
Geofrey Kibogoyo
Ndugu wanajumuiya ya Manchester mnakaribishwa katika party ya kumuaga mwanajuiya mwenzetu Geofrey Kibogoyo anayerudi nyumbani moja kwa moja kulijenga Taifa.
Sherehe itafanyika Novemba 7, 2009
saa moja jioni katika address hii
34 Falcon Court,
Old Trafford,
Manchester M15 5QD.
Chakula na kinywaji vitakuwepo kufika kwenu ndio kufanikisha shughuli ya kumuaga mwenzetu ambaye kwa muda aliokuwepo amejitolea kwa hali na mali kufanikisha shughuli za maendeleo ya jumuiya yetu,
karibuni sana
SEMA TU MDAU KASTAAFU KUBEBA BOX SASA ANARUDI BONGO KUPUMZIKA SIO KUJENGA TAIFA.
ReplyDeleteKAMA KUJENGA TAIFA ANAWEZA TU KUJENGA AKIWA HUKO HUKO MANCHESTER. HUKU ATAKUJA TU KUONGEZA IDADI YA WATU KWENYE FOLENI ZA BONGO.
Alikuwa akifanya nini na kwanini anarudi?
ReplyDeletemimi nimeona hiyo picha nikajua jamaa kafa, kumbe nikumuaga ya tutaonana mbele kwa mbele.I hope ana makaratasi ngoma ikidunda bongo arudie boxi lake uk.
ReplyDeletewatu hamkosi yakusema?mwenyewe kaamua kurudi nyumbani for good,kashamaliza kilichomleta uk..tutakuja kukuaga bila kukosa.
ReplyDeletekaka hongera kwa uwamuzi wako wambie na wazee wenzio wasiongopa kurudi home kwani nyumbani ni nyumbani tu, wapo wengi Manchester.
ReplyDeleteuamuzi bora huo mbona AFRICA maisha poa tu pesa yako
ReplyDeleteWabongo haooooo mtu akiamua kurudi nyumbani mwachukia, akikaa huku huku mwachukia jamani tufanyeje? Well, tutakuja tubanane tu hapo....na + sign ni kuwa wawekezaji wakubwa kutoka south wanatupenda kweli kweli hata degree hatuna lakini tukikanyaga tu airport na kazi mkononi tunayo....
ReplyDeleteduh hata mimi nilivyoona picha nikajuwa jamaa "AMESHARUDISHA SEAT NUMBER" JAMANI PICHA ZINGINE ZINATAFSIRIWA VINGINE...MME KAA ULAYA LAKINI MMESHINDWA KUSOMA KWA HILO..?!!!"KWA LUGHA YA WATU NI "BODY LANGUAGE". APART OF THAT , SI VIBAYA KURUDI NDUGU YANGU NIA YAKO NDIO ANAYOJUA MOLA WAKO..KWA HILO SIKUJAJI. MUNGU AKUFUNGULIE...AMIIIN
ReplyDeleteWelcome back ... Na mimi nilikuwa USA nimerudi bongo kitambo na sijuti
ReplyDeleteWaosha vinywa hamumuonei huruma mzee mzima, mnampiga madongo tu. Anyway, chaguo la picha halikuwa zuri, ukijumuisha na kichwa cha habari, wengi tulidhani 'mwingine huyo'!
ReplyDeletewe anony wa 12:12:00 PM umeongea pumba kweli. Eti "body language" katika picha yake inaonesha kuwa amekufa!? Kwani hiyo ni picha ya maiti au? Pumbaavvuuu
ReplyDeletemzee karibu Bongo huku kuna future.mimi mwenyewe nimekaa udengani (denmark)miaka 9 nimeguza majeshi mwaka huu mwanzoni.kuja kutumikia taifa langu na naona sikuchukua uhamuzi mbaya.Ni better asikuwambie mtu.
ReplyDeleteEngineer.Vodacom
VISA YA KUENDELEA KUISHI KUPIGA BOX IMEGOMA NDO MAANA ANARUDI, ASITUDANGANYE. MAANA SIKU HIZI UK BOADER AGENCY NI WAKALI WE ACHA TU!!!
ReplyDelete