wataalamu wanatuambua jua litapatwa mnamo julai 22 mwaka huu ambapo kuna sehemu mbalimbali duniani watashuhudia kupatwa kamili kwa jua. wadau mlio maeneo hayo tunasibiri taswira. maeneo yanayotabiriwa kuwa na kupatwa kamili kwa jua ni India, Nepal, Bangladesh, Bhutan, Myanmar, China, Japan na juu ya Kiribati. Vile vile sehemu za Marshall islands katika bahari ya Pacific.
Sehemu zingine ni Surat, Varanasi, and Patna in India, Thimphu huko Bhutan, Chengdu, Chongqing, Wuhan, Hangzhou na Shanghai huko China. Nchi karibu zote za Kusini Mashariki mwa Asia na visiwa kibao vya bahari ya Pacific. Visiwa vya Iwo Jima Kaskazini ndiko inasemekana wataona kupatwa kwa jua kwa muda mrefu kuliko sehemu nyingine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...