Home
Unlabelled
msaada tutani
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
MichuziBlogV2Most read Swahili blog on earth
Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.
Waalim ndiyo sahihi na ni neno ambalo limetoka kwenye Kiarabu, na siyo Walimu ... dRU
ReplyDeletehata mie kila siku nikipita hapo naona kichefuchefu,ni Waalimu si walimu,hicho ni kiswahili cha kusema zaidi si kuandika
ReplyDeleteni walimu..kutoka ktk kiarabu siyo tatizo kwani neno lililokopwa hubadilishika..
ReplyDeletemifano:
Kiarabu ni Salaam.
Kiswahili salamu.
Kiarabu ni asubhi()wataalamu waweza kosoa
Kiswahili ni asubuhi.
Anonymous wa kwanza na wa pili nyote ni ma-Idiot inaonekana hata somo la kiswahili hamkulisoma pamoja na huyo mtoa mada mwenyewe.
ReplyDeleteHiki ni kiswahili na siyo kiarabu kumbukeni hata kama maneno mengine yatakuwa yametoholewa kutoka katika kiarabu siyo lazima yatamkwe au kuandikwa kama kiarabu(original).maneno ya kiswahili yanatamkwa ka sauti za kibantu ambazo mizizi yake ni tofauti na kiarabu.
ikiwa WALIMU mnaona ina makosa basi NGE na MBU pia yana makosa!!!kwanini isiwe N'NGE badala ya NGE na kwanini isiwe M'MBU baadala ya MBU?????
What don't you understand? As long you understand, it's not an issue...
ReplyDeletekweli hao wajamaa wasituzingue kiswahili sahihi ni WALIMU,SALAMU, mambo ya AAAAA ni huko nchi nyingine mkifika, huku TZ ni mkato mkato tu single A period....mpo? waharibifu wa kiswahili mwanana nyie ebo! sorry kumbe tuko class..mdau mleta mada tusamehe unajua inauma sana kiswahili kupinduliwa pinduliwa...
ReplyDeleteWed Aug 26, 11:50:00 AM umeanza kwa mbwembwe kumbe wewe ndo sifuri kabisaaa,msaada wako uko wapi sasa bora hao wengine wametoa msaada? kumbukumbu zangu zinaonesha waalimu(sahihi) ni wingi na umoja ni mwalimu,walimu sidhanikama ni sahihi. ndo mawazo yangu
ReplyDelete- mdau uliyeleta mada, unakumbuka mfano wa 'boriti'?..kazi kukosoa wenzako..na wewe 'linanitizaga' ndo nini?..
ReplyDelete-wadau mlong'aka, ile 'kiarabu'ndo imewatia kichefuchefu ama?..mbona dRU amesema sawa tu? - "na ni neno ambalo limetoka kwenye Kiarabu"..asili yake kweli ni kiarabu (ilm/alm). Linaloipa ubantu ni 'w' ('ua'='wa') na ile u ya mwisho: m-W-alim-U..
-ukichukua mfano wa nomino zingine hasa za 'taaluma' za kiswahili zinazoanza na 'a-xxx' na kuleta jina 'mu-a' (= mwa), neno sahihi hapa ni 'waalim-u'..angalia: mwandishi = wa-a-ndishi; mwashi = wa-a-shi;mwasi = wa-asi; mwasisi = wa-asisi; mwandazi = wa-andazi (hii siyo ya mahamri, lol!!!)..walioandika hapo jengoni wamechemsha, warekebishe!..naomba kuwasilisha..
Mie naonaga(bad swahili) kuna wadau wagomvi sana ni wakorofi na ni dhahiri kuwa watafuta sababu wapigane ndondi
ReplyDeleteIf you remove all arabic words from swahili there would be left a bare skeleton, you cant remove all latin words from english
Mwalimu maalim ,salam saalam zote sawa
You say potatoes i say pota"toes you say either and i say.....
Ramadhani karim
Wakatabahu
lugha yetu ya kiswahili imetoka kwa waarabu halina ubishi hili kwiii kwiiiiiiii. Sio tu kukopa ni tumechukia kila kitu
ReplyDeletewaalimu ni wale wanaopenda kukaa mbele kwenye shughuli zinazohusiana na pilau mfano hitma,maulid,vilio,harusi nk lkn hawa ni WALIMU na akiwa mmoja kamwe hatoitwa mwaalimu bali ataitwa MWALIMU kwahio wakiwa zaidi ya mmoja wanaitwa "WALIMU
ReplyDeleteUmoja wa neno 'Walimu' ni 'Mwalimu'. Kwa hiyo, kifungu cha maneno 'Chama cha Walimu' ni Kiswahili sanifu kabisa. Tukumbuke kuwa Kiswahili na Kiarabu ni lugha mbili tofauti na kuazima neno kutoka lugha fulani hakukuzuii kulifanyia mofification mf. progamme na programu, compyuta na computer, n.k
ReplyDeleteBlog ya jamii idumu. Kwa maswali na majibu namna hii, blog yetu si tu kwamba itakuwa inaburudisha, inafariji, inachekesha n.k. lakini vilevile itakuwa inaelimisha yake ili mradi tu majibu yatolewe kwa ustaarabu na si kwa kukejeli!! Blog ya jamii idumuuuuuu.
ReplyDeletejohannes uko sawa kabisa. mchangiaji wa kwanza umesema sawa.
ReplyDeleteIDUMUUUUUUUU NA WADAU WAKE WADUMISHE USTAAARABU MILELE TUWE TUWE TUNACHEKELEA NA KUONGEZA SIKU NA KUJIFUNZA KWA RAHA ZETU, WITO KILA MTU SHANGILIA SEMA IDUMUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUUU.........
ReplyDeletePamoja na kutokana na Kiarabu, lugha za Kibantu, Kiajemi, Kihindi, Kijerumani na lugha nyinginezo, Kiswahili ni lugha inayojitegemea. Umoja wa neno Mwalimu ni Walimu na kamwe si Waalimu. Ni makosa kujaribu kushabihisha lugha kwa namna anayofanya mchangiaji wa mwanzo na wengineo. Yapo maneno mbalimbali kwa mfano gorofa, safina, tarehe, shahwa na kadhalika ambayo yamekubalika katika lugha ya Kiswahili kwa maana kidogo tofauti na yalivyo katika Kiarabu. Kwa hiyo jengo lile ni la chama wa walimu.
ReplyDeleteHere we go..
ReplyDeleteMwanafunzi = Wanafunzi
Mbeba box = Wabeba mabox
Mla vumbi = Wala vumbi
Fisadi = Mafisadi
Mwalimu = Walimu
Mmachinga = machinga
MWARABU = WAARABU
Need I say more?
Hakuna lugha isiyo na maneno ya mkopo (loan words). Kiswahili si hakijatokana na Kiarabu bali kina maneno kiliyotohowa toka katika Kiarabu. Kiswahili mzizi wake ni Kibantu. Tunaposema Kibantu tuna maana ya zile lugha zinazofanana fanana za kuanzia nchi za Afrika ya kati, Mashariki hadi kusini. Kwa mfano,katika lugha nyingi za nchi hizo wanapohesabu kuanzia moja, mbili, tatu hadi nne huwa matamshi ya namba hizo yanafanana. Pia maneno kama Mtu, Mwana, Mama/Mawe/Nyoko, Baba, Shangazi/Sengi, Mungu/Mulungu, Soni/Aibu, Munyu/Chumvi, Maji/Mazi, lia/lela/lila, Kufa/Afwile, Kula/Kulia.
ReplyDeleteTofauti moja kubwa kati ya iswahili na Kiarabu ni kwamba Kiswahili kinanyambulika wakati Kiarabu hakinyambuliki. Kunayambulika ni jinsi neno linavyoweza kupanuka mafano, Shambulia, shambulieni, shambuliana, shambulianeni nk.
kweli wote saumu. mpaka leo hii jumla ya mwalimu hamjui, siamini lakini ukweli ni walimu,
ReplyDeleteHilo jengo nilifikiri linaitwa MWALIMU BUILDING kumbe ni Chama Cha Walimu wa??????
ReplyDeleteKweli nimecheka sana kwa maoni ya wadau.
ReplyDeleteIla baada ya kicheko kwisha ndo nika anza kutafakari, je, kwa maoni ya wadau waliopita tunahitimisha kuwa tunajua kiswahili? Nimeishia kwenye maumivu ya kugundua kuwa kumbe wabongo hatujui kiswahili, lugha inayoaminika kutumika Bongo kwa ufasahaha. TUMENYANG'ANYWA TULICHOKUWA NACHO!
GJK
Katika wadau mliotoa maoni hapa kuna aliyeangalia Kamusi ya Kiswahili Sanifu, toleo la pili kama ilivyotolewa na TUKI inasemaje?
ReplyDeleteMaandishi yanatakiwa kurekebiswa. Neno sahihi hapo ni WAALIMU period.
ReplyDeleteHii mambo ya kusema si umeelewa ni upuuzi mtupu. Elimu muhimu sana jamani achane kuzugazuga tu wabongo, hadi lini?
Mnatia hasira ninyi
Hatusemi walimu wetu bali waalimu wetu, ninyi vipi?
ReplyDeleteUnajua hii inakuwaje? Mkurugenzi kiswahili hajui, bali kwa kuwa ni bosi huamua yote yeye. Watu wanaacha kupeleka kazi hizi kwa wataalu wa lugha hasa wanawaachia mabosi wabishi waamue.
ReplyDeleteWabongo kwa ubishi,sina hamu. Yaani hiyo walimu hata haikai sikioni.
lugha sahihi ni matumizi ambayo wazungumzaji wengi wa lugha wanaelekea kukubaliana kutokana na mazoea ya matumizi. neno 'walimu' ni sahihi zaidi ya 'waalimu'.
ReplyDeleteWacha watu wabishane maana hakuna reputable source online ya kuhakikisha lipi ni neno sahihi.
ReplyDeleteLabda tuwaombe Taasisi ya uchunguzi wa kiswahili (TUKI) nao waamke usingizini watuwekee an online version ya kamusi yao.
Halafu hawa jamaa wanapigania shule za bongo zitumie kiswahili kufundishia wakati hata muda tu wa kuweka hiyo kamusi yao mtandaoni hawana, au ndo wanataka wageuze mradi wa kiuchumi?
Hivi wabongo kweli tutaacha kubishana?
Mzee wa nanihii fikisha hili kwa huyo bosi wa TUKI, tuamshie huyo mtu. Kama wanataka kukuza kiswahili duniani inawabidi waamke na kuutumia mtandao kukinadi kwa kuweka official site ya kamusi ya TUKI. Mwambie aache uzembe.
Kwa nini waingereza hawabishani kama ni teachers au tichazi
Nimeingia website ya University of Dar es Salaam nika search "TUKI" kutoka kwenye search field yao, nilichokipata baada ya hapo kinafuata.
ReplyDeleteSearch Results
Warning: fopen(/home/ududsm/public_html/modules/search/dgssearch.cache) [function.fopen]: failed to open stream: Permission denied in /home/ududsm/public_html/modules/search/libs/utils.php on line 206
Warning: set_file_buffer(): supplied argument is not a valid stream resource in /home/ududsm/public_html/modules/search/libs/utils.php on line 209
Warning: fwrite(): supplied argument is not a valid stream resource in /home/ududsm/public_html/modules/search/libs/utils.php on line 213
Warning: fclose(): supplied argument is not a valid stream resource in /home/ududsm/public_html/modules/search/libs/utils.php on line 214
Search for query 'tuki' found no results. Search took 0.2 sec.
Nikafungua link inaitwa dictionary services nikakumbana na ERROR http://rdu.udsm.ac.tz:50000/dist/download
Sasa nimechemsha wacha watu wabishane tu.
Woote mumekosea, ile iilitakiwa iitwe Maalim.
ReplyDeleteMwalimu - Walimu
ReplyDeleteMifano zaidi....
Mwanafunzi - Wanafunzi
Mwanajeshi - Wanajeshi
Mwanasiasa - Wanasiasa
Mwanakamati - Wanakamati
Kwani wewe MWAALIMU wako wa kiswahili nani? lol.
ReplyDeletehakika tatizo watanzania kila mara ni masihara na ndio tatizo hata penye kuhitaji kupata nuru nyie ni masihara kibao.
ReplyDeletenavyokijuwa kiswahili ni hivi:
walimu hutumika katika shule hivyo ukisema MWALIMU ni mmoja na wengi WALIMU hivyo sawa.
ukija katika dini ya kiislam mwalimu huitwa MAALIMU NA WENGI PIA MAALIMU MFANO MAALIMU WOTE NJOONI HUKU INA BINDI SENTENCE NDIYO IJIELEZE NI KAMA MANENO MENGINE YA KISWAHILI UTALIJUA KUTOKANA NA SENTENSI MAANA HUWA LIN MAANA MBILI MFANO HIKI CHUNGU NI KUZURI KWA KUPIKIA MAHARAGE NA WAKATI HUO HUO HILI CHUNGWA LADHA YAKE CHUNGU KAMA SHUBIRI
Jamani ehh! kulikuwa na kipidi cha kiswahili enzi za Mwalimu radio Tanzania hivi bado kipo huko bongo ? haya yote yasingetokea ...mkishindwa kabisa mkamuone mzee ruksa awasaidie fasta ! hapo jibu ni Waalimu fullu stopu !Chief
ReplyDeleteUmoja wa 'walimu' ni 'mlimu', kama ilivyo watu (mtu), wahindi (mhindi), wabishi (mbishi), wajinga (mjinga) nk.
ReplyDeleteWingi wa nomino yoyote unazingatia mzizi wa neno hilo, kwa hiyo huwa inatangulizwa 'wa' nyuma ya mzizi wa neno, na kama ni umoja inatangulia 'm' iwapo mzizi wa neno unaanza na konsonanti au 'mw' iwapo mzizi wa neno unaanza na irabu(vowel).
Mifano:
-vivu: m-vivu, wa-vivu
-janja: m-janja, wa-janja
-athirika: mw-athirika, wa-athirika
-ajiri: mw-ajiri, wa-ajiri
-alimu: mw-alimu, wa-alimu.
Natumaini imeeleweka sasa kuwa kwa usahihi, wingi wa 'mwalimu' ni 'waalimu'.
kweli we kifimbo cheza umenichekesha na hiyo mifano hai yako sina hamu, tukirudi kwenye mada sahihi hapo ni waalimu, walimu iko veri rafu
ReplyDeleteNyote mliotoa maoni ni vichaa,mnataka kuwafundisha lugha "WALIOWAFUNDISHENI" nyie mpaka mkapata hekima za kuwahoji tena?Anae sema kiswahili ni kiarabu huyo bado ni mtumwa wa Waarabu,kiswahili ni kibantu bwana.Vipo vijineno vichache vya vilivyokopwa uarabuni kama Mwalimu,Hamsini,Mtihani na Mushkeli. Vijineno vingine vimetoka ufaransa kama safari na Nanasi,na vijineno vingine toka kiiengereza kama Shati,soksi na mengineyo,sasa utasemaje kiswahili ni Kiarabu?mshamba weeee rudi darasani,wenzio walipokuwa wakisoma ulikuwa ukiruka madirishani kwenda kupiga chabo!!!!
ReplyDeleteAnaesema Maalim ni sahihi hachelewi kukuambia 3 x 3 = 33 au wingi Umoja wa Chipsi ni Kipsi,umoja wa Vietnam ni Kietinam au wingi wa karakana ni Vyarakana(Wizi Mtupu!)
Nyote mliotoa maoni ni vichaa,mnataka kuwafundisha lugha "WALIOWAFUNDISHENI" nyie mpaka mkapata hekima za kuwahoji tena?Anae sema kiswahili ni kiarabu huyo bado ni mtumwa wa Waarabu,kiswahili ni kibantu bwana.Vipo vijineno vichache vya vilivyokopwa uarabuni kama Mwalimu,Hamsini,Mtihani na Mushkeli. Vijineno vingine vimetoka ufaransa kama safari na Nanasi,na vijineno vingine toka kiiengereza kama Shati,soksi na mengineyo,sasa utasemaje kiswahili ni Kiarabu?mshamba weeee rudi darasani,wenzio walipokuwa wakisoma ulikuwa ukiruka madirishani kwenda kupiga chabo!!!!
ReplyDeleteAnaesema Maalim ni sahihi hachelewi kukuambia 3 x 3 = 33 au wingi Umoja wa Chipsi ni Kipsi,umoja wa Vietnam ni Kietinam au wingi wa karakana ni Vyarakana(Wizi Mtupu!)
Mwalimu Julius K Nyerere
ReplyDeleteau
Maalim Julius K Nyerere.
MAALIM NI KAMA SEIF SHARIFF HAMAD KWAVILE HAJAWAHI KUFUNDISHA JAPO CHECHEKEA ILA MWALIM OFCOURSE NI JULIUS.K.NYERERE MAANA ALISHIKASHIKA CHAKI YLE MZEE
ReplyDeleteUtawajuwa tu watu ambao vichwa vyao vibovu Mwalimu=Kiswahili na Maalim =kiarabu Nyerere kafundisha Seif Shariff Hamad pia Kafundisha Chuo vyote nia mafundisho hata wewe ukiwafundisha Watu wawili au Mmoja kitu chochote unaweza kuwa Mwalimu au Maalim kwa hao watu Wawili au Mmoja sio Lazima mpaka Wakubatize hilo jina kila siku.
ReplyDeleteAnayesema kubishana hakuna aliyebishana Humu ni kufahamishana pengine mwengine atanikosoa mie pia kukosea. Ndio Critic zenyewe sio hahaha. Tunajaribu kufahamishana sio kubishana. Ila mie Maoni yangu binafsi ni Mwalimu ni Mmoja Wengi Walimu au sawa na kusema sehemu Chuo Cha Uwalimu au Ualimu? Pwani Mnajuwa kwamba Mwalimu pia ni Jina tu? Msije Kusikia Mwalimu Mkafikiri Ni Wa Chuo au Madrasa au Chekechea wengine wanapewa majina tu Bagamoyo,Kisarawe,Tanga,Mafia,Rufiji Mwalimu ni jina tu. James.