si kweli kwamba kila jengo la zamani dar limepigwa nyundo. mfano mmojawapo ni hili jengo ambalo limepigwa sopusopu na sasa ndio ofisi ya kodi na mapato ya mkoa wa dar

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 09, 2009

    Muhidin,

    Tusipotoshe ukweli. Ukweli ni kwamba majengo yaliyojengwa na Mjerumani yanalindwa na mkataba kati ya Serikali ya Tanzania na Ujerumani. Vinginevyo Majengo ya Ocean Road Hospitali tayari yangekuwa yameshavunjwa na kujengwa au kukarabatiwa kuwa mahoteli, migahawa, au maduka ya kitalii.

    Majengo yaliyojengwa na Mjerumani yanayovunjwa ni yale yaliyokuwa majumba ya kuishi. Mfano nyumba za Oysterbay kuanzia Mtaa wa Laiboni hadi Bwalo la Polisi na zile zinazotazamana na Kanisa la Mtakatifu Peter pale Ada Estate.

    Majengo yanayovunjwa katikati ya jiji na Kariakoo ni yale yaliyojengwa na kumilikiwa watu binafsi hususani Wahindi. Majengo hayo ambayo pia yamekuwa yakimilikiwa na Shirika la Msajiri wa Majumba na yakipangishwa kwa watu binafsi; kama lile la Salamander na yale ya Mtaa wa Zanaki na Indira Gandhi, la kwenye kona ya Mtaa wa Kisutu palipojengwa Haider Plaza. Mawenzi Hoteli na majengo mawili Pale karibu na Daily News palipokuwa Oxford Publishers. Majengo mengine ya kihistoria yaliyovunjwa ni yale yaliyopo mitaa ya Mirambo, Shabaan Robert, Ghana, Garden, na Chimara.

    Ukweli ndiyo huu.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 09, 2009

    Its sad kwa kweli how old buildings are being demolished, wakati yanaweza kuwa renovated to keep the history of our towns and cities...kwa kweli Tanzania tunarich history but slowly inapotea in the name of modernaization!
    Sad!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 09, 2009

    Duh, Jengo limependeza sana aisee, kama wangefanya hivi mpaka mikoani ingekuwa jambo la maana sana. Jamani tusiisahau mikoa yetu,kule nako kuna raia wa nchi.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 09, 2009

    Good! na mengine tunaomba wayapige sopusopu pia.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 09, 2009

    Ni jambo la kufurahisha sana kuona kuwa nyundo zina heshima kwa majengo yenye historia ya nchi.Jamaa kataja majengo ya hospitali ya ocean road, nakumbuka katika jengo moja hapo kuna commemorative plaque of the visit to German East Africa..Tanganyika...of ROBERT KOCH mjerumani mganga maarufu aliyetambua vidudu vya kifua kikuu.
    Misupu tuletee picha, min fadhilak
    Wakatabahu

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 09, 2009

    Mdau wa kwanza asante kwa kutufahamisha siri ya kihistoria. Nilipoona habari hii nilitaka kufanya utabiri kwamba baada ya miaka mitano nyundo itakuwa imeshatembea, kumbe kuna mkataba umewadhibiti wazee wa kazi. Kwa jinsi navyowafahamu watu wetu nina uhakika kwamba kuna watu wanahaha kutafuta namna ya kuuvunja mkataba huo. Time will tell.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...