzito sana ambazo zina mchafulia jina na kumtoa uaminifu Mh. Michuzi.
Ushauri wa bure kwa muandishi wa JF, next time aweze kutulia, kutumia busara, hekima, ushahidi wa kutosha ili aweze kutoa hoja zake kwa maana dunia ipo macho, Hasije kuchukua na kutumia chuki zake binafsi ktk kumchafulia jina Mh. Michuzi.
Innocent Until Proven Guilty, Michuzi is Innocent and will always be top and number One on everything, No one can stop that whether you like it or not...That is the fact.
MK
Michuzi isikukondeshe hiyo watu wataongea usiku watalala..Most of us love you...we were so happy to see you and talk to you when you were in DC...you are so down to earth kind of guy.
ReplyDeleteLeoKweli has no status.
ReplyDeleteJF Senior Expert Member Join Date: Wed Apr 2008
Posts: 282
Thanks: 57
Thanked 246 Times in 125 Posts
Rep Power: 22
Credits: 1,043,050
Re: Issa Michuzi na vekesheni
--------------------------------------------------------------------------------
Michuzi blog Net Worth is $ 50,618.20
Daily Page view is 22446
Daily Ads Revenue $ 69.34 which translate to $ 2070 per month. Do you want to tell me that with that additional income of $2070 per month which he generates from his blog , he cant afford extra holidays, give me a break.
Let us encourage kazi nzuri za watanzania wenzetu na si kuvunjana moyo.
yaani hii imeonyesha tena jinsi baadhi ya watanzania wengine akili zao ni duni yaani watu wanapoteza muda kuanza kujadilli kama issa michuzi anasafiri kwa pesa za walipa kodi sijui ni umaskini umetuzidi kwa nini msijadili mafisadi wanaokula mamilioni ya pesa kuliko kuanza kujadili visafari vya michuzi eti pesa za walipa kodi wewe yawezekana hata ulipi kodi unalalama tu hapa waandishi wa habari ni kawaida kuzunguka na msafara ya rahisi ni mambo ya kawaida nakutokana na maendeleo ya communication waandishi wa habaripia wanakuwa na nafasi ya kuripoti mambo yao private kupitia blogs ni mambo yanafanyika kwa waandishi wa habari wa cnn au BBC kwahiyo bwana mdogo kabla hujaanza kulalama na kutaka watu wachangie hoja yako ya kimpumbavu kaa chini na jaribu kujielimisha pum&%$§&?u
ReplyDeleteMuch to respect nanihii,you really raise the bar when it comes to blogger,nadhani blog ya nanihii ni nambari one anayebisha anyoshe mkono watu wamwone. Pili huyo anauliza michuzi kafikaje marekani kwanza aangalie tafsiri ya michuzi,maana yake ni pesa,
ReplyDeleteMichuzi uko juu, tena juu sana kwa blog yako ya kistaarabu.Kule tumepita wanaomiliki mtandao ule wanfikiri ni wao tu wenye akili, kumbe PUMBA TUPU.
ReplyDeleteNi vizuri wamekushambulia na watu hapa wameonyesha uozo ulikoko jamiiforums mtandao wa kijinga.
Wangejiita JamiiCST yaani Jamii Club of Stupid Thinkers.
Wewe endeleza libeneke na una connect na watu wa kawaida kabisa.Umenifurahisha p[ale ulipo nibeep na demu huko majuu linalokuzidi urefu ha ha ha ha !!!
michuziiiii,unakula bata sio.,ila ndugu yangu sikuhizi sio maskini mwenzetu ushakua tabaka tawala.
ReplyDeleteHuyu jamaa ana kazi tatu.
ReplyDelete1. Ni mpiga picha wa gazeti la serkali
2. Ni mdau wa blog(Anamiliki hii blog)
3. Ni shushushu (Usalama wa taifa) kitengo maalum cha mawasiliano ya internet . Huyu ndo alofanikisha kumuangamiza zeutamu...! Hii kazi ya ushushushu hasa ndo inayomfanya awe kwenye ziara za rais, na ile blog yake ipo kwa sababu maalum ;
1. kuwezesha kuangalia upepo wa siasa unaenda vipi kwa faida ya serkali ya CCM, kupitia comment za watanzania walio ndani na nje ya nchi...!
2. Kuwapumbaza watanzania walio ndani na nje ili wasiwe na muda wakutembelea blog za wanaharakati, amefanikiwa hili kwa kuweka vitu visivyoleta thread kwa serkali ya ccm, kwa kuweka matangazo ya urembo, mpira sijui (liverpool), na upuuzi mwengine tele, na hii inawafanya watanzania (hasa walio nje) wakose muda wa kujadili matatizo na umaskini unaoiandama tanzania kwa kukosa sera na uongozi mbovu...!
Napenda kumpongeza, amefanikiwa kwa hilo!
"call spade, a spade...!"
Mh Balozi na Mkuu wa Wilaya ya nanihiii
ReplyDeleteHuyo jamaa aliyeandika katika JF mimi ninamfahamu vizuri sana. Kijana aliyejaribu maisha na bahati mbaya amekuwa failure.
Amekuwa tapeli kazi yake ni kujipatia pesa kwa njia za udanganyifu. Amekuwa akichukua pesa za watu kwa ajili ya kuwaagizia magari ambayo ni hewa. HIvi tunavyoongea anatafutwa kwa ajili na Polisi kwa makosa mbalimbali ya udanganyifu.
Sioni ajabu kwa mtu kama yeye kuanzisha thread ile kule JF kwani anaona kuwa mafanikio ya Michuzi anatamani ndiyo yangekuwa ya kwake.
Pili, kule JF hiyo thread ni butu na pia iko chini ya kiwango cha JF. Lakini ni kwanini hata ma-moderator wao hawaifuti au kuificha, ni kwa sababu kwa njia moja au nyingine inaishambulia serikali, pia wanaiwacha kwa vile sasa hivi kuna mfanyabiashara mmoja maarufu hapo Dar anayemiliki makampuni kadhaa ikiweno TV stesheni na radio anatoa pesa kwa JF kwa ajili ya kuandika habari zozote zitakazobeba neno 'fisadi' au habari yeyote itakayomuunganisha mbaya wake kwenye ufisadi. Sasa hivi huyo mfanyabiashara huchukizwa na mafanikio ya kila mtu, kwa mfano hata hivi viblog vya akina michuzi anatamani angekuwa anavimiliki yeye.
Michuzi achana nao kabisa hawa jamaa wa JF kwao wanajua kila kiti hata wasichokijua wanajifanya wanakijua. Kuna jamaa mmoja kwenye ile forum baba yake alikuwa mgombea uraisi 2005 kupitia CCM alipigwa chini katika hatua ambayo hakutegemea, basi huchukua kila jambo analoongea na baba yake analiposti kwenye JF kwa nia ya kum-undermine aliyemshinda baba yake kwenye mchakato wa uchaguzi. Halafu huyu jamaa ana hasira sana na kiongozi mmoja ambaye anamhisi ndiye aliyekuwa kinara wa kusababisha baba yake kutoswa mapema. Jamaa alikuwa anafikiria sasa hivi ni jinsi gani ambavyo angekuwa anazitafuna pesa za walipa kodi kupitia wadhifa wa baba yake.
kusema kweli kaka Michuzi umenifungua macho leo. nimesoma maoni na kujua tabia ya watanzania. lakini vile vile nimegundua jambo jingine; kwamba kipindi fulani ulisema uko vakasheni Ethiopia na wakati huo President wetu alikuwa huko, sasa presida yupo DC na wewe pia vakesheni. hii inatia shaka fulani.
ReplyDeletelakini wewe unafanya kwenye gazeti la serikali. je raisi anazunguka na waandishi wangapi? kuna uwezekano wa kuwepo kwa matumizi mabaya ya hela ya mlipa kodi. tutaomba tume iangalie hili.
KUNA MCHAGGA ANAITWA J MUSHI AMEMKAZANIA MICHUZI SIJUI KAMCHULIA NINI.SOMENI KWENYE JAMII FORUMS.
ReplyDeleteBLOG YA WANYWA MBEGE.TENA LEO WAMEPATA TRAFIC YA AJABU KUTOKANA NA LINK YA MICHUZI WAMEPATA WATU KARNE ELFU KUMI KUTOKANA NA HABARI YA MKUU WETU WA WILAYA.
Nimejaribu kufungua li website lao haliko friendly kabisa sijui likoje likoje, ihii mwayego wewe ndo unaetukumbuka tunaojifunza computer globu yako ni rahisi kutumia. Kule mtaa wa pili ntashikwa tu na bosi wangu ni mbali mno. Asante kwa kudesign globu yako vizuri
ReplyDeleteMichuzi yuko vekesheni vacation au whatever kikubwa ni kwamba, kama mdau mmoja alivyokwishasema, anaendelea kama kawa- cha Kaisari anampa Kaisari na chetu wadau anatupatia. Now kama anafanya hivyo, what does it matter whether he is in Katmandu or Timbuktu? Si ndivyo anavyofanya akiwa Dar? We should be celebrating the wonders of TEKNOHAMA. Inawezesha kitu Kinaitwa tele-commuting mtu kufanya kazi akiwa mbali na kituo chake cha kazi, au anaendelea kuwa productive hata asipokuwa mahali ambapo palikuwa pakijulikana kama kituo cha kazi. Zamani, kabla TEKNOHAMA haijapiga hatua, usipokuwa kituoni kwako basi kazi hufanyi kama kazi ni za Kaizari au za wadau. Idumu TEKNOHAMA. Ila braza matukio ya home muhimu nayo tuendelee kuyapata hata uliwa vekesheni!
ReplyDeleteHivi kuna tofauti gani kati ya zeutamu na JF? Mimi naona zote zingefungiwa.
ReplyDeleteUKITOKA JAPA RUDINI NYUMBANI USA. WENYE WIVU WOTE WATAJINYONGA NA TUTAISHI DUNIA ISIYO NA MAJUNGU.
ReplyDeleteJF ina virusi msiingie.
ReplyDeleteMichu,
ReplyDeleteYaani sijui tuwaite haters au ndio for real these people are that thick(dense)! Yaani wana believe kweli uko "vekesheni" while accompaning the president on an official trip to the USA ! I mean how dumb are these people at Jamii Forums. I believe this is what is called "akili finyu" Pole sana bro. Anyways missed you when you were in DC this weekend maybe next time Azania Bitoz
Huyo aliyeuliza swali kule Jamii Forums kashindwa kuelewa lugha za Issa Michuzi.
ReplyDeleteMichuzi akisema yuko vekesheni maana yake yuko nje kikazi.
Mkuu wa Wilaya...
ReplyDeletePole kwa matatizo, usikate tamaa endeleza libeneke maana huku ndiko tunakopata vitu adimu. JF na wengine hawana mpya, kwani wee kwenda vekesheni sh.ngapi? wamezoea vya kunyonga wakiona umechinja wanajua na wee umenyonga. Ebu waambie umeanza kazi lini na ume-save kiasi gani mpk leo? achana nao wamefulia ramani haoooooo
Kwangua mapipa mkuu waaala usijali. Uzuri ni kuwa unatutupia nasi huo uhondo. Kuna ule msemo wa kizungu usemao- "Let the dogs bark, they can't stop the caravan to move on"
ReplyDeleteKILI
BG
MIMI NIJUAVYO "Vekesheni" litumikavyo na Michuzi, lina maana ya mapumziko. Tena siyo mapumziko bila kazi. Ila mapumziko ya kubadilisha kazi na mazingira kwa muda fulani, kama ziara nk. ambapo unaonana na watu tofauti, unatembelea maeneo tofauti n.k. Hapo kwake kichwa kinapumzika kwa kubadilisha shughuli. Lakini anakuwa kazini kama kawaida, kama vile tu angekuwa TZ.
ReplyDeleteShida yangu ni moja tu. Nikisoma maoni ya Wananchi wenzangu walio wengi (hopefully), ninagundua kuwa sisi tuna mtazamo mmoja usiotofautina kwa jinsi ya kuchambua mambo. Licha ya kuwa mtu wa JF kuwa labda ana wivu, au ana matatizo fulani kimaono nk, kama walivosema wengi, lakini hakuna waliodiriki kuonyesha udhaifu wa upande wa pili wa Bwana Michuzi.
1) Kulikuwa na shida gani ndugu yetu Michuzi kujibu maswali (mapigo) kwa maandishi kama walivyo'mpaka'?
2) Kuna uhakika gani kuwa habari nzima inaongelea matatizo ya Michuzi na si serikali inavyopanga safari ambazo kimsingi hazina faida kubwa sana?
3) Mfano, kungekuwa na hasara gani rais kutosafiri na msururu mrefu ambao umetomia mamilioni ya shilingi za TZ za walipa kodi? Wawekezaji unawafuata kwao badala ya kuwaalika waje wajionee mazingira? Potelea mbali hata serikali ingegharamia safari ya wawekezaji, ingekuwa bora.
4) Waziri wa Mambo ya nje katika safari hii kazi yake ni nini? Kama anaundishwa kazi na JK. Ni lini atakuwa tayari kuiwakilisha TZ bila rais?
5) Je, ni kweli kuwa rais wetu kuwa wa kwanza kuonana na Obama ni sifa kubwa? Does it make sense???
6) Naomab niishie hapa. Nadhani sisi tumekuwa tulivyo sababu hata namna ya kuangalia mambo tunafanana. Hatutaki kukosoana. Hata baraza la mawarizi na serikali, wakimshangilia na kumchekea mkubwa wao wanadhani ndio utendaji wa kazi. Hakuna anayediriki kuzungumzia upande wa pili wa shilingi. Dear fellow Tanzanians, let's not repeat the threads on the obvious, or the already said points..... Everyone is just embracing. What kind of thinking do we have, that makes us all common and the "same"????? Man!
ninachoelewa mtu kama unafanya kazi na ukisave unaweza kusafiri na pili kazi ya michuzi ni kutafuta habari sasa wanaotaka akae ofisini si waelewi... tatu natumaini michuzi ni mshapu wa kupata wafadili wa kuboresha kazi yake. watu wanatakiwa wafanye kazi na siyo majungu
ReplyDeleteNashukuru sana kwa kunitambulisha Jamii Forum...Nimepata mahali pa-kutoa maoni...
ReplyDeleteDuh hii mada imenifungua macho...kumbe bado watu wanafatilia vitu ambavyo haviwahusu moja kwa moja na vinauwauma kiasi hicho?...ila kosa lako michuzi ni kuwa hukuweka mini dictionary kwenye blog kusudi iwasaidie ambao sio wadau waanzilishi...mfano ukisema bwawa la maini wajue ni LIVERPOOL...sasa ukisema vekesheni....sio VACATION na ukisema ukerewe wjue unamaana gani...au utapoteza ladha...no lakini itasaidia kuondokana na huu upuuzi wa huyo aliyeanzisha bifu la kitoto....by the way ofisi ya CAG ipo wazi aandike barua kuomba maelezo ya matumizi
ReplyDeleteWewe kaka Michuzi hebu rudi nyumbani unazurura zurura nini habari nyumbani, Matukio, mambo chungumzima yanatokea nyumbani haupati taarifa zake wala sisi tuliozoea kusoma kupitia blog yako hatupati news zake. PLEEESE. Rais kesharudi nawe rudi haraka. Sioni kitakachokuwa kinakuweka huko tena. Picha za pozi za huko hatuzitaki tena njoo piga picha huko weka pozi bomba katika daraja la Manzese. Kama nawe umempata huko useme mapema sio uje uanze kutaja jina la mwingine ovyo ovyo bora usisalimishe mapema coz tunaona kumekukolea sana huko. NJOOOOO
ReplyDeleteMichuzi,
ReplyDeleteKwanza nirudie tena kukupa hongera kwa mafanikio ya hii Blog yako na kazi kubwa unayoifanya. Mie ni member mzuri wa JF na hii Blog. Baadhi ya wadau wanaotukana hapa na kutukana kule JF kwa kweli inasikitisha sana. Ila tuseme ukweli kuwa JF ni taifa kubwa sana na kule kama ulivyo msafara wa Mamba, basi na Kenge wamo. Sasa Michuzi wee, kuiweka hii mada hapa ili kuanzisha vita na JF, naona kama vile unarusha mawe wakati na wewe unaishi kwenye nyumba ya vioo. Please, ifute hii mada hapa na baadhi ya vitu acha tu viende. Ulichofanya kwa kweli ni kama kuongeza mafuta kwenye moto. Kule JF, waandishi hawajulikani ila hapa WEWE UNAJULIKANA. Kumekuwa na habari nyingi sana kule na watu wakisema kuwa zimetoka kwa NANIHII. JF ina umuhimu wake kwa Taifa na NANIHII ana umuhimu wake kitaifa. Kuna habari BALOZI wetu huwezi ziandika wala kuziweka kwenye blog yako. Ila hata wewe ukitaka, waweza kuziweka kwenye JF bila mtu kujua kuwa ni wewe. Idumu JF, idumu blog ya NANIHII. Libeneke liendelee. Mdau, wako Sikonge wa Sikonge.
Hivi ninyi mnaokaa Ulaya ndo dharau gani kuwaita watanzania wenzenu wanaokaa huku Tanzania eti wala vumbi? Hivi mnafikiri kukaa ulaya ni deal kubwa sana? Si kwamba watu wanaokaa huku hawawezi kukaa Ulaya, ila ni maamuzi tu. Kama ukikaa bongo unatengeneza hela za kutosha una shida gani ya kukimbilia Ulaya?
ReplyDeleteHapa bongo kuna watu kila mwaka wanaenda likizo ulaya na huko Ulaya kuna watu toka waondoke bongo hawajawahi kuja hata kusalimia. Kuna watu huko wazazi wao wamefariki hata nauli ya kuja kuhani msiba wameshindwa. Kuna haja gani ya kukaa ulaya unabeba maboksi na hali ukiwa huku unafanya kazi unapata mshahara wako mzuri. Tuache majungu maana kukaa Ulaya si deal kama wengine wanavyofikia. Wapo wenye mambo safi ulaya na wapo waliochoka mpaka basi huko huko Ulaya.
Mimi nawafahamu watu kibao ambao nimesoma nao wakakimbilia Ulaya, na sasa wanashindwa hata kurudi; Yaani wamefulia ile mbaya mpaka aibu.
Naomba niishie hapo.
Michuzi wewe endelea na starehe zako za Ulaya, labda wa kumlaumu ni JK anaye tembea na crew ya watu hamsini na safari zisizo na tija hata chembe kwa nchi yetu.
NASHURU MHESHIMIWA NANIHII AKA MZEE WA VEKESHENI AKA MICHUZI KWA KUINTRODUCE JAMIIFORUMS. JAMAA WAKO WAZI NA HAWABANII MAONI, NI DEMOKRASIA KWA KWENDA MBELE. MAONI YANAKWENDA INSTANTLY, HAKUNA KUSUBIRI YARUHUSIWE. NAJUUUUUTA KUCHELEWA KUIFAHAMU.
ReplyDeleteASANTE SANA MKUU WA NANIHII KWA KUNIFUNGUA MACHO. JAMIIFORUMS OYEEEE.
yeuwiiii kodi yangu!!
ReplyDeletesiku tutakuwa tu na sie wanasiasa,unabeba delegation iyo ya kufa mtu
maisha ni jinsi wewe utakavo sio watu watakavyo
sasa mboni JK karudi??wewe nanihii je kulikoni?
ni hayo
Jamani, Wachaga wana tatizo gani?
ReplyDeleteNyie wote mnaoitukana JF, Je mwajua kwamba, mwaka jana kuna habari iliandikwa ya kushumshukuru Mwanakijiji na Michuzi kwa kazi kubwa wanaoifanya? MICHUZI ulipewa HONGERA na ASANTE kwa kuisaidia JF wakati imepata matatizo. JF ina watu wa aina kibao. Kila mtu mle ana mawazo yake hivyo kusema JF iko hivi au vile ni makosa. Jamani ukitaka kuburudika, NJOONI KWA MICHUZI. JF inahusika zaidi na mambo ya SIASA ingawa pia yapo ya burudani, dini, mapenzi, miziki, ushauri wa matibabu/daktari, ushauri wa mambo ya computer nk. Wewe uliyeshindwa kuingia JF, tafadhali nenda tena na soma taratibu na kama ukishindwa, basi waandikie mafundi mitambo watakuelekeza. Inatakiwa kubonyeza kwenye "CONTACT" au bonyeza palipoandikwa "join our community today". Idumu JF, idumu BLOG ya nanii eliyepo VAKESHENI.
ReplyDelete__________________________________
http://www.jamiiforums.com/complaints-congrats-advice/10197-hongera-michuzi-na-mwanakijiji-kwa-kazi-nzuri.html
24th February 2008, 06:17 PM
Mwafrika wa Kike
Hongera Michuzi na Mwanakijiji kwa kazi nzuri
Pongezi nyingi sana zimeshatolewa kwa Mac na Mike na wana JF wote kwa kazi nzuri ya kuhakikisha kuwa JF inarudi hewani. Najua pia kuwa watu wengi sana wametoa vote of confidence kwa Mwanakijiji hasa (pamoja na mengine yote) kwa yale mahojiano ya BBC na mengine mengi sana aliyofanya muda wote huu Jf na wanaJF walipokuwa katika matatizo.
Nimekuwa msomaji wa michuzi na blog nyingine nyingi za watanzania kwa muda mrefu. Kwa vile bado hili halijafanyika hapa rasmi, naomba kutumia nafasi hii kumpongeza Michuzi kwa ushirikiano wake na kazi kubwa aliyofanya kuwajulisha wana JF mambo yote bila kinyongo wala ubaguzi. Najua kuna watu hapa wamekuwa wanasema kuwa Michuzi ana upendeleo kwa chama tawala na pia kuwa Michuzi anawabania watu wa nje na longolongo kibao. Naomba niseme hapa wazi kuwa hii si kweli na Michuzi ni Mtanzania mwenye haki na uchungu mkubwa na nchi yake.
Mimi binafsi nimekutana na michuzi katika ziara za Kikwete hapa US. The guy is one of the "ize going guys" from Tz I ever met hapa US ambao huwa kwenye misafara mikubwa kama wa Raisi. Wakati ambapo waandishi wa habari kutoka bongo walivyokuwa wakijitenga na kujifanya bize, huyu Michuzi ali-make sure anaongea na sisi watanzania na kutujulisha mambo mengi sana ya nyumbani.
Michuzi amekuwa anatumia blog yake pia kufikisha malalamiko ya watanzania walioko nje hasa inapokuja issue ya kutuma mizigo na pesa nyumbani. Michuzi amekuwa akiweka mafanikio ya watanzania katika elimu bila ubaguzi wala kinyongo katika blog yake. Hata pale ambapo barabara za nyumbani zinakuwa na mashimo ya muda mrefu, basi blog ya michuzi huweka picha hizo na matokeo yake mashimo hayo hufukiwa.
Ni kweli pia kuwa kuna mambo baadhi huwa hayaweki na kuna maoni ya watu yanabaniwa but ehneeee, hii ni side kick tu kwani yeye si ana kazi yake? mbona sisi hatubuguziwi wakati tukibeba boks zetu?
Hata kama anaweka habari za serikali, kwani huo pia si ni uamuzi wake? Pamoja na haya yote, Michuzi amesaidia sana katika sakata hili la kina Max na naomba nitumie nafasi hii kumpongeza hapa JF.
Ndimi Mdau wa Blog na Member wa JF.
Michuzi,
ReplyDeleteKwanza nirudie tena kukupa hongera kwa mafanikio ya hii Blog yako na kazi kubwa unayoifanya. Mie ni member mzuri wa JF na hii Blog. Baadhi ya wadau wanaotukana hapa na kutukana kule JF kwa kweli inasikitisha sana. Ila tuseme ukweli kuwa JF ni taifa kubwa sana na kule kama ulivyo msafara wa Mamba, basi na Kenge wamo. Sasa Michuzi wee, kuiweka hii mada hapa ili kuanzisha vita na JF, naona kama vile unarusha mawe wakati na wewe unaishi kwenye nyumba ya vioo. Please, ifute hii mada hapa na baadhi ya vitu acha tu viende. Ulichofanya kwa kweli ni kama kuongeza mafuta kwenye moto. Kule JF, waandishi hawajulikani ila hapa WEWE UNAJULIKANA. Kumekuwa na habari nyingi sana kule na watu wakisema kuwa zimetoka kwa NANIHII. JF ina umuhimu wake kwa Taifa na NANIHII ana umuhimu wake kitaifa. Kuna habari BALOZI wetu huwezi ziandika wala kuziweka kwenye blog yako. Ila hata wewe ukitaka, waweza kuziweka kwenye JF bila mtu kujua kuwa ni wewe. Idumu JF, idumu blog ya NANIHII. Libeneke liendelee. Mdau, wako Sikonge wa Sikonge.
Michuzi,
Achana na huyo jamaa anayejiita Sikonge anayeleta mambo ya JF katika globu yetu ya jamii. Huyo jamaa ni mmoja kati ya wale wenye user ID nyingi tu kule JF wanaoandika halafu wanajijibu wenye kwa kifupi wamedata!!!
Huna haja ya kuifuta kwani wao walipoanzisha kule mtaa wa pili walitegemea nini? mbona hawafuti wao kule?
Michuzi tuachie sisi tuwaeleze hao 'wajuaji' kuwa hii ni globu ya wastaarabu na tunaifurahia saaaana kwani haiendeshwi kwa kujificha-ficha, mambo haoa ni hadharani michuzi yupo kwa jina lake halisi.
Huyo jamaa anajidanyanga kuwa watu wanaochangia katika JF hawajulikani, sijui anaishi katika dunia gani, kwa taarifa yako watu wote wanachangia katika JF wanajulikana wote na mahali wanapotumia Kompyuta zao pia panajulikana. Kama wafanyakazi wa serikali na makampuni ndiyo kabisa, wanajulikana na wengi wao wanayoyaandika yanasomwa na wakubwa wao na kuwekwa katika mafaili husika. Hakuna siri katika mtandao JF msidanganye watu.
huyu mpiganaji wetu michuzi anastahili kula kuku for good kwani haya mambo ameyapatia tabu sana na hayakuja bure tu kama tunavyofikiria wengi wetu,mkiongelea mambo ya kula kodi kuna watu wanakula kodi za wavuja jasho mpaka hii leo na hawakulifanyia taifa jambo lolote la maana na watu wamekaa kimyaa,ila michuzi akila watu ndio husema sanaa!michuzi kwa maoni yangu endelea na kazi zako kama kawaida watu kusema ndio kawaida yao.
ReplyDeleteNaona mwanakijiji kaona tuko ngangari kumlinda mkuu wa wilaya wetu sasa anajikomba.
ReplyDeletebalozi tuachie tuwashughulie hawa wajinga watu wakuja.wameiba jina letu na bado wanaleta za kuleta.
Kaka Misupu mbona huyo jamaa alieandika huo upumbavu hatumii hekima na busara kama kweli anania nzuri na wewe si angekufuata akuulize na kama naye anataka safari aombe ni mbinu gani unafanya mpaka unaweza kujilipia safari zako. Ilibidi ajue kuwa wewe ni chuma na sio plastic, kila siku iendayo hewani naamini ni watanzania si chini 10,000 wanasoma blog yako kwa hiyo watu kukualika na kukughalamia safari yako ni kitu kidogo sana. Pili haujawahi kuchangisha michango kuombva usaidiwe ili usafiri sasa yeye kinamuuma nini? Tatu hata kama unafanya kazi sherikalini yeye inamuhusu nini au ndio anataka akuroge Mmmmmhh wabongo tumezidi kuchungulia maisha ya watu, Kaka naomba niwajulishe wadau kuwa wewe sasa ni sawa na OBAMA katika mambo ya habari kula raha kaka na fanya kazi yako wakileta ngebe waambie wapande juu wakazibe.
ReplyDeleteMichuzi hawa watu sidhani kama wanakujua wewe umetokea wapi. Ulianza kazi ya kupiga picha pale YMCA na "Gymkhana Pazi", hawa watu lazima uwaeleze enzi zetu wakati Lowassa anaendesha "VW Bittle" mzee Malai ana dalala Scholastica Mwenge Station, Pazi wamecheza na Al-Ally Mpira wa Kikapu na wewe unapiga Picha Gymkhana na Matiakisi wa motel Agip kauza uwanja wa Gymkhana kwa Wawekezaji hivyo hivyo, Michuzi waulize hawa watu walikuwa wapi. Mimi naona watu wengi hawajue Michuzi kaanza kazi muda gani. Endeleza kuwaelisha wananchi juu ya picha na matokeo.
ReplyDeletekale kajitu kafupi a.k.a mwanakijiji kameweka mada hapo juu tukashughulikie.
ReplyDeleteUnajua wachaga walafi wana matatizo...sio wachaga wote washenzi bali manyangumi waliojiundia NGO inayoitwa CHADEMA ndio wana roho mbaya....tunakufagilia kinoooma ....Tunakukaribisha Stockholm na tutakulipia ghrama zote za vekesheni halafu hao JF wakitaka wanywe sumu
ReplyDelete